- Source #1
- View Source #1
Rais wa Sudan Kusini, Salva Kiir Mayardit alitokwa na mkojo iliyolowesha suruali yake wakati wa kuimba wimbo wa Taifa kabla ya kuzindua mradi mpya wa barabara, Jumanne Desemba 13, 2022.
Video ya tukio hilo ilisambaa na kukawa na uvumi kuwa waandishi waliokuwa na rais Kiir siku hiyo wameuawa na wengine wamekimbilia Kenya.
Video ya tukio hilo ilisambaa na kukawa na uvumi kuwa waandishi waliokuwa na rais Kiir siku hiyo wameuawa na wengine wamekimbilia Kenya.
- Tunachokijua
- Mbali na Sudan Kusini kuwa na mazingira magumu ya wanahabari, waandishi waliokuwa na Rais hawajathibitishwa na mamlaka za nchi hiyo kuwa wamepotea.
Umoja wa Wanahabari wa Sudan Kusini walitoa waraka ukionesha kuwa hakuna muandishi aliyewekwa jela au kuuawa au kupotea baada ya tukio hilo kutokea.
Uchunguzi wa JamiiForums umebaini kuwa picha ya mtu aliyejinyonga ambayo inamtaja mtu huyo kuwa ni mwandishi aliyerekodi video ya Rais si sahihi. Mtu huyo alijinyonga mwezi Agosti 2022 hivyo hahusiki na taarifa inayonasibishwa naye na wala hakuwa mwandishi wa habari.