Wanasayansi Wafichua Dalili za Mwisho wa Dunia!

Wanasayansi Wafichua Dalili za Mwisho wa Dunia!

Setfree

JF-Expert Member
Joined
Dec 25, 2024
Posts
5,527
Reaction score
7,121
Kama huna habari, wanasayansi wamekuwa wakichunguza mwenendo wa ulimwengu (universe), na matokeo ya tafiti zao yamefichua jambo la kushangaza: ulimwengu hauko tuli, bali unapanuka kwa kasi kubwa sana.

Kupitia uchunguzi wa kina wa anga (astronomy), wamegundua kuwa kuna nguvu ya ajabu inayoitwa dark energy, ambayo ndiyo inachochea upanuzi huu wa ulimwengu. Nguvu hii inaonekana kuwa kubwa kuliko nguvu ya uvutano (gravity), na inaendelea kusukuma galaksi mbali mbali ziachane kwa kasi inayoongezeka kila siku.

Wanasayansi wametoa nadharia kadhaa kuhusu mwisho wa ulimwengu, mojawapo ni ile inayojulikana kama Big Rip. Nadharia hii inaeleza kuwa, kama hii nguvu ya upanuzi itaendelea kuongezeka, itafika mahali ambapo itashinda nguvu zote zinazoshikilia vitu pamoja, kuanzia galaksi, nyota, sayari, hadi atoms zenyewe. Hatimaye, kila kitu kitavunjika na kusambaratika kabisa.

Ajabu ni kwamba, nadharia hizo zinashabihiana sana na yale yaliyoandikwa katika Biblia Takatifu miaka mingi iliyopita. Maandiko yanatueleza kwamba siku ya mwisho inakuja. Siku hiyo mbingu zitateketezwa kwa moto na kutoweka, na viumbe vya asili vitayeyushwa.

Hivyo ni dhahiri mwisho wa ulimwengu unakuja, na utakuwa wa kutisha na wa ghafla.

Yesu Kristo alipokuwa duniani, kabla hajapaa mbinguni, alieleza dalili zitakazotangulia kurudi kwake na za mwisho wa dunia. Dalili hizo ni pamoja na kuongezeka kwa vita na machafuko, matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali, magonjwa hatari na yasiyo ya kawaida, kuongezeka kwa uovu na maasi, upendo wa watu wengi kupoa, watu kupenda fedha kuliko Mungu, kuibuka kwa manabii wa uongo nk.

Tukiangalia dunia ya leo, dalili hizo zinaonekana wazi mbele ya macho yetu. Hata mambo ya kusikitisha yanayoendelea huko Mashariki ya Kati, yalitabiriwa zamani kwamba yatatokea.

Inawezekana kabisa kwamba Mungu, kwa huruma zake, ameruhusu sayansi ithibitishe kwa njia hiyo kwamba mwisho upo ili hata wale wasiopenda kusikia Neno lake waujue ukweli huo.

Ndugu zangu, huu sio wakati wa kubeza wala kupuuza. Ufalme wa mbinguni umekaribia. Huu ni wakati wa kutubu dhambi, kumrudia Mungu kwa moyo wa dhati, kumwamini Yesu Kristo na kumpokea kwa imani mioyoni mwetu awe Bwana na Mwokozi wetu.

Tukifanya hivyo, siku ya mwisho itakapofika, hatutakuwa miongoni mwao watakaolia na kusaga meno, bali tutanyakuliwa hadi mbinguni na kupokea uzima wa milele.

Sources:
  • BBC – Theories about the end of the universe (Big Rip, Big Freeze, Big Crunch)
  • NASA – Research on expanding universe and dark energy
  • Biblia Takatifu – 2 Petro 3:12; Mathayo 24
 
Ndugu zangu, huu sio wakati wa kubeza wala kupuuza. Ufalme wa mbinguni umekaribia. Huu ni wakati wa kutubu dhambi, kumrudia Mungu kwa moyo wa dhati, kumwamini Yesu Kristo na kumpokea kwa imani mioyoni mwetu awe Bwana na Mwokozi wetu.

