Himidini... Hakuna mada negative. Haiwezekani kujifunza ikiwa mada zinaelemea upande mmoja... It would be absurd. Ila kuna kuleta mada kimzaha mzaha. Mada nyingi ambazo huletwa na kuonekana si za viwango si kwamba ni vitu ambavyo havipo katika jamii, ila mara nyingi hata msomaji unapo isoma unaona kabisa mrusha mada hakuwa serious, or as if tu alipost kufanya majaribio. Natamani zingekuwepo mada nitolee mfano; ila bahati mbaya or nzuri naona nyingi sana zimetolewa. Ila mfano; mtu anapoleta mada kama vile "Natamani kufanya ngono na kabinti ka miaka 14" si kwa kuomba ushauri - content unakuta inashabikia hilo tendo. Such a thread inakuwa si nzuri.
Michango ya member haipimwi kwa ukongwe bali kwa mada. Kuna members ambao ni wapwa na hoja zao ni msingi saa ingine kuliko hata member ambe ni wa zamani. Nadhani hapa Ukongwe unaongelewa in the sense wale ambao walikuwa hodari kushiriki na kuleta hoja za kujenga bila kujalisha misimamo katika hoja zao.
Option ya kufunga mada ni muhimu sana. Kuna mada ambazo hujadiliwa, ni applicable kabisa ila haiwezekani tena kujadiliwa na members wenyewe tokana na sababu mbali mbali tegemeana na content yenyewe. Hivyo mada inapokuwa ni applicable bado haifutwi, inabaki na kuwezekana kusoma but huwezi kuchangia. Kwa hapa MMU sikumbuki thread ipi ilifungwa, ila kuna threads Majukwaa kama ya Siasa na Intelligence hufungwa; na ukiweza kusoma toka post one hadi ya mwisho hata msomaji unaelewa kabisa ni kwa nini imefungwa.