Wanaoomba kulipiwa mahari Al Hikma wafika 1,000, wapo wanawake, wanatakiwa 50 tu

Swali langu ni kwa hao wanawake,wao si ndo wataja kiwango cha mahari ina maana wameshindwa kutaja msahafu au wametaja kisha wanaume zao wamekosa pesa za kununulia?
Jamani masahafu Ni kitabu kitakatifu lakini huwezi kwenda dukani kununulia unga ukapika ugari tujifunze kufanya reasoning, mwanamke akitaka msahafu sawa lakini yeye ndio ana haki ya kutaja nae ana mahitaji yake yanayotimizwa na pesa tukitumia masahafu nakesho tukikosa pesa ya kula tusomeane masahafu njaa iishe.....tuna manipulate dini Sana.
 
Hio taasisi imewaumbua wengi sana . Mkuu humu Jf tulikua tunaambiwa waislam hamshindwi kutoa mahari maana ni ndogo sana tena hata msahafu tu inatosha na harusi haina mahitaji sana. Sasa haya ya kulipiana mahari ni mageni kwa wengi wetu humu JF
Jamani masahafu Ni kitabu kitakatifu lakini huwezi kwenda dukani kununulia unga ukapika ugari tujifunze kufanya reasoning, mwanamke akitaka msahafu sawa lakini yeye ndio ana haki ya kutaja nae ana mahitaji yake yanayotimizwa na pesa tukitumia masahafu nakesho tukikosa pesa ya kula tusomeane masahafu njaa iishe.....tuna manipulate dini Sana.
 
Hizi mahari inaweza kuwa issue kabisa mpaka mtu kushindwa kuoa?.....

Mkishapendana, waomba mahari unawapiga sound tu kwa kutanguliza hata 10K na nyingine utaleta....ruhusa ya ndoa ikishapita tu imekula kwao.
 
Hio taasisi imewaumbua wengi sana . Mkuu humu Jf tulikua tunaambiwa waislam hamshindwi kutoa mahari maana ni ndogo sana tena hata msahafu tu inatosha na harusi haina mahitaji sana. Sasa haya ya kulipiana mahari ni mageni kwa wengi wetu humu JF
Mahari za waislama kwa ndoa nyingi Ni around 300K hio ni nyingi kwani ??

Simply, Kuna mahari za 400K au tuseme 300K hii still Ni ndogo the same time Kuna kijana anayefanya kazi kiwanda Cha sabuni au pale Pepsi kwa siku wanalipwa 5000/7000 kijana huyu kuweza kukusanya 400K ya pamoja sio jambo rahisi kamwe inaweza pita mwaka mzima, miaka 2 mpaka 3 na ajapata 400K ya pamoja....kwahio kulipiwa mahari hio HAIMAANISHI kuwa hio mahari sio ndogo.

Tukija kwenye mahari kuwa masahafu still Kuna maelfu ya ndoa ya afungwa kwa mahari ya msahafu kila mwaka.

Mbali na kuliangalia jambo hili kwwnyw mahari ila hili jambo la kijamii zaidi sehemu ya waislam kujamiiana pia
 
Siku chache baada ya Taasisi ya Al Hikma kutangaza uamuzi wa kuwalipia mahari vijana 50 ili waoe, zaidi ya vijana 1,000 wametuma maombi wakiwamo wanawake watatu wanaowaombea wachumba zao.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo

Shehe Nurdin Kishki amesema Dar es Salaam jana kuwa saa chache baada ya kutangazwa kwa ofa hivo taasisi hiyo ilianza kupokea maombi.

"Tulipotangaza tu siku ile ya Aprili 9 pale Uwanja wa Uhuru tulianza kupokea simu, kwenye kurasa zetu za kijami, barua pepe maombi ya vijana zaidi ya 1,000 wanaoomba kuozeshwa," alisema Shehe Kishki.

Alisema dirisha la kuchukua fomu za maombi limefunguliwa jana hadi Mei 5 mwaka huu na watakaochaguliwa baada ya kufungishwa ndoa pia watapatiwa semina ya ndoa ndipo watakabidhiwa wake zao.

"Hatutaki ndoa hizi ziishie baada ya fungate kwenye talaka. Ndio maana hatutaki vijana wa kukurupuka tu baada ya kusikia tangazo hili, tumelenga wale wenye nia na shida kweli ya mahari. Tunaamini talaka za vijana zikiongezeka ndio na mmomonyoko wa maadili unaongezeka," alisema Shehe Kishki.

Alisema baada ya taratibu zamaombi na mchujo kukamilika ndoa hizo zinatarajiwa kufanyika baada ya miezi mitatu hadi minne kuanzia sasa.

Ametangaza masharti manane kwa waombaji ili kupata sifa ya kulipiwa mahari na kuozeshwa ikiwemo waombaji kuwa tayari wa-metoa posa na kupangiwa mahari.

Alitaja masharti ya vijana wanaotaka kuingizwa kwenye programu hiyo kuwa ni lazima kijana mwombaji awe Muislamu kwa kuwa ndoa hizo zitafungwa na kusimamiwa na Shehe Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zuberi Bin Ally.

Aidha, alisema sharti lingine ni lazima kijana mwombaji asiwe na mke, awe amejaza fomu maalumu ya maombi, lazima afanyiwe usaili, awe tayari kufunga ndoa ya pamoja Dar es Salaam, awe Mtanzania na lazima athibitishwe na imamu wa eneo lake.

