Wana-JF: Ujumbe Mzito Toka Serikali!

Status
Not open for further replies.
Nikuunge mkono Mwl Moshi kwa yote matatu kimsingi, lakini natofautiana nawe kuwa hata "truth" sio "absolute" ndio maana mambo mengi bado yako debatable. Mambo mengi yanayochukuliwa kuwa "truth" ni makubaliano tu ya jumuiya fulani (wanataaluma, jamii, nk) kuwa yachukuliwe hivyo, na siku ushahidi tofauti ukipatikana kilichokuwa "truth" chaweza kubadilika kuwa sivyo tena (na hivyo wanakubaliana juu ya "ukweli mpya"). Mifano iko mingi. Kwa hili peke yake, si sawa hata kidogo kuzuia watu wasijadili jambo fulani, kwa sababu hata hiyo dhana tu ya kuwa mjadala huo uwepo au usiwepo ni debatable. Kwa mfano tunapozungumzia maisha binafsi ya kiongozi, tunamaanisha nini, na kwa mujibu wa nani? Kujadili afya ya kiongozi ni sawa au si sawa? Kimsingi hakuna mwenye jibu ambalo tunaweza kulichukulia kama "absolute truth" kuhusu swali hili, wengine watasema ni sawa na watatoa sababu, wengine watasema si sawa, na sababu watakuwa nazo, na zote zinajadilika. Kinachopaswa zijadiliwe zote, hoja "nyonge" itajifia yenyewe, na zile zenye nguvu zitabakia.

Labda kama Field Marshal ES anataka kubadilisha slogan ya JF iwe kuwa "We no longer dare to talk openly!" lakini tukumbuke members wengi wako hapa kwa kuwa wanapata nafasi ya ku-ventilate. Jibu la kuwapa hao serikali ni sisi kuendelea kujadili hoja yoyote inayofika ukumbini humu, zile zenye udhaifu zitajifia zenyewe na zile zenye nguvu kimantiki zitadumu na kuleta impact kama ambavyo tayari imeshatokea huko serikalini na kwingineko zitakakogusa.

AWARD1.jpg
 
..ujujmbe wa kamanda ungeweza kuwa na mantiki kama angeutoa kama maoni...yake,lakini umeonekana kama vile serikali inataka kutu dictate...nahisi watu watakuwa mbogo zaidi...i look this in pycho angle!!!

HATA HIVYO SERIKALI WAKITAKA KWENYE WEB YAO YA IKULU WAWEKE FORUM AU PALE TVT..NDIO WAWEKE MASHARTI...MIMI NADHANI WANA JF NI WATU HURU.....HAWASTAHILI KUSHURUTISHWA
 
..ujujmbe wa kamanda ungeweza kuwa na mantiki kama angeutoa kama maoni...yake,lakini umeonekana kama vile serikali inataka kutu dictate...nahisi watu watakuwa mbogo zaidi...i look this in pycho angle!!!

HATA HIVYO SERIKALI WAKITAKA KWENYE WEB YAO YA IKULU WAWEKE FORUM AU PALE TVT..NDIO WAWEKE MASHARTI...MIMI NADHANI WANA JF NI WATU HURU.....HAWASTAHILI KUSHURUTISHWA

cosign_3d_lg-1.gif
 
Kwangu naona hapa watu wa serikali wanahaha na kujaribu kutujengea inferiority complex. Kwanza mamods wamekuwa wakifanya kazi nzuri sana kuhakikisha zile rules za JF zinafuatwa, mara nyingi tumeshuhudia watu wakiwa banned kwa kutumia lugha chafu au za uchochezi. Naamini zile zile sheria za mwanzo zinafaa sasa kwa nini tuongeze sheria zingine? Sawa watu wasiwe emotional kuna mtu anajua 100% atareact vipi akiibiwa na akabahatika kumuona kibaka wake, atambusu?atacheka au atalia? sijui ila emotions zingine (ambazo si matusi) zinatokana na circumstances ambazo ndugu zetu viongozi wanatuxpose kwazo.
Long Live JF na hongera sana mods.
 