Amina Mtumishi.

Usingemalizia na hayo maneno ya juu hapo ningejua ID yako imehackiwa.
 
Ukitaka kujua tupo nyakati gani na tunaelekea wapi, tafuta unabii wa tatu na wa mwisho wa Bikira Maria wa Fatma alipowatokea Lucia, Francis na Yasinta, mwaka ule wa 1917. Kati ya mambo makubwa aliyowaambia ni kuwa maafa mengi yatatokea kuanzia mwaka 2020, na yatapata nguvu zaidi kuanzia mwaka 2025, na magumu zaidi yatatokea kipindi cha nusu ya pili ya karne ya 21 (ina maana ni kuanzia miaka ya 2050). Mambo yatakayotokea baada ya mwaka 2050 yanatisha. Tukio mojawapo alilolisema ni kuangamia nusu ya wanadamu ndani ya dakika 1. Na sababu kubwa alisema ni watu kutompokea Yesu Kristo na kutouishi upendo wake. Lucia alipomwambia Papa John Paulo wa pili, alitetemeka, na akasema anaogopa kuutangazia Ulimwengu kwani watu watakata tamaa.

Jambo la muhimu ni kuyaishi mapenzi ya Mungu ambayo yamesimikwa katika Yesu Kristo aliye na utimilifu wa nafsi 2, mwanadamu na Mungu kamili, na ambaye kwa kupitia yeye pekee, wokovu wa Ulimwengu umewekwa.
 
Kama huna habari, wanasayansi wamekuwa wakichunguza mwenendo wa ulimwengu (universe), na matokeo ya tafiti zao yamefichua jambo la kushangaza: ulimwengu hauko tuli, bali unapanuka kwa kasi kubwa sana.

Kupitia uchunguzi wa kina wa anga (astronomy), wamegundua kuwa kuna nguvu ya ajabu inayoitwa dark energy, ambayo ndiyo inachochea upanuzi huu wa ulimwengu. Nguvu hii inaonekana kuwa kubwa kuliko nguvu ya uvutano (gravity), na inaendelea kusukuma galaksi mbali mbali ziachane kwa kasi inayoongezeka kila siku.

Wanasayansi wametoa nadharia kadhaa kuhusu mwisho wa ulimwengu, mojawapo ni ile inayojulikana kama Big Rip. Nadharia hii inaeleza kuwa, kama hii nguvu ya upanuzi itaendelea kuongezeka, itafika mahali ambapo itashinda nguvu zote zinazoshikilia vitu pamoja, kuanzia galaksi, nyota, sayari, hadi atoms zenyewe. Hatimaye, kila kitu kitavunjika na kusambaratika kabisa.

Ajabu ni kwamba, nadharia hizo zinashabihiana sana na yale yaliyoandikwa katika Biblia Takatifu miaka mingi iliyopita. Maandiko yanatueleza kwamba siku ya mwisho inakuja. Siku hiyo mbingu zitateketezwa kwa moto na kutoweka, na viumbe vya asili vitayeyushwa.

Hivyo ni dhahiri mwisho wa ulimwengu unakuja, na utakuwa wa kutisha na wa ghafla.

Yesu Kristo alipokuwa duniani, kabla hajapaa mbinguni, alieleza dalili zitakazotangulia kurudi kwake na za mwisho wa dunia. Dalili hizo ni pamoja na kuongezeka kwa vita na machafuko, matetemeko ya ardhi sehemu mbalimbali, magonjwa hatari na yasiyo ya kawaida, kuongezeka kwa uovu na maasi, upendo wa watu wengi kupoa, watu kupenda fedha kuliko Mungu, kuibuka kwa manabii wa uongo nk.

Tukiangalia dunia ya leo, dalili hizo zinaonekana wazi mbele ya macho yetu. Hata mambo ya kusikitisha yanayoendelea huko Mashariki ya Kati, yalitabiriwa zamani kwamba yatatokea.

