Zanzibar-ASP
JF-Expert Member
- Nov 28, 2013
- 10,129
- 35,152
Hayawi hayawi sasa yamekuwa, Arusha kumekucha upya baada ya Godbless Lema kutua nchini na kulitikisa jiji lolote la Arusha kwa kishindo cha mapokezi, shamrashara mitaani na mkutano mkubwa wa hadhara.
Sasa makundi mbalimbali ya wanaCCM yameamua kupiga kelele kwa mbunge wa Jimbo la Arusha mjini, Mrisho Gambo ili atoke mafichoni na kuitisha mkutano wa hadhara ili kujibu kishindo na mapigo na hoja za Lema. Mpaka sasa CCM Arusha hawajatoa tamko lolote rasmi, huku wakingojea huenda labda Kinana atakuja kufanya ziara ili kufufua mwamko wa wanaCCM wa Arusha ambao wamepoa sana. Weekend hii (Jumamosi ya leo?) Mama Samia alitarajiwa kuwa jijini Arusha kiserikali na hatakuwa na ratiba yoyote ya kufanya vikao vya ndani vya CCM wala kuonana na wananchi moja kwa moja.
Kwa miaka kadhaa uhusiano wa uongozi wa CCM Arusha na Mrisho Gambo umekuwa mbaya kiasi cha kila upande kufanyiana fitina kila mara.
Sasa makundi mbalimbali ya wanaCCM yameamua kupiga kelele kwa mbunge wa Jimbo la Arusha mjini, Mrisho Gambo ili atoke mafichoni na kuitisha mkutano wa hadhara ili kujibu kishindo na mapigo na hoja za Lema. Mpaka sasa CCM Arusha hawajatoa tamko lolote rasmi, huku wakingojea huenda labda Kinana atakuja kufanya ziara ili kufufua mwamko wa wanaCCM wa Arusha ambao wamepoa sana. Weekend hii (Jumamosi ya leo?) Mama Samia alitarajiwa kuwa jijini Arusha kiserikali na hatakuwa na ratiba yoyote ya kufanya vikao vya ndani vya CCM wala kuonana na wananchi moja kwa moja.
Kwa miaka kadhaa uhusiano wa uongozi wa CCM Arusha na Mrisho Gambo umekuwa mbaya kiasi cha kila upande kufanyiana fitina kila mara.