Naamini serikali wana lengo zuri la kuhakikisha kuwa maadili mazuri yanafuatwa na Watanzania mahali popote walipo. Kama ujumbe huo ni wa kweli (na assume hivyo) basi ninaomba serikali yetu katika kutusaidia kutekeleza ujumbe wao huo.

a. Watangaze kwenye magazeti ya serikali, redioni, TV n.k kuwa matusi yamepigwa marufuku na Mtanzania yeyote awe chumbani kwake, kijiweni, sokoni, n.k haruhusiwi kusema neno lolote la matusi na watutangazie adhabu itakayowapata watakaokiuka.

b. Pia itakuwa vizuri watuwekee maneno ya matusi ambayo yanapigwa marufuku kusikika au kutumika pamoja na vitendo. Uhuru wa maneno ni mkubwa zaidi kuliko uhuru wa vitendo. Hivyo wakituorodheshea matusi na madaraja ya matusi (kama first class, second class, nk) tutajua ni maneno gani tunaweza kuyatumia. Hivyo watatusaidia kujua kama fuska, mjinga, mzembe, fisadi n.k ni matusi ya daraja gani?

c. Wakishatoa hiyo definition tunaomba waongeze maafisa usalama wa maadili (Moral Police) ili washinde mitaani na kwenye mtandao kutafuta nani amesema nini na kuchukua hatua mara moja.

d. Wakimaliza kwenye maneno ninawashauri waanze kuangalia mavazi ya Watanzania ili tujue watanzania wanatakiwa kuvaa nguo za namna gani kama alivyojaribu Bi. Hawa Ghasia. Kwa sababu baadhi ya nguo zinachochea mawazo ya matusi, naamini itakuwa vizuri kama serikali itatangaza nguo za namna gani zivaliwe na Watanzania. Nashauri vazi la kanzu, gagulo na kaniki yawe ni mavazi ya lazima kwa Watanzania!

e. Wakimaliza hayo ninawashauri waje na utaratibu wa kuhakikisha kuwa watu hawachukuliani mademu au wanaume. Hii itapunguza maneno mengi ya mtaani ambayo huchochea maneno ya matusi. Utaratibu huo unaweza kuhusisha teknolojia ya kisasa ya mawasiliano ambapo kama Mbunge mmoja wa CCM alivyowahi kupendekeza wale wote wanaochukua wake/waume za watu wawekwe alama. Napendekeza wavae ribbon za aina fulani hivi. Za rangi ya zambarau ni nzuri zaidi.

f. Kwa vile maafisa wengi wa serikali na utumishi wa umma wanatumia muda mrefu kutumia email za matusi na picha za ngono (ushahidi upo) na vichekesho ambavyo wakati mwingine vinapakana na vya "kighaidi" napendekeza serikali iweke nembo kwenye compyuta zote za serikali ili wale wanaoependa kuangalia picha za ngono kompyuta zao zigome na waendelee na kazi.

g. Kwa vile ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka ni tatizo dogo nchini, napendekeza watawala wetu waendelee na kuhangaika na Jambo Forums na wapange vikao vya jinsi gani ya kuishughulikia huku wezi wa fedha za umma na wanaotumia mabaya madaraka yao wakiendelea kutanua. Kwa vile JF ndio tatizo kubwa kabisa linaloikabili nchi yetu sasa hivi, napendekeza "task force" mpya iundwe na Waziri Mkuu (wanaweza kumuomba Mhe. Lowassa kwa ushauri wa jinsi ya kufanya hivyo) ili iweze kushughulia dharura hii ya Jambo Forums.

Wakishafanya hivyo, mimi nawaunga mkono kwa ushauri wao huo wa bure!!
 
Ni vizuri umeleta ujumbe huo ili na sisi tukupe vipande vya kuwapelekea.

Lakini kwa nini wasije wenyewe wanakutuma wewe?

Nauliza hivi kwa sababu hapa JF mtu yeyote anaweza jiunga akasema kile anachodhani ni sahihi.

Nadhani bado unamkumbuka Kaka Mcha, alikuja hapa akamtetea Lowassa kwa uhodari,nguvu na uaminifu wake wote, mwisho kama vile kutabiri anguko kuu la Lowassa aliachia ngazi ili kijiwe kipate kuendelea kwa desturi yake.

Kaka mcha alikuwa na mchango fulani hapa JF,lakini 75% ya hoja zake zilikuwa pumba ambazo zilimlemea akalazimika kuwajibika hapa JF.

Umesema tusijadiri maisha yao binafsi kwa sababu tunawagombanisha na wake zao?

Sidhani kama sababu ya kuongelea maisha yao binafsi ni kuwagombanisha wao na wake au waume zao.

Wao ni Public Figure kwa hiyo Twenty four seven wako Under Scrutiny wanataka au hawataki.

