Game Theory
Platinum Member
- Sep 5, 2006
- 8,545
- 835
Nikuunge mkono Mwl Moshi kwa yote matatu kimsingi, lakini natofautiana nawe kuwa hata "truth" sio "absolute" ndio maana mambo mengi bado yako debatable. Mambo mengi yanayochukuliwa kuwa "truth" ni makubaliano tu ya jumuiya fulani (wanataaluma, jamii, nk) kuwa yachukuliwe hivyo, na siku ushahidi tofauti ukipatikana kilichokuwa "truth" chaweza kubadilika kuwa sivyo tena (na hivyo wanakubaliana juu ya "ukweli mpya"). Mifano iko mingi. Kwa hili peke yake, si sawa hata kidogo kuzuia watu wasijadili jambo fulani, kwa sababu hata hiyo dhana tu ya kuwa mjadala huo uwepo au usiwepo ni debatable. Kwa mfano tunapozungumzia maisha binafsi ya kiongozi, tunamaanisha nini, na kwa mujibu wa nani? Kujadili afya ya kiongozi ni sawa au si sawa? Kimsingi hakuna mwenye jibu ambalo tunaweza kulichukulia kama "absolute truth" kuhusu swali hili, wengine watasema ni sawa na watatoa sababu, wengine watasema si sawa, na sababu watakuwa nazo, na zote zinajadilika. Kinachopaswa zijadiliwe zote, hoja "nyonge" itajifia yenyewe, na zile zenye nguvu zitabakia.
Labda kama Field Marshal ES anataka kubadilisha slogan ya JF iwe kuwa "We no longer dare to talk openly!" lakini tukumbuke members wengi wako hapa kwa kuwa wanapata nafasi ya ku-ventilate. Jibu la kuwapa hao serikali ni sisi kuendelea kujadili hoja yoyote inayofika ukumbini humu, zile zenye udhaifu zitajifia zenyewe na zile zenye nguvu kimantiki zitadumu na kuleta impact kama ambavyo tayari imeshatokea huko serikalini na kwingineko zitakakogusa.