Wanafunzi waliofukuzwa UDSM ni mkono wa JK

hata baadhi ya wale walinzi wetu (polisi) walisha waambia wanafunzi kuwa "subirini yatakayo wakuta, hamuwezi kumzomea mkuu (JK)". kwahiyo hili hata mimi nakubaliana nalo
 
Kuna tetesi zilizoenea huku mtaani na pale UDSM kwamba hii fukuza fukuza ya wanafunzi ni malipizi ya JK baada ya kuzomea alivyoenda kupewa degree ya heshima. Inasemekana Museven alimuuliza JK "hawa wanaokuzomea unawalipia ada?" JK alijibu "ndiyo" Museven aliendelea "ingekuwa Uganda ningewafukuza wote hawa na kudahili wengine"...Je inawezekana JK alifuata ushauri wa Museven? Maana wanaomjua wanadai ni mtu wa visasi sana. Nawasilisha.

Jamani huku sasa ni kwenda mbali sana. Pamoja na kwamba tumepewa uhuru wa habari, lakini ni hekima kuutumia uhuru huo kwa mambo ya maana na mambo ya kweli. Jakaya si mtu wa kufanya mambo kama haya hata kidogo. Andikeni vitu vya maana na vyenye kufundisha jamii, acheni kuandika uzandiki, umbea na uwongo wenye nia na lengo la kupotosha umma. Ningekuwa na uwezo wa kumshauri Raisi kikwete ningemwambia aondoe uhuru wa habari haraka sana ili kuokoa jamii kudanganywa kwa habari mbovumbovu kama hizi.
 
huo mkono unaweza kuwa na ukweli ndani yake kwasababu hata baadhi ya walinzi wetu (polisi) wanasema hivyo huku mitaani kwetu. bahati mbaya sasa wengi wa wanaofukuzwa si wahamasishaji wa mgomo.
 
Na BUKOBA kuna wafunzi 5 wamefukuzwa shule walihudhuria kongamano liliandaliwa na CDM wamefukuzwa hii serikali ni nuksi

Kama hii nikweli niwazi kwamba ccm haiwezi achia madaraka hata kama itashindwa uchaguzi kwa 98% na chama chochote,vinginevyo tujifunze kujitoa muhanga kama wenzetu wa nchi za uarabuni
 
Kosa la wanafunzi UDSM: Kosa kubwa la kimkakati walilolifanya ni kufanya fujo kama za kuvunja vioo vya magari na uharibifu mwingine. Kwa msomi wa chuo kikuu, hili ni kosa kubwa sana. Mbona UDSM imewahi kufanikiwa sana ktk madai yao kwa kuandamana tu pasi kufanya fujo? Imeenda wapi hiyo UDSM? Imetoka wapi hii UDSM ya kuvunja mageti? Mkiandamana au kugoma kwa amani hamtasikika? Hapa ndipo wanapofanya "wabaya" wenu wawape jina baya.

Kosa la uongozi wa Chuo: Mara kadhaa, Prof. Mkandala amenukuliwa akikiri kwamba suala la mikopo lina matatizo sana. Hili hata viongozi wakuu wa serikali wamelisemea na ndio maana tume iliundwa kutafiti njia/namna bora ya kutoa mikopo. Sina tatizo sana na uamuzi wa chuo kuwafukuza wanafunzi, tatizo ni pale uongozi wa UDSM unapotaka hao wanafunzi wasisome tena VYUO VYA UMMA na wasipate mkopo wa serikali tena. Adhabu kali na katili kama hizi ni za kikoloni, hazipaswi kutumika miaka 50 baada ya uhuru. Inaturudisha nyuma kipind cha "ujima" ambapo jamii zetu zilitupa watoto waliozalia na ulemavu na kutoa kafara watu.

Adhabu hii sio ya kisomi maana haimpi mwanafunzi nafasi ya kujirekebisha na kufuata "mkondo mwema" hapo baadae. Ni adhabu ya kukomoana. Hawa maprof. wa seneti na council walipaswa wawe walezi wa kimaadili wa wanafunzi hao na sio kufanya kazi kama roboti au jasusi fulani.
 
Jamani huku sasa ni kwenda mbali sana. Pamoja na kwamba tumepewa uhuru wa habari, lakini ni hekima kuutumia uhuru huo kwa mambo ya maana na mambo ya kweli. Jakaya si mtu wa kufanya mambo kama haya hata kidogo. Andikeni vitu vya maana na vyenye kufundisha jamii, acheni kuandika uzandiki, umbea na uwongo wenye nia na lengo la kupotosha umma. Ningekuwa na uwezo wa kumshauri Raisi kikwete ningemwambia aondoe uhuru wa habari haraka sana ili kuokoa jamii kudanganywa kwa habari mbovumbovu kama hizi.

hizi ndiyo tetesi zilizopo mtaani, tueleze basi jamii inadanganywa vipi? Na kwanini unafikiri kwamba hawezi kufanya hivyo.
 
Sawa wamewafukuza lakini tunaamini msg imefika kwa jamii na serikali ya Jk, lazima kuna kitu wamejifunza. Ukombozi hauji hivihivi ni lazima wengine wajitoe mhanga, au mnataka waatanzania wakionew wanyamaze kama makondoo................ukombozi utafika tu
 
kama kweli uko mkono wa baba Rizone basi hilo no suala la visasi visivyo na msingi. kikubwa ni pale serikali inapotekeleza maswala ya kuwafukuza wanachuo kwa sababu tu wanadai haki yao hili hali wanakaa kimya kwa watendaji wa serikali kama akina Luhanjo, Jairo, Ludovic Utoh na wengine wengi waliofanya wizi na kugunduliwa tume za bunge bila kuchukuliwa hatua zozote. kuwafukuza na kuwafungia wasidailiwe popote pale hapa nchini ni kuwanyima haki zao za msingi za kupata elimu. Prof Mukandara ni mtekelezaji wa amri zinazotolewa na viongozi wa juu serikalini ili tu kulinda maslahi yake na wale waliomuweka hapo alipo. Yeye Prof MUKANDARA ni janga la Taifa kama yalivyo majanga mengine. Kama kosa ni kuharibu mali za chuo wangeaadhibiwa kutokana kosa lenyewe kutegemeana na gharam za mali halisi iliyoharibika. Hivi kosa wlilofanya wanafunzi hawa lina ghrama kiasi gani kwa Taifa ukilinganisha na wizi wa wazi uliofanywa na akina Luhanjo. Tunatumia visingizio vya kuvunja amani ya nchi wakati wavunjaji wa amani niwao wenyewe waloiko madarakani kutokana na matenda yao. Tunasema tutasimama kidete kutetea Taifa letu kwa gharama yoyte ile na wala hatutorudi nyuma. Wao wana POLISI na SILAHA na sisi tuna HIKI na MUNGU.
 
Bahati mbaya sana UDOM walipogoma na chuo kufungwa UDSM waliwabeza sana kuwa mgomo wa ktoto usio na madai ya msingi. Na hata waliporudshwa baadhi ya wanafunzi UDSM walibeza eti Waliorudi ni wasaliti eti walitakiwa wagome kushinikiza wenzao warudishwe,Sasa wangegomaje wkt hamna mtu wa kuwaunganisha, serikali yao yote imefukuzwa na chuo,.LEO hii UDSM Wanaface a challenge ya kutowasaliti wenzao 50 waliofukuzwa. Tabia ya UDSM ya kujitenga na kujiona wao ni bora zaidi ya wanachuo wenzao, kwamba kila wanalofanya wao ni sahihi hata kama si sahii.
Nawakilisha.
 
wakati wa kupiga kura kipindi cha uchaguzi wa 2010 wanafunzi hawahawa wa mlimani walifanyiwa mtima nyongo ili wasiweze kupiga kura kama haki yao ya msingi. Leo hii wanafukuzwa ili kunyamazisha harakati zao za kupapmbana na kudai haki. This is another ting bom na hawtaishia hapo wataenda mbele kupambana kama akina Mbatia waliofukuzwa chuo kipindi cha mzee waw RUKSA. tunaamini watakuja na tutawapokea kama mashujaa kwa kujitoa mhanga kwa ajili ya wengine. WAKATI WA UKOMBOZI NI SASA
 
pasipo kuangalia wao wanawajenga hawa wanafunzi kijamii japo si kielimu kutokana na kuwafukuza bila kuangalia adhari zake baadae.
 
Kama aliweka kisasi na BÅBU SEYA, atashindwaje kuweka kisasi na sisi wanaUDSM?
 
Kufukuzwa chuo si mwisho wa maisha yako ingawa nasikia mkandala na jeikei wamekubaliana kwamba hao wanafunzi waliofukuzwa wasidailiwe na chuo chochote hapa nchin,ila wapigane watatoka tu kwani utafiti unaonyesha college/university drops-out wamefanikiwa sana kimaisha. "Wako wapi walionicheka shuleni nilipofeli? Pilika zangu mtaani zimenifikisha mbali,93 nipo boda naitafuta south africa,leo najichanganya tu america ndivyo maisha yanachange leo nipo ndani ya terrano,kesho vx au range"-SUGU
 
Hapa JK wala si wa kulaumiwa. Tatizo ni moral compass ya Prof Mukandara tu. Yeye kama mzazi anapaswa kufikiria walichogomea hao watoto ni cha msingi, ila navyofahamu, kama siyo yeye basi wanawe au wajukuu zake watakuja kukutana na mkono wa hao walioathirika na ndiyo watakapo tambua kuwa kumfukuza mtu chuo si jambo la maana. Unajua hao vijana waliofukuzwa wanaweza kwenda kujitoa muhanga na kumuua? Inauma sana jamani, maana maisha ni magumu, shule ndiyo inapaswa itoe unafuu kwa hao vijana, then wanawafukuza, ni taifa gani hili? Yaani viongozi wa Tanzania ni wabinafisi sana, hawapendi wenzao wapate maendeleo, ni sawa na hao waliowafutia matokeo darasa la saba, wanataka waende wapi? kwa nini hao watoto darasa la saba wasifundishwe maadili (ethics) ya kuibia mitihani? kwa sababu naamini wao na walimu wao pia hawafahamu, tena usikute waalimu ndiyo wachochezi wa kuvujisha mitihani, then leo wanaadhibiwa tu hao watoto, je wahusika wakuu? Bongo ujinga mtupu!
 
Back
Top Bottom