Sababu kuu ya msingi ya kusema maisha binafsi ya Viongozi wa seruikali ya SISIEMU na nyingine yeyote itakayo kuja ni kuhakikisha , maisha ya kiongozi haya create matatizo na tamaa kiasi cha kumfanya aanze kuuza vyandarua vya msaada, au kutumia fedha ya maendeleo vijijini kufanya makongamano ya kukata kwa mundu huko Bagamoyo.

Umalaya ni mzigo mkubwa sana ndani ya nchi.
Umalaya wa viongozi wetu ni chanzo cha tufani nyingi za kujitakia.
Umalaya wa viongozi ni chanzo kikubwa cha kuyumba na kurudi nyuma kiuchumi kwa Familia za viongozi , jamiii na Taifa kwa ujumla.
Umalaya wa viongozi wetu ni gharama ya nyongeza juu ya mzigo mkubwa wa umasikini ambao nao asili yake vile vile ni uongozi wao usio na vision.

Kama kiongozi anataka kuwa na wake 7 basi awe mkweli aoe hao wake 7 tujue moja. Lakini mchezo wa kutembea wanavua kaptula kila mtaa wanakaribisha Riwaya za kashfa za kujitakia hapa JF

Wewe rais mzima kwa nini ukatembee na mke wa mtu??

Kwa nini usijichagulie kidosho katika vidosho waliojaa tele katika kila kona ya Tanzania uka specialize kama yule mnyama Fungo anaye kunya sehemu moja tu maisha yake yote???!!

Haya tunajua uloda wa mkeo unausikia tu kwa vile ni miaka kibao tangu mpeane visogo. Kwa nini msipeane taraka kama rais wa Ufaransa na kuanza life na kimwana mpya ukatunyima sababu za kusema?

Mchezo wa kutembea na wake za watu, watoto wa shule na wafanyakazi wa chini yakoambao si wake zako kisheria na kiimani na mara nyingi kwa kutumia rungu tulilo kupa UFE.
Nasema UFE.

Sisi hapa JF hatujadiri maisha ya viongozi wenye wake wengi, tunajadiri maisha ya viongozi wanao tumia vibaya Vitumbua na kuni zao, kibay zaidi kwa gharama zetu walipa kodi.

Kiongozi akiwa na nyumba ndogo 3 akipeleka nyumba moja London kwenye shopping na nyingine zilizo baki zitadai kwenda, ili kujitoa kimaso maso Kiongozi huyo inabidi abebe gharama na kufadhiri shopping za vimada wake wote. Kwa vile mshahara wake na maluplupu hayana uwezo wa kukidhi gharama hiyo,ni wazi kwamba ataihamishia gharama hiyo kwetu wananchi matokeo yake ni haya ya kusaini mikataba ya ovyo na kupokea Rushwa kwenye kila jambo na kujenga tamaa nyingi za ajabu.

Hivi unajua kila tunapolipa ziada ya Bill za umeme Lowassa Rostamu na Timu yao nzima wanapata fedha za kunulia wake zao na vimada wao Poda za bei mbaya na hata Kukodi ndege kwenye ziara za kuendeleza ufisadi.

Sisi tukikung'aza kwenye Rada zetu tutauweka wazi udhaifu wako. Lengo la kuweka wazi aibu yako ni kuuonyesha umma asili ya tamaa yako na jinsi ambavyo kiongozi wewe ni bomu la machozi na mzigo kwa kila mwananchi. Mkeo au mumeo akijua udhaifu wako hiyo inakuwa ni by the way na si lengo la shughuli nzima ya kuanika maovu yako ya nguoni.

Uhuru ni Uhuru, Uhuru wa kuweka mipaka na mtu yeyote yule si uhuru ni utumwa.

Serikali ina sehemu nyingi sana za kutoa maagizo yake RTD na TvT magazeti na Mikutano ya hadhara. Binafsi sioni sababu wao kutumia member wa JF kutoa maoni yao yasiyokubalika na yenye kutaka sisi wana JF tuone simanzi.

Mke wa Malecela mama ANNA KILANGO kwa maneno yake mwenyewe alisema yuko tayari kwenda kinyume na mzee Malecela kama mzee huyo ataleta hoja utumbo ili kulinda maslahi ya walio mchagua na wananchi wote wa Tanzania.
Maneno ya ANNA ni dalili moja kwamba hata huko serikali tuna watu ambao wako tayari kurisk kila kitu ili kuweka mambo ya kitaifa sawa. Kinyume cha maneno ya ANNA, tuna watu ndani ya serikali wanao taka tufunike vinywa vyetu kwa gharama zetu eti sababu viongozi wahanga hao wanakosa raha na heshima yao inapindishwa kwa kelel zetu.

