Wananchi wamemchoka JK?

Kwenye gari mliokuwemo wala amzidi 20 halafu mnataka kuwasemea Watanzania zaidi ya milioni 40. JK chaguo la Mungu, Askofu Kilaini.
 
Jk ni kipenzi cha watanzania nyie mlio kosa urais mkamchukia poleni yeye anawatumikia watanzania nyie mnazoza.
 
Mkuu mwambie na molemo aka t.makene kuwa jk anakubalika sana kuliko unayemheshimu-mzee slaa,jk ni chaguo la mungu na tunaimani naye.
 
Wewe mfumo unakusumbua akuna kiongozi anayependwa na watu wote. Ni ujinga tu ulionao
 
Maoni ya kwenye Dala dala la vibarua hayaakisi mawazo ya watanzania! Kama mnadhani kachokwa turuhusu agombee tena chini ya hii katiba mpya muone watavokula za uso wale watu wenu, jakaya kachokwa Jf sio mtaani, kuna watu wanadhan mawazo ya multiple ID ya jf ndo ya watanzania.
 
Maoni ya kwenye Dala dala la vibarua hayaakisi mawazo ya watanzania! Kama mnadhani kachokwa turuhusu agombee tena chini ya hii katiba mpya muone watavokula za uso wale watu wenu, jakaya kachokwa Jf sio mtaani, kuna watu wanadhan mawazo ya multiple ID ya jf ndo ya watanzania.
Umeshasahau kuwa uchaguzi uliopita tu "alikula ngwala" mpaka akampigia magoti muumini mwenzie Lipumba "aokoe" jahazi.Akigombea 2015 itabidi atembee na mtungi wa hewa ya oxygen,maana itakuwa sio zomeazomea hiyo!!!!
 
Labda kama itatokea kama ilivyotokea kwa Ben, aliongezewa miezi miwili baada ya mgombea mwenza wa chama kimoja kufariki
 
Tumechoka kuongozwa na wagonjwa na mijitu anayozurura hovyo....
 
Akiongezewa miaka miwili kwa ajili ya katiba basi tujue kwamba miaka hiyo yote hatakuwa hapa nchini bali atakuwa hewani muda wote hadi kipindi cha nyongeza kinaisha akiwa ndani ya ndege.
 
Kikwete ni mtu wa watu na ni rais bora sema katiba yetu haitoi fursa ya mtu kuongezewa muda wa urais.

Kwelini bora,maana hatakwa kusafiri tuu keshawashinda maraisi wote Duniani. Ukijumlisha milage unaweza kukuta ashafika mwezini na kurudi. Sasa akiongezewa muda si atafika sayari ya Jupiter?
 
Leo tukiwa tunaenda job asubuhi kwa gari lakzini ( Staff bus) tukawa tunasikiliza dondoo za magazeti mara kikasomwa kichwa cha habari katika gazeti la Raia Mwema chenye muundo wa swali kuwa "JK Kuongezewa muda?" watu karibu wote basi zima wakaguna na kusema "mmmh tena? inatosha!" Mara ukaibuka mjadala humo ndani huku watu wengi wakisema hawataki kusikia hiyo habari.

Swali ni kwamba ni kweli wananchi wamemchoka mheshimiwa kiasi hicho? Na je hali ikoje katika eneo ulilopo?

Hilo ni swali au jibu, binafsi nimemchoka sana lkn raia ktk eneo langu hawataki hata kumwona
 
Nataka niwe mkweli...naumia sana kila nikisimamishwa barabarani na ving'ora kumpisha mtu ambaye amekuwa chanzo cha masikitiko makubwa kwangu na kwa Watanzania wengi. Na hili nalisema kwa kuliganisha haya mawili. Je ni UAMUZI UPI ULIO BORA: Kuacha kusimamia rasilimali za taifa na kudhibiti ufisadi? AMA : kuwapa uhuru wa kusema watakavyo raia kama ishara ya upendo kwao?
 
Kwa khulka zetu watanzania, rais akiwapo madarakani hubezwa sana. Ila aondokapo madarakani 'sisi' hugeuka na kusema, ni afadhali ya aliyepita alikuwa ni kiongozi bora.
Nakumbuka tamthilia ya jinsi mzee Mwinyi na wimbi la ugeni wa mageuzi kidemokrasia ilivyokuwa, ambapo alitusiwa sana na hata kudharaulika hata na wanafunzi lukuki wa UDSM nyakati hizo. Ila alipoondoka tu na mzee Ben kukamata dola...alikumbukwa sana mzee ruksa. Vivyo hivyo kwa mzee Ben alipokuwa madarakani na alipoondoka, na ndivyo inavyokuwa na itakavyokuwa kwa JK baada ya hatamu ya uongozi wake kumalizika.

Hizi ni khulka zetu wanaadam ziwavyo.
 
Kwenye gari mliokuwemo wala amzidi 20 halafu mnataka kuwasemea Watanzania zaidi ya milioni 40. JK chaguo la Mungu, Askofu Kilaini.
Kiongozi yeyote unayemfahamu ni chguo la Mungu ndiyo maana Mungu amesema Kila mtu na aitii mamlaka iliyo kuu; kwa maana hakuna mamlaka isiyotoka kwa Mungu; na ile iliyopo umeamriwa na Mungu.
 
Kikwete ni mtu wa watu na ni rais bora sema katiba yetu haitoi fursa ya mtu kuongezewa muda wa urais.

Lazima uwe unafaidika na uongozi wake,vinginevyo hata leo ,itakuwa bora kuliko kuendelea mpaka 2015.
 
Back
Top Bottom