Wanafunzi hawa waliopata zero wanaenda wap?

Wanafunzi hawa waliopata zero wanaenda wap?

Halafu utakuta walikuwa wanapigwa fimbo kila siku badala ya kujua changamoto zinazowakabili na kwanini hawaelewi

Ni mjinga tu atakaefurahia haya ila kuna tatizo kwenye mfumo wote wa Elimu
Yaani hawajui kufundisha na waliofaulu wamekariri tu kila kitu
Emmm; siafiki sana habari ya kupigwa fimbo kutokana na kutoelewa masomo ya darasani. Lakini mwanafunzi anayechapwa fimbo kwa makosa ya kijinga-jinga au uzembe ni halali.Kwa mfano mwanafunzi anaambiwa usiwe na wala usitumie simu hapa shuleni(Tunajua wanazo cm huko nje)au anaambiwa awe darasani wakati wa masomo-lakini yeye anazurura huko nje akichapwa nakubaliana kwani ni onyo na ni kwa manufaa yake.
 
Kwahiyo mwenye "D" zote na "C" mbili atleast akapata division 4 ya point 26 ambayo anaweza kwenda chuo au kusoma kidato cha tano (5) huku ana-reseat ni sawa na wenye "F" zote?! we vipi?!

Division 0 maana yake ni Failure!.. ni kama la saba tu wala haesabiki kwenye kundi la waliosoma sekondari. (Huyu kapoteza muda tu..., yaan alienda kukua,kujifunza uhuni wa kijinga, kupata mademu, mabwana na kupata washkaji na kuvuta bange basi!)

Division 4 hana ufaulu wa kwenda kidato cha tano ila anaweza kusoma mambo mengine au kurudia shule na akafanya vizuri.
Kuna mtu mmoja namjua alipata four zile za 26/27

Mzee wake akamfanyia mpango aende shule Fulani akaanza form 5 huku anarisiti form four Ili apate credit aruhusiwe kufanya Pepa la six

Akaja pata credit mwaka huu mwakani akapiga Pepa la six akakunja div 1.6

akaenda Chuo akapiga law akafumua sana. Yaani kama gari ilipigwa starter Sasa imepata Moto ngoma inayeeya!!

Akaenda Law school akamlamba uwakili

Saivi ni hakimu mkoa Fulani.

Inawezekana sana kuba watu sio kuwa hawana Akili Bali wanahitaji booster.

Mwengine

Alipata four ya 26 lakini alikuwa na credit zote akapiga five na six akatoka na div III enzi za mkwere akaenda Chuo kusoma bachelor ya uhasibu

Leo ana kazi na ana masters yake safi
 
Kuna diplomasia
Uhamiaji
Kurasini
ZIMEPAKANA HIZO
Watoto wanakula bangi kama chakula.
Mwalimu jichanganye wanakudunda... yaani hata class ukimshikia fimbo mwanafunzi wanakusaka nje ya shule wanakupiga hatari.

Ulizia walimu hapo
Kuna mmoja alimfata mwalimu akamwambia upo kwenye list kaa kwa kitulia usifatilie watu
.....nakaa maeneo ya karibu na hizo shule....

WATOTO NI WAHUNI KULIKO MAELEZO.
Tena nahisi hayo matokeo wamestandadaiz.halali halali hamna wa kupata 3 pale.na woote hao walimaliza la saba kwa ufaulu wa A$B
Watoto wa uswazi hao

Sent from my Infinix X657 using JamiiForums mobile app
 
Zingewekwa fani elekezi endapo mwanafunzi akipata O au 4 aende kusoma kwa malipo madogo kupunguza msongamano wa vibaka na vijidada vidangaji mtaani

Uchomeleaji
Gereji
Ufugaji
Ujenzi
Upishi
Sarakasi
Music
Footbal
Na fani zingine mbali mbali wangeweka malipo kidogo ya kujiunga kwa mfano 100,000 uniform na kuanza cozi na zingekuwa zinadumu kwa miaka miwili na zingefanywa za lazima utake usitake utaenda endapo umepata zero au dv 4

Watoto wadogo wamekuwa vibaka wanakufa ovyo
Visichana vidogo vinajiuza mpaka huruma vinazaa zaa tu
 
Kuna mtu mmoja namjua alipata four zile za 26/27

Mzee wake akamfanyia mpango aende shule Fulani akaanza form 5 huku anarisiti form four Ili apate credit aruhusiwe kufanya Pepa la six

Akaja pata credit mwaka huu mwakani akapiga Pepa la six akakunja div 1.6

akaenda Chuo akapiga law akafumua sana. Yaani kama gari ilipigwa starter Sasa imepata Moto ngoma inayeeya!!

Akaenda Law school akamlamba uwakili

Saivi ni hakimu mkoa Fulani.

Inawezekana sana kuba watu sio kuwa hawana Akili Bali wanahitaji booster.

Mwengine

Alipata four ya 26 lakini alikuwa na credit zote akapiga five na six akatoka na div III enzi za mkwere akaenda Chuo kusoma bachelor ya uhasibu

Leo ana kazi na ana masters yake safi
Mungu ana maguvu sana! Pia nafkiri hawa wanaopataga division four za 26-27 waangaliwe kwa jicho la tatu kabla hata hawajatoa hayo matokeo yao... wanaonesha wazi wana uwezo ila huenda sababu fulani fulani ziliwayumbisha. Hasa wale wenye points "26"
 
Usiingize Ujinga kwenye Discussion zenye mantiki. Huyo Diamond wako ana secret zake zilizomfanya afike pale... usipende kudanganyika na kuhadaika na mafanikio ya watu usiowajua kiundani. Fikiri kama mwanaume mwenye akili timamu. Shauri yako!
Kwani diamond sio mtu, we ndo umeleta ujinga wa ajabu wabongo sisi tunaakili fupi kinoma
 
Back
Top Bottom