Kifupi ni kwamba tutatoa siri ya kiongozi yeyote asiye muadilifu kwa staili yeyote tuitakayo bila kujali wadhifa na heshma yake.

Heshma ipi wakati kesha ipindisha?????!!!
 
Ni vizuri umeleta ujumbe huo ili na sisi tukupe vipande vya kuwapelekea.

Lakini kwa nini wasije wenyewe wanakutuma wewe?

Nauliza hivi kwa sababu hapa JF mtu yeyote anaweza jiunga akasema kile anachodhani ni sahihi.

Nadhani bado unamkumbuka Kaka Mcha, alikuja hapa akamtetea Lowassa kwa uhodari,nguvu na uaminifu wake wote, mwisho kama vile kutabiri anguko kuu la Lowassa aliachia ngazi ili kijiwe kipate kuendelea kwa desturi yake.

Kaka mcha alikuwa na mchango fulani hapa JF,lakini 75% ya hoja zake zilikuwa pumba ambazo zilimlemea akalazimika kuwajibika hapa JF.

Umesema tusijadiri maisha yao binafsi kwa sababu tunawagombanisha na wake zao?

Sidhani kama sababu ya kuongelea maisha yao binafsi ni kuwagombanisha wao na wake au waume zao.

Wao ni Public Figure kwa hiyo Twenty four seven wako Under Scrutiny wanataka au hawataki.

Sababu kuu ya msingi ya kusema maisha binafsi ya Viongozi wa seruikali ya SISIEMU na nyingine yeyote itakayo kuja ni kuhakikisha , maisha ya kiongozi haya create matatizo na tamaa kiasi cha kumfanya aanze kuuza vyandarua vya msaada, au kutumia fedha ya maendeleo vijijini kufanya makongamano ya kukata kwa mundu huko Bagamoyo.

Umalaya ni mzigo mkubwa sana ndani ya nchi.
Umalaya wa viongozi wetu ni chanzo cha tufani nyingi za kujitakia.
Umalaya wa viongozi ni chanzo kikubwa cha kuyumba na kurudi nyuma kiuchumi kwa Familia za viongozi , jamiii na Taifa kwa ujumla.
Umalaya wa viongozi wetu ni gharama ya nyongeza juu ya mzigo mkubwa wa umasikini ambao nao asili yake vile vile ni uongozi wao usio na vision.

Kama kiongozi anataka kuwa na wake 7 basi awe mkweli aoe hao wake 7 tujue moja. Lakini mchezo wa kutembea wanavua kaptula kila mtaa wanakaribisha Riwaya za kashfa za kujitakia hapa JF

Wewe rais mzima kwa nini ukatembee na mke wa mtu??

Kwa nini usijichagulie kidosho katika vidosho waliojaa tele katika kila kona ya Tanzania uka specialize kama yule mnyama Fungo anaye kunya sehemu moja tu maisha yake yote???!!

Haya tunajua uloda wa mkeo unausikia tu kwa vile ni miaka kibao tangu mpeane visogo. Kwa nini msipeane taraka kama rais wa Ufaransa na kuanza life na kimwana mpya ukatunyima sababu za kusema?

Mchezo wa kutembea na wake za watu, watoto wa shule na wafanyakazi wa chini yakoambao si wake zako kisheria na kiimani na mara nyingi kwa kutumia rungu tulilo kupa UFE.
Nasema UFE.

Sisi hapa JF hatujadiri maisha ya viongozi wenye wake wengi, tunajadiri maisha ya viongozi wanao tumia vibaya Vitumbua na kuni zao, kibay zaidi kwa gharama zetu walipa kodi.

Kiongozi akiwa na nyumba ndogo 3 akipeleka nyumba moja London kwenye shopping na nyingine zilizo baki zitadai kwenda, ili kujitoa kimaso maso Kiongozi huyo inabidi abebe gharama na kufadhiri shopping za vimada wake wote. Kwa vile mshahara wake na maluplupu hayana uwezo wa kukidhi gharama hiyo,ni wazi kwamba ataihamishia gharama hiyo kwetu wananchi matokeo yake ni haya ya kusaini mikataba ya ovyo na kupokea Rushwa kwenye kila jambo na kujenga tamaa nyingi za ajabu.

