Jamani huku sasa ni kwenda mbali sana. Pamoja na kwamba tumepewa uhuru wa habari, lakini ni hekima kuutumia uhuru huo kwa mambo ya maana na mambo ya kweli. Jakaya si mtu wa kufanya mambo kama haya hata kidogo. Andikeni vitu vya maana na vyenye kufundisha jamii, acheni kuandika uzandiki, umbea na uwongo wenye nia na lengo la kupotosha umma. Ningekuwa na uwezo wa kumshauri Raisi kikwete ningemwambia aondoe uhuru wa habari haraka sana ili kuokoa jamii kudanganywa kwa habari mbovumbovu kama hizi.
JK siyo mtu wa visasi na siyo mtu wa kuendesha ofisi kimajungu na fitina watu hawajamuelewa ndiyo maana wanavumisha kwamba yeye ndiyo alikuwa anamchafua Dr Salim na Sumaye kwa njia za propaganda na magazeti ili aweze kupita yeye kuwa Rais, na wengine wanavumisha kwamba ni mbinafsi anashirikiana na watu katika kufanya maovu lakini akipata tu anachokitaka anakugeuka hata kama itamaanisha uawe au ufe kisiasa kama inavyodaiwa kamgeuka Lowassa, kwahiyo na hisi hata hii wanafunzi siyo kwamba analipiza kisasi na wengine wanaenda mbali kwamba katika kipindi chake swala la udini lipo juu sana kutokana na uwezo wake mdogo wa kuongoza nchi hivyo kuamua kuingiza propaganda za kidini kama defensive mechanism
Kuna tetesi zilizoenea huku mtaani na pale UDSM kwamba hii fukuza fukuza ya wanafunzi ni malipizi ya JK baada ya kuzomea alivyoenda kupewa degree ya heshima. Inasemekana Museven alimuuliza JK "hawa wanaokuzomea unawalipia ada?" JK alijibu "ndiyo" Museven aliendelea "ingekuwa Uganda ningewafukuza wote hawa na kudahili wengine"...Je inawezekana JK alifuata ushauri wa Museven? Maana wanaomjua wanadai ni mtu wa visasi sana. Nawasilisha.
tumeshakuzoea hapa JF, wewe ndie mdaku wa kwanza. Kwani nani amesema Shigongo ni mdaku? mbona una majungu we mzee?Huo ni udaku. Mpelekee Shigongo.
JK siyo mtu wa visasi na siyo mtu wa kuendesha ofisi kimajungu na fitina watu hawajamuelewa ndiyo maana wanavumisha kwamba yeye ndiyo alikuwa anamchafua Dr Salim na Sumaye kwa njia za propaganda na magazeti ili aweze kupita yeye kuwa Rais, na wengine wanavumisha kwamba ni mbinafsi anashirikiana na watu katika kufanya maovu lakini akipata tu anachokitaka anakugeuka hata kama itamaanisha uawe au ufe kisiasa kama inavyodaiwa kamgeuka Lowassa, kwahiyo na hisi hata hii wanafunzi siyo kwamba analipiza kisasi na wengine wanaenda mbali kwamba katika kipindi chake swala la udini lipo juu sana kutokana na uwezo wake mdogo wa kuongoza nchi hivyo kuamua kuingiza propaganda za kidini kama defensive mechanism
Na BUKOBA kuna wafunzi 5 wamefukuzwa shule walihudhuria kongamano liliandaliwa na CDM wamefukuzwa hii serikali ni nuksi