"Hivi ninavyoongea tayari tumeshapokea maombi kutoka nje ya nchi wakiomba kuozeshwa akiwemo kijana Mtanzania anayeishi Misri. Lakini sisi tumewalenga vijana wa hapa nchini na lazima wakidhi vigezo hapo ili fedha isitumike kwa watu wasio na uhitaji," alisema Shehe Kishki na kuongeza:

"Tutalipa mahari, ukumbi, chakula, vifaa vidogo vidogo vya hapa nchini na lazima wakidhi vigezo hapo ili fedha isitumike kwa watu wasio na uhitaji," alisema Shehe Kishki na kuongeza:

"Tutalipa mahari, ukumbi, chakula, vifaa vidogo vidogo vya chumbani na bwana harusi atapewa kadi 20,10 kutoka upande wake na 10 upande wa mkewe kuja kushuhudia ndoa yake hiyo.
Hee.....maajabu haya.
 
Binadamu tunafanya maisha yanakuwa magumu sana, yaani unatoza mahali yakuolewa binti yako kiasi cha kumshinda muoaji matokeo yake anaghailisha na kuoa.
 
Baada ya ndoa kufungwa, na baada ya miezi sita kupita, katika ndoa 50 zitakazo kuwa salama ni ndoa 10 pekee, nazo baada ya miaka miwili kutakuwa hakuna ndoa,
Why:
Nafsi ya muoaji ya dhati na upendo wa dhati huwa haifungwi na mahari,ukizingatia mahari huweza kulipwa kidogo kidogo au awamu kwa awamu.
Tuwaombee mema, ndoa zao zitadumu inshaAllah
 
Ila KIUME, ni bora uende ukweni na kitu kidogo, uwaambie hali tete wakuvumulie upambane kutafuta mahari ukipata utalipa kilichobaki. Hii ya kulipiwa mahari imekaa kiboya sana. Kama umeshindwa kupambana kupata mahari, utaweza kweli kupambana kulisha mke na mtoto? Hata kama mnapendana kiasi gani, mtoto wa kiume kama huna uwezo, huna hela zako, usikimbilie ndoa maana hamtakula penzi lenu.
Ukioa wakati huna uwezo ili utimize masharti ya imani kuna wasamaria wema watakusaidia kukulelea mkeo, na ndio hapo utapiga simu redioni kuomba wimbo wa kisa cha mpemba..
 
Siku chache baada ya Taasisi ya Al Hikma kutangaza uamuzi wa kuwalipia mahari vijana 50 ili waoe, zaidi ya vijana 1,000 wametuma maombi wakiwamo wanawake watatu wanaowaombea wachumba zao.
Mkurugenzi wa taasisi hiyo

Shehe Nurdin Kishki amesema Dar es Salaam jana kuwa saa chache baada ya kutangazwa kwa ofa hivo taasisi hiyo ilianza kupokea maombi.

"Tulipotangaza tu siku ile ya Aprili 9 pale Uwanja wa Uhuru tulianza kupokea simu, kwenye kurasa zetu za kijami, barua pepe maombi ya vijana zaidi ya 1,000 wanaoomba kuozeshwa," alisema Shehe Kishki.

Alisema dirisha la kuchukua fomu za maombi limefunguliwa jana hadi Mei 5 mwaka huu na watakaochaguliwa baada ya kufungishwa ndoa pia watapatiwa semina ya ndoa ndipo watakabidhiwa wake zao.

"Hatutaki ndoa hizi ziishie baada ya fungate kwenye talaka. Ndio maana hatutaki vijana wa kukurupuka tu baada ya kusikia tangazo hili, tumelenga wale wenye nia na shida kweli ya mahari. Tunaamini talaka za vijana zikiongezeka ndio na mmomonyoko wa maadili unaongezeka," alisema Shehe Kishki.

Alisema baada ya taratibu zamaombi na mchujo kukamilika ndoa hizo zinatarajiwa kufanyika baada ya miezi mitatu hadi minne kuanzia sasa.

Ametangaza masharti manane kwa waombaji ili kupata sifa ya kulipiwa mahari na kuozeshwa ikiwemo waombaji kuwa tayari wa-metoa posa na kupangiwa mahari.

Alitaja masharti ya vijana wanaotaka kuingizwa kwenye programu hiyo kuwa ni lazima kijana mwombaji awe Muislamu kwa kuwa ndoa hizo zitafungwa na kusimamiwa na Shehe Mkuu wa Tanzania, Mufti Abubakar Zuberi Bin Ally.

Aidha, alisema sharti lingine ni lazima kijana mwombaji asiwe na mke, awe amejaza fomu maalumu ya maombi, lazima afanyiwe usaili, awe tayari kufunga ndoa ya pamoja Dar es Salaam, awe Mtanzania na lazima athibitishwe na imamu wa eneo lake.

"Hivi ninavyoongea tayari tumeshapokea maombi kutoka nje ya nchi wakiomba kuozeshwa akiwemo kijana Mtanzania anayeishi Misri. Lakini sisi tumewalenga vijana wa hapa nchini na lazima wakidhi vigezo hapo ili fedha isitumike kwa watu wasio na uhitaji," alisema Shehe Kishki na kuongeza:

"Tutalipa mahari, ukumbi, chakula, vifaa vidogo vidogo vya hapa nchini na lazima wakidhi vigezo hapo ili fedha isitumike kwa watu wasio na uhitaji," alisema Shehe Kishki na kuongeza:

"Tutalipa mahari, ukumbi, chakula, vifaa vidogo vidogo vya chumbani na bwana harusi atapewa kadi 20,10 kutoka upande wake na 10 upande wa mkewe kuja kushuhudia ndoa yake hiyo.
Hii kitu iliishaje? Vijana walifanikiwa kuozeshwa?
 
Back
Top Bottom