Hivi unajua kila tunapolipa ziada ya Bill za umeme Lowassa Rostamu na Timu yao nzima wanapata fedha za kunulia wake zao na vimada wao Poda za bei mbaya na hata Kukodi ndege kwenye ziara za kuendeleza ufisadi.

Sisi tukikung'aza kwenye Rada zetu tutauweka wazi udhaifu wako. Lengo la kuweka wazi aibu yako ni kuuonyesha umma asili ya tamaa yako na jinsi ambavyo kiongozi wewe ni bomu la machozi na mzigo kwa kila mwananchi. Mkeo au mumeo akijua udhaifu wako hiyo inakuwa ni by the way na si lengo la shughuli nzima ya kuanika maovu yako ya nguoni.

Uhuru ni Uhuru, Uhuru wa kuweka mipaka na mtu yeyote yule si uhuru ni utumwa.

Serikali ina sehemu nyingi sana za kutoa maagizo yake RTD na TvT magazeti na Mikutano ya hadhara. Binafsi sioni sababu wao kutumia member wa JF kutoa maoni yao yasiyokubalika na yenye kutaka sisi wana JF tuone simanzi.

Mke wa Malecela mama ANNA KILANGO kwa maneno yake mwenyewe alisema yuko tayari kwenda kinyume na mzee Malecela kama mzee huyo ataleta hoja utumbo ili kulinda maslahi ya walio mchagua na wananchi wote wa Tanzania.

Kifupi ni kwamba tutatoa siri ya kiongozi yeyote asiye muadilifu kwa staili yeyote tuitakayo bila kujali wadhifa na heshma yake.

Heshma ipi wakati kesha ipindisha?????!!!

untitled0.jpg
 
Naamini serikali wana lengo zuri la kuhakikisha kuwa maadili mazuri yanafuatwa na Watanzania mahali popote walipo. Kama ujumbe huo ni wa kweli (na assume hivyo) basi ninaomba serikali yetu katika kutusaidia kutekeleza ujumbe wao huo.

a. Watangaze kwenye magazeti ya serikali, redioni, TV n.k kuwa matusi yamepigwa marufuku na Mtanzania yeyote awe chumbani kwake, kijiweni, sokoni, n.k haruhusiwi kusema neno lolote la matusi na watutangazie adhabu itakayowapata watakaokiuka.

b. Pia itakuwa vizuri watuwekee maneno ya matusi ambayo yanapigwa marufuku kusikika au kutumika pamoja na vitendo. Uhuru wa maneno ni mkubwa zaidi kuliko uhuru wa vitendo. Hivyo wakituorodheshea matusi na madaraja ya matusi (kama first class, second class, nk) tutajua ni maneno gani tunaweza kuyatumia. Hivyo watatusaidia kujua kama fuska, mjinga, mzembe, fisadi n.k ni matusi ya daraja gani?

c. Wakishatoa hiyo definition tunaomba waongeze maafisa usalama wa maadili (Moral Police) ili washinde mitaani na kwenye mtandao kutafuta nani amesema nini na kuchukua hatua mara moja.

d. Wakimaliza kwenye maneno ninawashauri waanze kuangalia mavazi ya Watanzania ili tujue watanzania wanatakiwa kuvaa nguo za namna gani kama alivyojaribu Bi. Hawa Ghasia. Kwa sababu baadhi ya nguo zinachochea mawazo ya matusi, naamini itakuwa vizuri kama serikali itatangaza nguo za namna gani zivaliwe na Watanzania. Nashauri vazi la kanzu, gagulo na kaniki yawe ni mavazi ya lazima kwa Watanzania!

e. Wakimaliza hayo ninawashauri waje na utaratibu wa kuhakikisha kuwa watu hawachukuliani mademu au wanaume. Hii itapunguza maneno mengi ya mtaani ambayo huchochea maneno ya matusi. Utaratibu huo unaweza kuhusisha teknolojia ya kisasa ya mawasiliano ambapo kama Mbunge mmoja wa CCM alivyowahi kupendekeza wale wote wanaochukua wake/waume za watu wawekwe alama. Napendekeza wavae ribbon za aina fulani hivi. Za rangi ya zambarau ni nzuri zaidi.

f. Kwa vile maafisa wengi wa serikali na utumishi wa umma wanatumia muda mrefu kutumia email za matusi na picha za ngono (ushahidi upo) na vichekesho ambavyo wakati mwingine vinapakana na vya "kighaidi" napendekeza serikali iweke nembo kwenye compyuta zote za serikali ili wale wanaoependa kuangalia picha za ngono kompyuta zao zigome na waendelee na kazi.

g. Kwa vile ufisadi na matumizi mabaya ya madaraka ni tatizo dogo nchini, napendekeza watawala wetu waendelee na kuhangaika na Jambo Forums na wapange vikao vya jinsi gani ya kuishughulikia huku wezi wa fedha za umma na wanaotumia mabaya madaraka yao wakiendelea kutanua. Kwa vile JF ndio tatizo kubwa kabisa linaloikabili nchi yetu sasa hivi, napendekeza "task force" mpya iundwe na Waziri Mkuu (wanaweza kumuomba Mhe. Lowassa kwa ushauri wa jinsi ya kufanya hivyo) ili iweze kushughulia dharura hii ya Jambo Forums.

Wakishafanya hivyo, mimi nawaunga mkono kwa ushauri wao huo wa bure!!

salute-1.jpg
 
Hatuwezi kupangiwa na serikali ni kitu gani cha kujadili na ni kipi si cha kujadili.Huu ni upumbavu na ukosefu wa akili timamu,ukishakubali kuwa kiongozi kubali na kubeba msalaba wake,sisi ndiyo waajiri wenu,mnaboronga halafu mtupangie cha kuongea,Yaani Tanzania imekua ni nchi inayokumbatia mafisadi,umaskini wa kujitakia huu.Kama hawataki kusemwa waache kazi,ndoa zao zikivunjika who cares,ni kweli wengi wao ni wahuni.
 
Hili li-serikali letu ni la ajabu sana na linaendeshwa na mijitu mimbumbumbu kweli..(nawathubutisha mje mnikamate na mimi kwa kuwatukana). Hawawezi kuwaambia watu nini cha kusema. Badala ya kushughulikia mambo ya maendeleo yenyewe inabaki kushughulikia mijitu ya kwenye mitandao ambayo mingi iko ughaibuni. Hii mijamaa ya serikali yote mifala tu and I double dare them to come and get me. God damn it!!!
 
Mkuu Sana Mzee ES

Naomba kabla ya kujibu, print haya majibu uwapelekee wakupe majibu ya hoja hizi. Mwanzo niliposoma nilielekea kukubaliana na wewe hila
naona hoja zimekuwa kali sana kinachotakiwa wapelekee print out ya majibu, uone kama kweli wameridhika.

Mimi kwa mtazamo wangu naona wataridhika na watafarijika na majibu yaliyotolewa, kwa kifupi JF hakuna matusi, na nifedhea kwa watu wazima kama Sisi kutwambia tunatoa matusi kinachoongelewa hapa ni kwa Uwazi na UKweli(hatufanyi UFISADI)
 
FMES,
Ahsante sana kwa hoja zako, moja kati ya utajiri wa lugha yetu ya kiswahili ni misemo mingi iliyosheni busara kama huu
'MTU ANAWEZA AKAKUNYIMA MAJI LAKINI SIYO NENO' Sina haja ya kufafanua zaidi yahapo.

Kimsingi ninataka kusema kwamba FMES ana hoja ambayo ni valid kabisa, kutaka ku-ignore hoja yake kwa vigezo vya emations nadhani si sahihi kabisa. JF haiko hapa kwa ajili ya kupambana na serikali, ni vema JF iwepo na kuijenga ifikie kiwango cha kuwa ni sauti mbadala ya wananchi isiyopitia kwa wawakilishi wao yaani wabunge, madiwani nk. Ni vema tukawa na vision ambayo ni dynamic rather than vision mgando.

Let us come to a point whereby hata majibu ya serikali yapatikane moja kwa moja bila ya kusubiria vikao vya bunge. Katika kufanikisha yote haya we need partners to work with, ikiwa ni pamoja na serikali na taasisi zingine. tusiingiwe na hofu ikiwa kuna dalili za kuonyesha kwamba serikali inaweza kuwa mshirika katika kufanya kazi na JF. ikibidi JF ijibadilishe ili iwe na nguvu na maana zaidi ya kuwatumikia wananchi, hakuna haja ya kuogopa zaidi ya kujadili hoja na kufikia mwafaka.

