Wanaharakati: Ziachieni simu za VodaCom!

Wana JF kama kweli ni mwanaharakati uwe makini na VODA kwani ni ya Fisadi RA sasa kama unapanga kukata mirija yake ya unyonyaji atafuatilia kwani Simu zote anasikiliza.Raia kwa Wabunge wanaharakati muachane na VODA msije mkahusika kwenye ajali za kupanga.Maharamia hawa wa ajali za kupanga walipofanikiwa kwa Wangwe sasa wameona ni njia nzuri ya kuwadhuru maadui wao.Hongera kwa aliyetoa Rai ya kuachana na VODA.Mimi naitupa sasahivi na RA ajue ameula wa chuya kwa kufuatilia mawasiliano ya watu.Serikali itaharibu sekta ya mawasiliano kama itawaachia Mafisadi wawe kama mashushushu kwenye mitandao ya simu za mkononi.
 

Ili tufike huko lazima tuanzie harakati zetu mahali fulani hasa pale palipo dhahiri kama...
 
Ili tufike huko lazima tuanzie harakati zetu mahali fulani hasa pale palipo dhahiri kama...
sawa kabisa,hatuwezi kupinga mafisadi wakati tunakula nao.Tukae pembeni tufichue njama zao.
 
voda ni ya wenye uwezo kama mimi,
kama huwezi gharama nenda tigo,

usiniharibie hamu ya kiti moto hapa kona bar!!!
mweeee!
 
Endasuphai Wana Jamii,Habari inoo,Za siku nakubaliana kabisa na Ole Mwanakijiji sasa hivi kama wewe ni (mwanaharakati) na unatumia Mtandao wa Voda wataanza ku-trace simu za watu wote wanaowatilia shaka hasa (wanaharakati) hivyo kaeni chonjo saa mbaya.
 
Du! sasa tufanye nini? Tuache kupiga simu?
 

Hii imetokana na marketing ya Voda. Sio watu kuwa wajinga bwana. Mbona Ulaya kuna hali hii hii kwa upande wa vitu kama maduka, nk. Au utavitofautisha hapo?
 
 
Mwanakijiji amwambie bosi wake Mengi apige marufuku vyombo vyake vya habari kutoa matangazo ya Vodacom kwanza. Ukimalize hilo weka tundiko la kususia Precision air kwa kuwa Mramba ana hisa na ni fisadi.

Bila kusahau wasafiri wote wa ndege watumie Jomo Kenyata airport halafu waje kwa bus kwa kuwa uwanja wetu wa ndege unatumia rada ya mafisadi. Tususie noti za benki kuu kwani huko ndio asili ya ufisadi mkubwa

Pia usisahau kuhamasisha wananchi wasitumie umeme wa IPTL, Dowans, Songas, Kiwira (kama upo ) nk
 


Mkuu Masatu kumbe kweli unajua huo ufisadi upo kama ulivo uainisha mwenyewe hapo juu, isipo kuwa hupendi tu hao mafisadi watengwe/wakwamishwe?


Mimi nadhani kwa vile wote tunawajua hao mafisadi wapo, jithihada yoyote ile ya kuwakwamisha/kuingilia mirija yao ya kuendelea kutufisadi ni ya kuungwa mkono kwa nguvu zote!
 
thanx to Pundamilia and furthermore we have not been given concrete grounds for having to do away with Vodacom do's....
i'll be back
 


hii ni habari?vitisho?mkwara? Wewe kama mwandishi wa siku nyingi wa kijarida na majarida kwa nini usieleze kitu kikaeleweka hata kwa sentence 1 kuliko kutoa vitisho na kuacha habari ina ning'inia itatufanya tuamini hata habari nyingine ni kwa 'bora siku iende'/kusukuma siku mbele au kuchangamsha genge na habari kama hizi ni sensitive sana.
 


Kubembelezwa jama, lazima kwanza kupetpet na kumfagilifagilia, kwa mfano kumwambia mzee safi sana.... tuko pamoja mkuu....wewe ni kichwa sana...kila siku unasema haya.....umeshaandika sana kuhusu....unajua sana....ndio mzee...unayosema ni kweli na kweli tupu....hakuna mwanaharakati zaidi yako....., hilo nalo neno.....

Yanafuata mazungumzo baada ya habari hata kwa PM.
 
Mwanakijiji kawatahadharisha wanaharakati wa KWELI, wanaofahamika kwa kauli na matendo yao kuhusu ufisadi. Sio sisi tunaopinga ufisadi kwa majina bandia!
 
Kwa wale msio kwenye system..viongozi kibao sikuizi wanaongea kwa mafumbo kwenye simu...zinasikilizwa! Watanzania hatujui privacy ni nini tcra wanatuambia tukaregister sim card..kuna thread nilianzisha watu wamechunia..ukweli ndo huo..ata ulaya its not a must to register a sim card!! Kuna mambo yanafanyika na haki zetu kuvunjwa sisi tunabaki kubishana juu ya nia za Mwanakijiji...
 
Mwanakijiji kawatahadharisha wanaharakati wa KWELI, wanaofahamika kwa kauli na matendo yao kuhusu ufisadi. Sio sisi tunaopinga ufisadi kwa majina bandia!

Wildcard,

Kwa nini unadhani JF hakuna wanaharakati wa kweli?

Kuna mbinu nyingi za kupigana vita, si lazima wote tushike bunduki na kwenda mstari wa mbele! Wengine kazi yao inaweza kuwa ni kupeleleza uwezo wa adui na mambo anayokusudia kufanya na si kushambulia!
 
Wachangiaji wanashindwa kuelewa "targeted audience" = Wanaharakati
Mwanakijiji ni mwanadamu, ana madhaifu yake, hisia, vionjo na ushabiki. Lakini katika hili ana ujumbe mzito tena wa Kizalendo. Asiye Mwanaharakati ni kinyume chake na hana haja kuwa na wasi kuendelea kutumia Vodacom maana hana lolote la ki-harakati au ki--mkakati analoweza kuanika wala kupoteza bali kuongeza nguvu ya kiuchumi ya wasio Wanaharakati.
Sikuwepo!
 
SMU,
Najua humu JF pia wamo. Nawashangaa wale wanaomshambulia Mwanakijiji badala kushambulia hoja yake ambayo ina walengwa wake.
 

Wait a minute.... unadai yeye katumia haki yake kutoa maoni na haina kila mtu atakubaliana nae au atapingana nae. Upo sahihi kabisa! and thats exactly wot im doing here... kwani hiyo haki ya "kutoa maoni" ni ya Mwanakijiji tu wengine hatuna?

Kwa taarifa yako na wewe pia umetumia haki yako kutoa maoni na kuna watakaokuunga mkoo na watakao kupinga ndio maana ikaitwa public forum.

Baada ya kusema hayo wewe endelea kutoa maoni kwa uhuru nami niache niji nafasi
 
tukisusia voda tuamie mtandano upi? mzee MM tafadhali nahitaji ushauri wako?
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…