Inawezekana kabisa kwamba Mungu, kwa huruma zake, ameruhusu sayansi ithibitishe kwa njia hiyo kwamba mwisho upo ili hata wale wasiopenda kusikia Neno lake waujue ukweli huo.

Ndugu zangu, huu sio wakati wa kubeza wala kupuuza. Ufalme wa mbinguni umekaribia. Huu ni wakati wa kutubu dhambi, kumrudia Mungu kwa moyo wa dhati, kumwamini Yesu Kristo na kumpokea kwa imani mioyoni mwetu awe Bwana na Mwokozi wetu.

Tukifanya hivyo, siku ya mwisho itakapofika, hatutakuwa miongoni mwao watakaolia na kusaga meno, bali tutanyakuliwa hadi mbinguni na kupokea uzima wa milele.

Sources:
  • BBC – Theories about the end of the universe (Big Rip, Big Freeze, Big Crunch)
  • NASA – Research on expanding universe and dark energy
  • Biblia Takatifu – 2 Petro 3:12; Mathayo 24
View attachment 3561406
Wow, Setfree !
Long time no see. How have you been?
 
Hakuna mwisho wa Dunia ila Kuna mwisho wako
Unachosema kina nusu tu ya ukweli. Ni sawa kabisa, kila mtu ana mwisho wake binafsi (kifo), lakini kudai hakuna mwisho wa dunia kabisa ni hitimisho lisilo na ushahidi.

Katika Biblia Takatifu, Mungu ameelezea wazi mambo mawili tofauti: mwisho wa mtu binafsi na mwisho wa ulimwengu. 2 Petro 3:10 inasema: "Siku ya Bwana itakuja kama mwizi; mbingu zitapita kwa mshindo mkubwa, na vitu vyote vitateketezwa."

Hapo hazungumzii mtu mmoja kufa, anaongelea ulimwengu mzima kubadilishwa/kuondolewa.

Pia, Ufunuo wa Yohana 20:11 inasema: "Kisha, nikaona kiti cha enzi kikubwa cheupe, na yule aketiye juu yake. Dunia na mbingu vikatoweka mbele ya macho yake, na havikuonekana tena."

Hii ni lugha ya wazi kabisa ya mwisho wa mfumo mzima wa dunia, sio maisha ya mtu mmoja mmoja tu.

Hata kama wewe ni Atheist na unaikataa Biblia, ziamini basi hizo nadharia za wanasayansi kuhusu uwezekano walioutaja wa mwisho wa ulimwengu. Na kama hutaki kukubaliana na wanasayansi, kubaliana basi hata na Wazee wetu waliotangulia waliosema: "Kila chenye mwanzo kina mwisho" Dunia ilikuwa na mwanzo hivyo lazima itakuwa na mwisho. Ukiendelea kupinga, nakusikitikia kwa sababu utajuta sekunde ya kwanza tu baada ya kuondoka duniani. Na hutakuwa na nafasi tena ya kutubu na kuamini. Soma Luka 16:27–31 ujue yanayotokea mtu akifa.
 
Sisi wakati tunanyoshana 29th-October alitupatanisha nani... Wauwane tu, ni sawa tu...

Cc: Mahondaw
Huwezi kusema hayo kama unapenda kwenda mbinguni mwisho wa dunia ukifika.
Nakazia tena kwa Andiko jingine hili: "Usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema anatoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu."(3 Yohana 1:11)
 
Huwezi kusema hayo kama unapenda kwenda mbinguni mwisho wa dunia ukifika.
Nakazia tena kwa Andiko jingine hili: "Usiige lile lililo baya bali lile lililo jema. Yeyote atendaye mema anatoka kwa Mungu, bali atendaye mabaya hajamwona Mungu."(3 Yohana 1:11)
Wacheeni wanyoshane mpaka akili ziwakae sawa...


Cc: Mahondaw
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom