lifeofmshaba
JF-Expert Member
- Feb 19, 2011
- 867
- 219
- Thread starter
- #21
Hii kitu hii, itauwa wengi.
mkuu alisema mzee rukusa hiyo ni sukari, ikiingiwa mdudu au vinyongo itamaliza wengi
Hii kitu hii, itauwa wengi.
Hii kitu hii, itauwa wengi.
I dought hata kama ni kweli Mwalimu alitaka kumbaka au ni set up.
Hainingii akili kuwa Jean alipeleka maelezo ya maandishi kwa mwalimu nyumbani kwake tena usiku. My take ni kwamba kama kulikuwa na dalili za kumtaka kimapenzi huyo mwanafunzi basi Jean atakuwa alishaona hizo dalili na kwamba swala la kwenda nyumbani kwake usiku lingekuwa la hatari kwa maana ya exposure kwake? Nadhani kwa mwanafunzi kiwango chake asingefanya hivyo hilo linawezekana tu kama alipanga kumset huyo mwalimu...just speculating.
Adaiwa kutaka kumbaka mwenzao
Ni mwalimu wao wa nidhamu
Wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Bulongwa kilichoko Wilaya ya Makete mkoani Iringa, wamemuua kwa kumshambulia kichwani mkufunzi wa chuo hicho, Dk. Jumbe Mafingo, kwa madai ya kupinga jaribio lake la kutaka kumbaka mwanafunzi mwenzao.
Taarifa za awali za makachero wa polisi zilieleza kuwa mkufunzi huyo aliuawa baada ya kutuhumiwa kwamba alitaka kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi wa kike, Jean Laison Mwakabuta kwa kutaka kumbaka.
Tukio hilo la kuuawa kinyama kwa mkufunzi huyo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, lilitokea juzi usiku nyumbani kwake mjini hapa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, Dk. Mafingo alifikwa na umauti baada ya mwanafunzi huyo kuamua kwenda nyumbani kwake usiku ili kumkabidhi maelezo yake ya kimaandishi kuhusu sababu zilizomfanya alale nje ya chuo.
Ilielezwa kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye nyumba ya mwalimu huyo, mwanafunzi huyo alianza kupiga kelele kuwa anabakwa.
Alisema kufuatia kelele hizo, wanachuo wengine waliamka katika vyumba vyao na kwenda hadi eneo la tukio na kuanza kumshambulia kichwani mkufunzi huyo hadi kumuua.
Kamanda Mangalla alisema Dk. Mafingo aliuawa kwa kushambuliwa na kitu kizito kichwani.
Huyu Jean Laison Mwakabuta, aliambiwa na Dk. Mafingo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, aandike maelezo ya maandishi kwa sababu gani alilala nje ya chuo,...baada ya kuandika maelezo hayo, aliamua kuyapeleka nyumbani kwa mkufunzi huyo usiku, sasa baada ya kugonga mlango na hatimaye akaruhusiwa kuingia, alianza kupiga kelele kwamba anabakwa na ndipo wanafunzi wenzake waliposikia kelele wakaamka na kukimbilia eneo hilo na kumshambulia mkufunzi huyo hadi kufa, alisema Kamanda Mangalla.
Ilidaiwa kuwa siku moja kabla ya tukio hilo, uongozi wa chuo hicho cha Bulongwa ulitoa ridhaa kwa wanachuo wote kwenda kutembea nje ya chuo kwa lengo la kuwapunguzia msongo wa mawazo ya masomo na Jean Laison Mwakabuta hakurejea chuoni hadi siku iliyofuata.
Kamanda Mangalla, alisema wanachuo wanne akiwamo mwanafunzi Jean, wametiwa mbaroni kuhusiana na mauaji hayo.
CHANZO: NIPASHE
maoni: hivi watu wanashindwa kuoa wake zao wa halali, naona kina dada nao wameshituka sasa
Safi sana tablet....
There is more inside story kuliko hiyo
jiulize kwa culture ya bongo, tena vijijini kama Bulongwa, inakuaje mtoto wa kike aliyelala nje ya shule anakwenda kwa mwalimu wa nidhamu ambaye alikua mnoko sana shuleni billa woga?
Huyu mwalimu kwa nini alifungua?
How long didi it take from binti kuingia ndani hadi kelele?
Inakuaje wanafunzi wote wawe tayari ready and armed kumvamia mwalimu?
Tuelewavyo sisi, ni kwamba hii kitu ilisukwa na ina mtu mwingine ambaye si mwanafunzi ana atajulikana very soon
Adaiwa kutaka kumbaka mwenzao
Ni mwalimu wao wa nidhamu
Wanafunzi wa Chuo cha Uuguzi cha Bulongwa kilichoko Wilaya ya Makete mkoani Iringa, wamemuua kwa kumshambulia kichwani mkufunzi wa chuo hicho, Dk. Jumbe Mafingo, kwa madai ya kupinga jaribio lake la kutaka kumbaka mwanafunzi mwenzao.
Taarifa za awali za makachero wa polisi zilieleza kuwa mkufunzi huyo aliuawa baada ya kutuhumiwa kwamba alitaka kumdhalilisha kijinsia mwanafunzi wa kike, Jean Laison Mwakabuta kwa kutaka kumbaka.
Tukio hilo la kuuawa kinyama kwa mkufunzi huyo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, lilitokea juzi usiku nyumbani kwake mjini hapa.
Kwa mujibu wa Kamanda wa Polisi Mkoa wa Iringa, Evarist Mangalla, Dk. Mafingo alifikwa na umauti baada ya mwanafunzi huyo kuamua kwenda nyumbani kwake usiku ili kumkabidhi maelezo yake ya kimaandishi kuhusu sababu zilizomfanya alale nje ya chuo.
Ilielezwa kuwa muda mfupi baada ya kuingia kwenye nyumba ya mwalimu huyo, mwanafunzi huyo alianza kupiga kelele kuwa anabakwa.
Alisema kufuatia kelele hizo, wanachuo wengine waliamka katika vyumba vyao na kwenda hadi eneo la tukio na kuanza kumshambulia kichwani mkufunzi huyo hadi kumuua.
Kamanda Mangalla alisema Dk. Mafingo aliuawa kwa kushambuliwa na kitu kizito kichwani.
Huyu Jean Laison Mwakabuta, aliambiwa na Dk. Mafingo ambaye ni mwalimu wa nidhamu chuoni hapo, aandike maelezo ya maandishi kwa sababu gani alilala nje ya chuo,...baada ya kuandika maelezo hayo, aliamua kuyapeleka nyumbani kwa mkufunzi huyo usiku, sasa baada ya kugonga mlango na hatimaye akaruhusiwa kuingia, alianza kupiga kelele kwamba anabakwa na ndipo wanafunzi wenzake waliposikia kelele wakaamka na kukimbilia eneo hilo na kumshambulia mkufunzi huyo hadi kufa, alisema Kamanda Mangalla.
Ilidaiwa kuwa siku moja kabla ya tukio hilo, uongozi wa chuo hicho cha Bulongwa ulitoa ridhaa kwa wanachuo wote kwenda kutembea nje ya chuo kwa lengo la kuwapunguzia msongo wa mawazo ya masomo na Jean Laison Mwakabuta hakurejea chuoni hadi siku iliyofuata.
Kamanda Mangalla, alisema wanachuo wanne akiwamo mwanafunzi Jean, wametiwa mbaroni kuhusiana na mauaji hayo.
CHANZO: NIPASHE
maoni: hivi watu wanashindwa kuoa wake zao wa halali, naona kina dada nao wameshituka sasa
Inawezekana kabisa kuwa wanafunzi walishajipanga kumsaidia mwenzao. Nasema hivyo kwa kuwa mimi pia nilishakuwa mwanafunzi. Ila kujipanga huko kunaweza kukawa ni sababu ya mwalimu kumtaka huyo dada apeleke barua nyumbani kwake. Huyo mwanafunzi yawezekana amewambia wenzie mwalimu kanambia nipeleke barua home kwake usiku. Wenzake wakamwambia nenda, akitaka kukubaka piga kelele tutakuja kumtia adabu! Kwa nini akupokea barua nje na kumwacha mwanafunzi aende zake? AU kama ni mwalimu wa nidhamu na anajua nidhamu kwa nini akumtimua na barua yake ili aipeleke kesho yake ofisini?
kamanda, pamoja na signature yako kusema nisikuchukulie serious, on this one you are dead right!!!kamanda angalia hapo nilipopaweka buluu kisha nisome hapo chini
1) Hii habari inasisitiza mara mbili kwamba "uamuzi" wa kwenda kwa mkufunzi usiku ni wa mwanafunzi na wala hakushurutishwa kwenda, ukisoma hapo buluu kwa umakini utagundua kwamba mkufunzi alimtaka mwanafunzi awasilishe maelezo ya maandishi ya kujitetea tu habari haikuonesha wakati wala mahala. Sasa mwanafunzi "anapoamua" kwenda kuwasilisha usiku tena nyumbani kwa mkufunzi inabidi tujiulize.
2) Habari inasema "mara alipoingia alianza kupiga kelele kwamba anabakwa", another weak point ,wataalam wanasema even crime need time and signs to happen.
3) Kama alivyoainisha mkuu MTM, hao waliovamia lazima walikuwa well organised kabla mavamizi, ni ngumu sana kuskia kelele tu tena nyumbani kwa mtu ukatoka straight na confidence ya kwenda kuuwa.
Lakini mengine yote ni mepesi , zito ni hapo habari inaposema kwamba ni uamuzi wa mwanafunzi kwenda kuwasilisha hayo maelezo usiku nyumbani kwa mkufunzi.
Dah! Hii kubwa.
Kwa maelezo ya mwanzo inaonesha huyu dada alisuka mpango na wenzake kama kumkomoa flani huyo ticha! ALIAMUA kupeleka barua ya maelezo NYUMBANI mida ya USIKU, alipoingia TU akaanza kupiga KELELE! Asingekufa huyo Dr wangeweza kuget away with it: kwa vile wamemuua, basi WATAJUTA MAISHA YAO YOTE kwa sababu wako likely zaidi kula nondo kwa kipindi kirefu tu, na hvyo future zao ZIMEVURUGIKA......!
Lakini hebu give me a break........., Kwani mwanafunzi wa chuo ni wa kuhangaikia kiasi cha kumzuia asilale nje?
kamanda angalia hapo nilipopaweka buluu kisha nisome hapo chini
1) Hii habari inasisitiza mara mbili kwamba "uamuzi" wa kwenda kwa mkufunzi usiku ni wa mwanafunzi na wala hakushurutishwa kwenda, ukisoma hapo buluu kwa umakini utagundua kwamba mkufunzi alimtaka mwanafunzi awasilishe maelezo ya maandishi ya kujitetea tu habari haikuonesha wakati wala mahala. Sasa mwanafunzi "anapoamua" kwenda kuwasilisha usiku tena nyumbani kwa mkufunzi inabidi tujiulize.
2) Habari inasema "mara alipoingia alianza kupiga kelele kwamba anabakwa", another weak point ,wataalam wanasema even crime need time and signs to happen.
3) Kama alivyoainisha mkuu MTM, hao waliovamia lazima walikuwa well organised kabla mavamizi, ni ngumu sana kuskia kelele tu tena nyumbani kwa mtu ukatoka straight na confidence ya kwenda kuuwa.
Lakini mengine yote ni mepesi , zito ni hapo habari inaposema kwamba ni uamuzi wa mwanafunzi kwenda kuwasilisha hayo maelezo usiku nyumbani kwa mkufunzi.
Amini tusiamini kwamba wote tulikuwa wanafunzi na ninakumbuka pia jinc walimu wa nidhamu wanavochukiwa, kutokana na adhabu aliyoitoa mkufunzi huyo, mwanafunzi yule alitakiwa kuyawasilisha maelezo yale muda wa kazi. Tujiulize
1. Kwa nini apelele maelezo usiku?
2. Kwa nini alipoingia tu apige kelele?
3. Kitu gn kilifanya urahisi wa wanafunzi hao kumpiga mkufunzi bila vithibitisho?
Tafakari! Chukua hatua, lazima kuna bifu la kibinafsi.
mimi naomba turudi kwenye ukweli pia,
je walimu wana tabia za kuomba ngono kwa kutumia cheo ?
jibu liko wazi ni ndio
hii habari kusema DENT aliamua kupeleka barua kwa ticha kweli inatia walakini kwa upande wa huyo mwanafunzi
lakini pia haya ni maneno ya nani? yawezekana ni muhandishi wa habari
jamii yetu ina CHALLENGE nyingi kufuata taratibu ni kama tunaogopa ukoma.
kwa mimi ninavyofikiria kama mwalimu angekuwa na mipaka katika ya kazi yake na masikini yake wanafunzi wasingepeka barua kwake.
SWALI GUMU, NI JE HIYO NI BARUA YA KWANZA KUPELEKWA HAPO NYUMBANI KWA MWALIMU USIKU?
mimi naomba turudi kwenye ukweli pia,
je walimu wana tabia za kuomba ngono kwa kutumia cheo ?
jibu liko wazi ni ndio
hii habari kusema DENT aliamua kupeleka barua kwa ticha kweli inatia walakini kwa upande wa huyo mwanafunzi
lakini pia haya ni maneno ya nani? yawezekana ni muhandishi wa habari
jamii yetu ina CHALLENGE nyingi kufuata taratibu ni kama tunaogopa ukoma.
kwa mimi ninavyofikiria kama mwalimu angekuwa na mipaka katika ya kazi yake na masikini yake wanafunzi wasingepeka barua kwake.
SWALI GUMU, NI JE HIYO NI BARUA YA KWANZA KUPELEKWA HAPO NYUMBANI KWA MWALIMU USIKU?
Mkuu! the only source of information ambayo tunayo basi ni hii thread yako na ndio maana tunaibua masuali kutokana na thread inavyojieleza. Na kuhusu hapo red, Hilo tatizo kweli lipo lakini kisheria kila tatizo linahukumiwa kipekee kulingana na ushahidi unaowasilishwa, (hakuna ushahidi wa kwamba wengi wanafanya..... katika mahakama). All in all kwa habari ilivyowasilishwa basi nakuhakikishia huyo mwanafunzi kibao kitamgeukia tu, labda waje na masimulizi mapya.
Suala langu muhimu ni: Kwanini aliamua (rejea thread yako) kuwasilisha maelezo usiku tena nyumbani kwa mkufunzi?
nimesikia kwamba huyo mwalimu alikua awe principal na wengi hawakupenda kwani alikua mnoko...
jiulizeni polisi walipata taarifa saa ngapi, mapanga wanafunzi waliyatoa wapi??
there were outside people as well
Huyo mwanafunzi kwa nini ameenda usiku kwa mwalimu? nahisi ni deal limepangwa tu
Hivi jiulize huyo msichana aliitwa kupeleka usiku huo hiyo barua au alitaka kumkomesha prof wa watu?katika hii post utata huko hapo kwenye hiyo, mimi najiuliza je ilikuwa mara ya kwanza barua kupelekwa usiku kwa mwalimu