Kiboko ya Jiwe
JF-Expert Member
- Apr 7, 2020
- 12,712
- 36,173
Mtu mwenye akili ndogo, mwenye roho ya umaskini ni kama mchawi tu.
Furaha yake ni kuona tajiri anashuka sio yeye kupanda. Maskini wa akili na kipato waliufurahia sana utawala wa Magufuli maana walikuwa wanaamini matajiri wanakomeshwa na wataishi katika wimbi la ufukara kama wao kitu ambacho ni impossible.
Maskini ambaye mwingine hata cheti cha kidato cha 4 hana anapata raha akisikia kuwa boss ambaye ana PhD katumbuliwa, hajui kuwa huyu msomi bado ataendelea kutafuna Kodi zao mpaka afe.
Maskini wa akili na mali anaamini kila tajiri ni mwizi wa mali za umma.
Maskini wa akili na mali waliufurahia sana sakata la vyeti fake, baadaye zahanati zingine zikakosa wahudumu wakafia kwenye mabenchi. Kama mtu ana cheti cha taaluma na anafanya vizuri kulikuwa na ulazima wa cheti cha kidato cha nne? Magufuli aliwaweza sana maskini wa akili na mali.
Viwanda viliyumba na vingine kufungwa, kampuni nyingi viliyumba na zingine kufungwa masking wa akili na mali waliufurahia sana wakasahau kuwa huko sekta binafsi ndiko kunakotoa ustawi kwa wananchi.
Maskini wa akili na mali wanafurahi sana kumwona mtoto wa jirani mwenyewe degree au diploma hana kazi eti kwakuwa yeye watoto wake wote ni wavuta bange na wacheza singeli.
Furaha yake ni kuona tajiri anashuka sio yeye kupanda. Maskini wa akili na kipato waliufurahia sana utawala wa Magufuli maana walikuwa wanaamini matajiri wanakomeshwa na wataishi katika wimbi la ufukara kama wao kitu ambacho ni impossible.
Maskini ambaye mwingine hata cheti cha kidato cha 4 hana anapata raha akisikia kuwa boss ambaye ana PhD katumbuliwa, hajui kuwa huyu msomi bado ataendelea kutafuna Kodi zao mpaka afe.
Maskini wa akili na mali anaamini kila tajiri ni mwizi wa mali za umma.
Maskini wa akili na mali waliufurahia sana sakata la vyeti fake, baadaye zahanati zingine zikakosa wahudumu wakafia kwenye mabenchi. Kama mtu ana cheti cha taaluma na anafanya vizuri kulikuwa na ulazima wa cheti cha kidato cha nne? Magufuli aliwaweza sana maskini wa akili na mali.
Viwanda viliyumba na vingine kufungwa, kampuni nyingi viliyumba na zingine kufungwa masking wa akili na mali waliufurahia sana wakasahau kuwa huko sekta binafsi ndiko kunakotoa ustawi kwa wananchi.
Maskini wa akili na mali wanafurahi sana kumwona mtoto wa jirani mwenyewe degree au diploma hana kazi eti kwakuwa yeye watoto wake wote ni wavuta bange na wacheza singeli.