Wanaomwibia Rais Samia ndio wanalipa vyombo vya habari na mitandao ya kijamii kumsifia anaupiga mwingi! Anawajua?

Resilience

JF-Expert Member
Jan 4, 2023
879
4,125
Watu wale wanaoiba mali za umma, watu wale wale ambao makampuni na maeneo yao ya utawala yamejaa ubadhirifu ndio hao hao wanalipia gharama za vipindi kwenye radio na televisheni wamsifie kwamba anaupiga mwingi.

Watu wale wale ambao anawatumbua kila siku kwa kushindwa kumsaidia ndio hao hao wanapokuwa uraia wanazunguka mitandaoni kumsifia na kuandaa midahalo ya anaupiga mwingi lengo likiwa kuwafanya wasaidizi wake wawarudishwe wakaendelea kunyonya.

Je, wanaomsaidia mama kuongoza wanaona kundi hili linafanya sawa kumpaka mama mafuta kwa mgongo wa chupa? Wanamsaidia vipi mama kuvuka katika kiunzi hiki ambacho hakijawahi kuleta maendeleo endelevu Duniani?
 
Back
Top Bottom