Wanandoa na extended family

Siwezi sema sana maana sijawahi kukaa na extended family..
Ila naamini kwenye kupenda boga na ua lake...

Kama unampenda mumeo sidhani kama uta enjoy kumuoana hayuko happy...maana kama ni yeye tu ndio ametoka kwenye ukoo... unadani atakuwa na furaha kama ndugu zake wanakula mlo mmoja...? Wanaume wengine walilelewa mambo safi ila wazazi wakafa along the way...na mume ndio akabaki jicho...sasa uoni huo ni ukatili kumkataza kuwa close na ndugu zake?

Nina mdogo wangu ni stubborn sana lakini nimemsifu wamemjengea mama mkwe wake nyumba hapa town ili asiendelee kukaa kijijini; that way wame solve tatizo la kutokaa na ndugu maana huyu mdogo wangu ana ukorofi asingeweza. Na si kwamba wana ela kiivyo wamekopa yeye na mumewe...
 
Kidogo kwa ndugu wengine mimi naona wanaume wanaweza kukoroma lakini si kwa mama mzazi,na mama akiongea mfano kama si mimi niliyekubeba miezi tisa utafanya hivi...basi mwanaume hata kama alikuwa na msimamo wote unayeyuka.


Kwa upande wangu sina mtu ambaye anaweza kuingilia familia yangu nikamwacha. Nawashauri wanaume waache woga kwa mama zao kwani ndiyo mwanzo wa matatizo kwenye ndoa zao!
 

Kama hujawahi kuishi na ndugu basi omba Mungu uendelee hivyo hivyo. Ukisikia tunawalaani ndugu usidhani kwamba hatuwapendi au hatuna huruma kwa jinsi wanavyoteseka. La hasha, tumefikia hapo baada ya kuponzwa na hiyo huruma/

Hata kama ungeamua kulala na ndugu zako kitanda kimoja ili waone kwamba unawajali, bado hutaweza kuwaridhisha. Bora wakae kwao na pale unapoweza uwasaidie. Kwani kadri unavyotaka kuwapa maisha yasiyopishana na yako ndivyo unavyoharibu.
 
Kwa upande wangu sina mtu ambaye anaweza kuingilia familia yangu nikamwacha. Nawashauri wanaume waache woga kwa mama zao kwani ndiyo mwanzo wa matatizo kwenye ndoa zao!

Kama ulikuwa kichwani mwangu.
 
Kuna watu roho zao zimening'inia
hawabebeki hata kwa mbeleko ya chuma especially ndugu wa mwanaume make wanaona wameoa ukoo wote
ndugu wa mke huwa hawana nguvu sana wengi wao kulinganisha na upande wa kiumeni
 

Mkuu umeongea kitu cha maana!

Kuchora MSTARI...tena mapema kabisa ni jambo la muhimu sana especially kwa sisi wanaume.

I learned it from my daddy...he was firm and am implementing it squarely. Life partner unamchagua ukiwa mtu mzima na akili zako timamu...but huwezi kuchagua ni dada/kaka ama baba/mama wa aina gani ndo awe family member wako! It just happens tu wakawa wanafamilia wako...BUT a life partner unachagua.
 
Mfumo huo wa kijamaa na undugu umeshapitwa na wakati..... Sehemu nyingi duniani hakuna tena kubebana kama vile mtu anakilema!! maLovers wanaishi wawil na vitoto vyao kama wamezaa!!

Exactly ila kwa family za kitanzania/ africa bado ni ngumu,umetoka tu honeymoon unakutana na msururu wa ndugu wameshajifungasha virago vyao wsnahamia kwako,daah aisee halafu wao ndo wanakua mababa wenye nyumba on behalf of their brother,just imagine,hii niliishuhudia kwa best yangu,tulisimamia ndoa yake sasa siku amerudi toka honeymoon alikuta ndugu wa mume washahamia
 

Vilevile kuna ndugu wanadiriki kwenda kwa mganga kuhakikisha mume anatengana na mke tena ukute ndugu yao ana mali nyingi basi huwa wanahisi.mke anafaidi sana
 
ni kuvumiliana tu no one is perfect,na tusiwe wepesi kushtakishtaki kila kitu vingine ni vya kuachana navyo na kukubali kuwa ni mapungufu ya huyo ndugu,kushtakishtaki sana mwisho wa siku utaonekana wewe ndio mwenye matatizo na si hao ndugu,mwenzako anamjua ndugu yake vizuri kuliko hata wewe,akikufanyia visa na ukawa unam treat vizuri mwisho ya siku atajirudi mwenyewe na kujiona mjinga
 
Mimi sijuhi nina huruma sana au nini? Afu sipendi kuishi maisha ya kushindana kama niko vitani...
Mama mkwe wangu ananipenda kiama na sijuhi nilimtendea nini mie NK maana alikaa kwangu miezi 2 tu...lakini amerudi kwao imekuwa simulizi...tuwapende wakwe zetu jamani watatupenda na sie...yani mpaka mawifi wananipigia simu kunishukuru kwa kumlea mama yao vizuri...

Nilimwambia kabisa HG huyu mama m treat like a queen hata kama sipo...akikooa mpe atakacho...nilimwekea mpaka bill ya maziwa in addition ya ninayowanunulia wanangu...maana alinambia ana vidonda vya tumbo...

Sasa huyu mama mkwe wala hana dhiki lakini alikaa kwa mke mwenzangu cha moto alikiona...kwa kuwa yuko reserved alishindwa kumwambia mwanawe kuwa anataka kuja kwetu hawezi kaa na mkewe...


 
Vilevile kuna ndugu wanadiriki kwenda kwa mganga kuhakikisha mume anatengana na mke tena ukute ndugu yao ana mali nyingi basi huwa wanahisi.mke anafaidi sana

yaah lakini hawa so wengi ukilinganisha name wanawake wanao kwenda kwa waganga kuhakikisha Mume ana tengana au kukorofishana name ndugu.
 

Shukuru dear huyo wako ana moyo wa kuridhika,wangu najitahidi kadri niwezavyo lakini wapi,sichoki na sitachoka nitafanya zaidi.

Alikuwa kwa mke mwenzangu wameshindwana hadi Hg kafukuzwa,nikaona nimchukue na mimi maana kule yalitokea maneno usipime familia nzima ilichafuka,Wifis wakawasha maneno balaa.

Nimejifunza kupitia makosa ya mwenzangu,najitahidi kadri niwezavyo,namtreat kama queen kuliko hata mama yangu mzazi still vijineno bado,navidharau tu kama sioni. Kubwa zaidi yuko hapa kwa matibabu now its six months anasumbuliwa na pressure,hakuna hospital yoyote kubwa ya hapa Dsm hatujaenda,hakuna kipimo hatujampima,vyote yuko safi,kidogo ilionekana ana cholesterol,na vifupa vya shingoni vimejikunja kidogo coz ya umri but Dr. Kasema si shida sana atumie dawa ya kuchua tu na kuna vidonge alipewa,kuna clinics fulani upanga za wahindi nako tumeenda,dawa gani sijui za pressure hajatumia,but leo yuko poa kesho bad unampima pressure unakuta normal tunashindwa hata kuelewa nini kinamsumbua,dakika kacheka dk kazidiwa,mpka sasa nimeacha kwenda hata kazini nimuhudumie maana nikitoka tu hata kama nimemuacha mzima huku nyuma ntapata simu kazidiwa ukipima pressure iko normal au imezidi kidogo tu,nikishinda home no problem. Namuomba Mungu tu anivushe juu ya hili.
 
My dear nyumba kubwa Shukuru huyo wako ana moyo wa kuridhika,wangu najitahidi kadri niwezavyo lakini wapi,sichoki na sitachoka nitafanya zaidi.

Alikuwa kwa mke mwenzangu wameshindwana hadi Hg kafukuzwa,nikaona nimchukue na mimi maana kule yalitokea maneno usipime familia nzima ilichafuka,Wifis wakawasha maneno balaa.

Nimejifunza kupitia makosa ya mwenzangu,najitahidi kadri niwezavyo,namtreat kama queen kuliko hata mama yangu mzazi still vijineno bado,navidharau tu kama sioni. Kubwa zaidi yuko hapa kwa matibabu now its six months anasumbuliwa na pressure,hakuna hospital yoyote kubwa ya hapa Dsm hatujaenda,hakuna kipimo hatujampima,vyote yuko safi,kidogo ilionekana ana cholesterol,na vifupa vya shingoni vimejikunja kidogo coz ya umri but Dr. Kasema si shida sana atumie dawa ya kuchua tu na kuna vidonge alipewa,kuna clinics fulani upanga za wahindi nako tumeenda,dawa gani sijui za pressure hajatumia,but leo yuko poa kesho bad unampima pressure unakuta normal tunashindwa hata kuelewa nini kinamsumbua,dakika kacheka dk kazidiwa,mpka sasa nimeacha kwenda hata kazini nimuhudumie maana nikitoka tu hata kama nimemuacha mzima huku nyuma ntapata simu kazidiwa ukipima pressure iko normal au imezidi kidogo tu,nikishinda home no problem. Namuomba Mungu tu anivushe juu ya hili.
 
Last edited by a moderator:
Wamama wengi wakizeeka wanapenda kudeka; wanakuwa kama watoto hasa wakiwa kwa watoto zao wa kiume...hata mimi mama mkwe huwa analalamika kuumwa lakini akienda hospital hawaoni kitu...kuna doctor mmoja akasema ni uzee...ilikuwa shughuli...kila siku anamlaani yule daktari...ila na miye nilimuona ni careless unajua ukimwambia mtu uumwi ni uzee maanake subiri kufa siku zimeisha...

Mimi kumridhisha nilikuwa nabadili hospitals tu...tena namsaidia kumlaani yule daktari...
Afu wanaume bana mume wangu yeye ni kama hapendi sana mama yake aje aje pale home...lakini at the same time akija nika mtreat vizuri unamwona anvyofurahi...
Nadhani si kwamba hawataki ndugu zao ila wanaogopa conflict na wake zao...wanakupima tu...sasa ukitaka kutumia power vibaya na wewe unapigilia msumari...

Mama yangu yeye yuko dar na ana umri kidogo sawa na mama mkwe ila yeye udongo mzuri bado ana nguvu...basi kuna siku alikuja pale kwangu eti akamshawishi alale pale...wakalala wote chumba kimoja wameshakuwa mashoga...wakashinda wanaongelea twist za sijuhi 1940s wakiwa vijana...its so lovely...mama yangu yeye wala si mtreat kihivyo kwa kuwa ni mwelewa...na wala a mind...

Hila nashukuru hakuwahi kunifanya nisiende job...kwanza kazi yangu hainibani lakini nilikuwa nahakikisha sishindi home...maana ndio mwanzo wa mikwaruzo...tunaonana kwa masaa na kuongea mambo mazuri tu...


 
Hapo kwenye rangi umemaliza kila kitu, na usipokuwa careful unaweza kupoteza hata kibarua maana muda mwingi utakuwa unamshughulikia mama mzaa chema. Kuna rafiki yangu humu tunaongea sana kuhusu haya ya mama mzaa chema wake, jina kapuni, bahati nzuri mwenye mama yake akiona vituko vimezidi anamwambia mama sasa wakati wa kurudi kwako umewadia safari njema. Mama anakuwa hana hili wala lile bali kufunga virago vyake.

 

Ni kweli wangu lakini 56 yrs si kwamba ni mzee kwa umri huu bado sana,mama yangu ni mzee zaidi na ana tatizo kama lake na anaumwa kwelikweli lakini nampatia matibabu kule aliko na si msumbufu wa kiivyo. Nami nilijua kwangu coz nami si mshindaji wa home nilijua tutakaa lakini imekuwa tofauti naona sasahiv anamchukia direct msichana wangu Wa kazi,nimeongea na binti yangu huyo ajitahid avumilie na amtreat vile atakavyo,kule kwa shemej yangu yalikuwa ni kama hivihivi.

Kuhangaika hosp sichoki but kinachoniumiza ni madawa tu anayokunywa ni hatar kwa afya yake,kama ujuavyo unapohamia hosp nyingine unaanza upya,au ile kurudi rudi hosp akilalamika anachoumwa anapewa dawa,loh! Hapa naweza fungua pharmacy kwa jinsi hayo madawa aliyonayo,yani hakuna ugonjwa ambao hatujauchunguza,alipiga hadi MRI but hakuna kitu.Nachoshukuru Mungu kazi hainibani sana but usimamizi wangu ni muhimu sana. Hubby namuona kiasi fulani kachoka lakini najua ni kitu ambacho hawezi kuconfess kwangu.
 

Ni kweli wangu lakini 56 yrs si kwamba ni mzee kwa umri huu bado sana,mama yangu ni mzee zaidi na ana tatizo kama lake na anaumwa kwelikweli lakini nampatia matibabu kule aliko na si msumbufu wa kiivyo. Nami nilijua kwangu coz nami si mshindaji wa home nilijua tutakaa lakini imekuwa tofauti naona sasahiv anamchukia direct msichana wangu Wa kazi,nimeongea na binti yangu huyo ajitahid avumilie na amtreat vile atakavyo,kule kwa shemej yangu yalikuwa ni kama hivihivi.

Kuhangaika hosp sichoki but kinachoniumiza ni madawa tu anayokunywa ni hatar kwa afya yake,kama ujuavyo unapohamia hosp nyingine unaanza upya,au ile kurudi rudi hosp akilalamika anachoumwa anapewa dawa,loh! Hapa naweza fungua pharmacy kwa jinsi hayo madawa aliyonayo,yani hakuna ugonjwa ambao hatujauchunguza,alipiga hadi MRI but hakuna kitu.Nachoshukuru Mungu kazi hainibani sana but usimamizi wangu ni muhimu sana. Hubby namuona kiasi fulani kachoka lakini najua ni kitu ambacho hawezi kuconfess kwangu.
 
Mfumo huo wa kijamaa na undugu umeshapitwa na wakati..... Sehemu nyingi duniani hakuna tena kubebana kama vile mtu anakilema!! maLovers wanaishi wawil na vitoto vyao kama wamezaa!!

Mfumo umepitwa na wakati?? Mhhh hivi mkuu unajua tunaishi nchi gani au umesahau maisha yetu au haujui uchumi wetu na tamaduni zetu?
Unataka kuruka stage ili tuishi kama ulaya??
Acha kuruka stage inawezekana hiyo hatua tutaifikia lakin sio leo wala kesho.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…