Ningependa kuona kuwa inawafikia watanzania wengi hasa wale walioko vijijini hata kama ni kuwa na kompyuta za community. Katika kufanikisha yote haya kuaminiana ni muhimu na kutaleta mawasiliano mazuri katika watawaliwa na watawala. Mimi ninaona tufikirie kufika mahali ambapo kila mwananchi aweze kuinua sauti yake na ikasika.

TUNAHITAJI WASHIRIKA UNLESS KAMA TUNATAKA KUWA WABINAFSI.
 
Mkuu Sana Mzee ES

Naomba kabla ya kujibu, print haya majibu uwapelekee wakupe majibu ya hoja hizi. Mwanzo niliposoma nilielekea kukubaliana na wewe hila
naona hoja zimekuwa kali sana kinachotakiwa wapelekee print out ya majibu, uone kama kweli wameridhika.

Kama ndoa zao zinavunjika jamani si ni kutokana na matendo yao? kwani JF ndio wanavunja ndoa au wanawatuma mkafanye ufuska? Kama mtu ni mzizi tumuite nanai? kama mtu ni fisadi tumuite nani? na kama mtu ni muongo tumuite nani? Mwizi aitwe mwizi hakuna tofauti wa mwizi wa silaha na wa kalamu wote ni wezi tuu. Kijiko kiitwe kijiko na sepeto liitwe sepeto hicho ndicho kinachofanyika hapa JF.

Mimi kwa mtazamo wangu naona wataridhika na watafarijika na majibu yaliyotolewa, kwa kifupi JF hakuna matusi, na nifedhea kwa watu wazima kama Sisi kutwambia tunatoa matusi kinachoongelewa hapa ni kwa Uwazi na UKweli(hatufanyi UFISADI)


Nadhani serikali ndio wanatutukana. Kitendo cha kutuambia tufunge midomo yetu na kutuchagulia nini cha kusema na nini cha kuacha ni tusi kubwa tena la nguoni. Mkuu ES naona jamaa wakisoma majibu ya wakuu wa hapa JF watakuwa wamepata majibu sahihi kuwa JF sio kijiwe cha wahuni, JF sio kijiwe cha kutukana, JF hawataki kuburuzwa.

Sisemi mengi maana naona washikaji wamesema ya kutosha. Hao viongozi waambie wawe na maadili mazuri kama kuna siku watasikia jina lao limetajwa kwa ubaya hapa JF au popote pale zaidi litakuwa linatajwa kwa sifa nzuri.

Nadhani kitendo cha wao kutumia muda wao kushinda huku JF na kutafuta namna ya kutuzima badala ya kufanya kazi ambayo tumewaajiri na wanalipwa kwa kodi zetu ni Matusi makubwa sana kwa wananchi na kwa taifa kwa ujumla.

Wafanye kazi waone kama hawatasifiwa hapa JF. Mkuu ES najua umeleta huu ujumbe hapa kwa nia nzuri sana ila agalia sana mkuu jamaa wanaweza kukutumia na kukufanya kibaraka bila kujua. Najua mjumbe hauwawi lakini pia wapelekee ujumbe wa wana JF kama walivyojibu hii hoja.
 
Good to be back JamboForums. Mkuu ES naona wazee walikuweka pannel. I have few things i want to comments on,
  • When you decide that you want to run for plublic office, ni wazi yakwamba unafahamu kwamba there is no more private life. Hii ipo kila kona ya dunia, hivyo basi it is almost imposible kwa kiongozi au superstar kuwa na maisha kama normal citizen. Hata hivyo it is not right kumtukuna mtu yoyote for any reason, this is not only viongozi, but even normal citizen.
  • We as citizen, we have rights to know if your dating outside your marriage, we have rights to know if you gave your son or spause a contract deal illegal. Hivyo basi, there is no protection act inayomlinda kiongozi yoyote wa kiserikali mwenye kutenda maovu, iwe ya kifamilia, kijamii au kiuchumu. If we believe that any kiongozi ana mwanamke wa nje, we will come here and provides facts. We will do that because we believes it is moral wrong to practice that kind of staff, also kiongozi ni mfano kwa jamii and we will not torolate mifano mibovu.

Hivyo basi, ni juu yao vingozi kulinda hadhi zao. Tutazungumza pasipo kugopa wala kutetereka pindi tutakapo gundua ta kwamba kiongozi yoyote anajitumbukiza kwenye maadili mabovu. Na hili halitakuwa na mipaka, yaani ni kuanzia CUF mpaka CCM.
 
Hizi ni dalili za kuogopa vivuli vyao wenyewe. Kama kiongozi anafanya yale ambayo yanatakiwa na sheria za nchi afanye na akayafanya na tukaona matunda yake,hakuna atakayehangaika naye hapa JF. Kuna viongozi wengi tu waadilifu ambao hata majina yao yanatajwa vizuri tu hapa JF. Umeshasikia Pinda kaongelewa vibaya hapa? hakuna,kwanini awe lowassa,karamagi na Mgonja? Kuna tatizo hapa,ndiyo maana sisi wenye nchi lazima tupige kelele. Unapokuwa kiongozi lazima maisha yako yawe wazi,kama maadili yako ni machafu hatutasita kukuandika hapa. Kwahiyo,tunachotaka sisi ni wafanye kazi.
 
Nina point tatu.
  1. Si sawa kupangiwa na serikali cha kujadili.
  2. Si sawa hata hivyo kutumia matusi hapa. Si sawa vile vile kusema vitu kama ugonjwa wa mtu. Hata daktari haruhusiwi kusema ugonjwa wa mtu, sembuse wana JF?
  3. Si kweli kwamba freedom ni absolute. We are free to do good; but no one is free to do evil. It is an axiom in Philosophy that freedom is not absolute. Truth is absolute but freedom is not.
Kwa hivyo basi, nakubali kwamba tuwe na standards hapa, lakini ziwe za kujipangia sisi wenyewe na sio kupangiwa na serikali.

Mkuu Moshi,

Umemaliza kila kitu hapo. Lazima tuwe fair hata kwa sisi wenyewe ju ya hili.
 
I do smell something hapa lakini kila mtu ana uhuru wa kusema lake .Mimi nakuomba sana FMES tupe mfano wa maisha ya mtu binafsi ambayo ilikuwa ni mada hapa .Watu wanaweza kutolea mifano kwa mambo yao ya vimada nk .Lakini JF haijawahi kuwa na mada kuhusu maisha ya mtu .Kumbuka ukisha kuwa kiongozi pia maisha yako ni yetu sisi Watanzania .Ndiyo maana ya kuwa kiongozi na hapa huwa hakuna matusi huwa ni ukweli kwamba Fulani anafanya kitu fulani na mtu fulani na ndiyo maana mambo yanaenda hivi lakini sijawahi kuona Mada hapa inamsema Lunyungu na maisha yake hapana .Kidogo nina maswali mengi kwenye siri uliyo tupa lakini mimi ni Mzee hapa I read between the lines.
 
ilipoongea na mbunge mmoja hivi karibuni na nikamuuliza swali kwa nini bunge lilizorota miaka yote? Akanipa majibu mawili

(i) Kila mbunge anawaza kuwa waziri siku moja ni wabunge wachache sana wanaotaka historia ije watambue kama walikuwa ni wabunge wazuri
(ii) Fall back position. wengi wa wabunge wetu kama wakiachishwa ubunge wamekisha

Haya majibu yananifanya nimsamehe mtoa hoja
 
"Kama tukianza kuchafuana hapa,sidhani kama kuna Mwanasiasa yoyote atabaki" Edward Lowassa!


Mkuu FMES

hii ina maanisha viongozi wote ni wachafu,hivyo bila kuwasema kwamba ni wachafu hawatabadilika,tabia ya maisha yao binafisi na yenyewe ni ufisadi,rejea maana halisi ya neno Ufisadi.tupo hapa kupinga Ufisadi na mambo mengine machafu.

wewe kiongozi atembee na mke wa mtu ndio tusiseme,uantaka aendelee??naamini umetumwa na karamagi.
 
Ukikubali kuwa kiongozi ni kwamba wewe unakuwa ni kioo cha jamii...kama wewe unaendekeza ngono ukiripotiwa usilalamike. Tumeambiwa ufisadi na rushwa si kuiba pesa tu..hata kudai na kufanya ngono na mtu kwa kutumia wadhifa ulionao ni ufisadi na ni rushwa hiyo.

Kama wanagombana na familia ni juu yao inaonekana hawana maadili kabisa. Wachague moja waachie ngazi ili waweze kufanya ngono zao au wawe makini na kazi zao wasiendekeze ngono.

Kama kiongozi akiendekeza umalaya na akafahamika ni lazima ajadiliwe hapa. Pia ni katika kupambana na UKIMWI. Kama wana ndoa zao kwanini watoke nje...wakitoka nje tutawamulika na tutawaanika hapa bwana.
...
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom