Mohamed Said
JF-Expert Member
- Nov 2, 2008
- 20,921
- 30,265
AGA KHAN PATRON WA EAMWS ALIPOKUTANA NA VIONGOZI WA BAKWATA MIAKA YA 1980
Nakusudia In Shaa Allah kuweka hapa makala mbili au tatu hivi kueleza yaliyotokea baada ya miaka mingi na Aga Khan aliyekuwa Patron wa EAMWS kujaribu upya kusaidia Waislam wa Tanzania lakini safari hii kupitia BAKWATA.
Naamini yapo mafunzo makubwa kwetu na Waislam na wananchi kwa ujumla wataielewa historia ya BAKWATA na viongozi wake.
Aga Khan si mgeni Tanzania na waliomuingiza nchini ni Waislam katika miaka ya 1930 kwa ajili ya kutoa misaada kwa Waislam.
Katika miaka ya 1930 baba yake huyu Aga Khan wa sasa Shah Karim Al Hussein, Sir Sultan Mohamed Shah alitembelea Tanganyika na katika mradi mmoja wapo aliofika kuuangalia ulikuwa ujenzi wa shule ya Al Jamiatul Islamiyya School, Mtaa wa Agrrey na New Street uliokuwa ukijengwa na Waislam chini ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Katika hafla ile mwanafunzi aliyesoma risala mbele ya Aga Khan alikuwa Abdul Sykes.
Miaka mingi baadae Abdulwahid Sykes sasa kijana na mwanasiasa akajachaguliwa kuwa mjumbe katika Bodi ya Elimu ya Aga Khan).
Aga Khan alivutiwa sana na juhudi zile walizoonyesha Waislam wa Tanganyika za kutaka kujiendeleza katika elimu na akatoa fedha zilizowezesha kumaliza ujenzi wa shule yote kwa ukamilifu wake.
Aga Khan akatoa changamoto kwa Waislam wa Afrika Mashariki kuwa Muislam akichanga shilingi moja kwa ajili ya maendeleo ya umma yeye ataoa shilingi moja vilevile juu yake.
Huu ulikuwa sasa wakati wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS).
Kitendo hiki cha Aga Khan kilikuwa msaada mkubwa kwa Waislam kwani wakati wa ukoloni ni Ukristo pake yake ndiyo ulikuwa na fursa ya kupata misaada kutoka nje.
Ushirikiano huu wa Aga Khan na Waislam wa Tanganyika uliendelea vizuri sana.
Aga Khan kupitia EAMWS alijenga shule nyingi hadi kufikia sasa kutaka kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam chini ya usimamizi wa Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Tewa Said Tewa na Aziz Khaki aliyekuwa mwakilishi wa Aga Khan Tanzania.
Hii ilikuwa mwaka 1968 baada ya Tanganyika kuwa huru.
Aga Khan na EAMWS kutaka kujenga chuo kikuu hapo ndiyo matatizo yakaanza baina ya Nyerere na uongozi wa EAMWS.
Kisa hiki ni maarufu hapana haja ya kukirejea.
Sasa tuingie kwenye kisa chenyewe.
Miaka mingi ikapita na mwishowe Nyerere akatoka madarakani na serikali ikashikwa na Ali Hassan Mwinyi.
Kwa takriban miaka 20 Aga Khan hakupata kutia mguu Tanzania.
Katika utawala wa Mwinyi Aga Khan akaja Tanzania.
Katika mazungumzo na Rais Mwinyi, Rais Mwinyi akaomba msaada wa Aga Khan katika nyanja tatu - Elimu, Kilimo na Afya.
Aga Khan akamueleza Rais Mwinyi kuwa Aga Khan walikuwapo Tanzania miaka ya nyuma wakisaidia katika elimu kupitia EAMWS.
Hili suala la elimu likamgusa sana Aga Khan kiasi cha yeye alipomaliza mazungumzo na Mwinyi akamwamrisha Katibu wa Elimu wa Aga Khan Tanzania, Riyaz Gulamani awakaribishe viongozi wa Waislam wa iliyokuwa EAMWS pamoja na viongozi wa BAKWATA katika chakula cha jioni ili wajadili maendeleo ya Waislam.
Katika viongozi wa EAMWS walioalikwa katika hafla ile alikuwa Tewa Said Tewa.
Kutoka BAKWATA walioalikwa walikuwa Sheikh Mkuu wa BAKWATA Hemed bin Jumaa, Adam Nasibu aliyekuwa katibu wa BAKWATA, Mustafa Songambele mzee wa CCM na mwanakamati katika BAKWATA na Waislam wengineo.
Kutoka EAMWS aliyealikwa alikuwa Tewa Said Tewa.
Baada ya chakula Aga Khan akawaeleza nia yake ya kuwaita na akawataka watoe wanachotaka wafanyiwe na Aga Khan katika elimu.
Hapa ndipo ''drama,' ilipoanza.
Akasimama kiongozi mmoja wa BAKWATA na mzee wa CCM, Mustafa Songambele, akamwambia Aga Khan, ''Serikali ya Tanzania inawatosheleza Waislam katika elimu na hawahitaji msaada kutoka kokote.''
Mustafa Songambele
Naomba nisimame hapa.
Mkasa huu kwa mara ya kwanza alinihadithia Riyaz Gulamani.
Sikuamini kama inaweza kuwa kweli.
Kisa hiki nikaja kuhadithiwa tena na Tewa Said Tewa kama vile alivyonihadithia Riyaz Gulamani.
Hapo ndipo nikaamini kuwa kisa kile hakika kilitokea na Mzee Tewa akanipa na jina la huyo aliyesema maneno yale.
Tuendelee.
Aga Khan kwa upole kabisa akajibu kuwa jana yake alikuwa na Rais na yeye kaomba msaada wa elimu.
Hapo sasa ndipo likazuka zogo baina ya viongozi wa BAKWATA na Waislam wengine mbele ya mgeni Aga Khan.
Kufupisha mkasa.
Kabla hajaondoka kufuatia yale aliyosikia na aliyoshuhudia, Aga Khan akamwambia Riyaz, ''Inaelekea hawa ndugu zetu bado hawajawa tayari lakini ushauri wangu ni kuwa uache mlango wetu wazi.
Siku yoyote watakapokuwa tayari basi tutatoa msaada.''Picha: Aga Khan na Songambele.
Nakusudia In Shaa Allah kuweka hapa makala mbili au tatu hivi kueleza yaliyotokea baada ya miaka mingi na Aga Khan aliyekuwa Patron wa EAMWS kujaribu upya kusaidia Waislam wa Tanzania lakini safari hii kupitia BAKWATA.
Naamini yapo mafunzo makubwa kwetu na Waislam na wananchi kwa ujumla wataielewa historia ya BAKWATA na viongozi wake.
Aga Khan si mgeni Tanzania na waliomuingiza nchini ni Waislam katika miaka ya 1930 kwa ajili ya kutoa misaada kwa Waislam.
Katika miaka ya 1930 baba yake huyu Aga Khan wa sasa Shah Karim Al Hussein, Sir Sultan Mohamed Shah alitembelea Tanganyika na katika mradi mmoja wapo aliofika kuuangalia ulikuwa ujenzi wa shule ya Al Jamiatul Islamiyya School, Mtaa wa Agrrey na New Street uliokuwa ukijengwa na Waislam chini ya Al Jamiatul Islamiyya fi Tanganyika.
Katika hafla ile mwanafunzi aliyesoma risala mbele ya Aga Khan alikuwa Abdul Sykes.
Miaka mingi baadae Abdulwahid Sykes sasa kijana na mwanasiasa akajachaguliwa kuwa mjumbe katika Bodi ya Elimu ya Aga Khan).
Aga Khan alivutiwa sana na juhudi zile walizoonyesha Waislam wa Tanganyika za kutaka kujiendeleza katika elimu na akatoa fedha zilizowezesha kumaliza ujenzi wa shule yote kwa ukamilifu wake.
Aga Khan akatoa changamoto kwa Waislam wa Afrika Mashariki kuwa Muislam akichanga shilingi moja kwa ajili ya maendeleo ya umma yeye ataoa shilingi moja vilevile juu yake.
Huu ulikuwa sasa wakati wa East African Muslim Welfare Society (EAMWS).
Kitendo hiki cha Aga Khan kilikuwa msaada mkubwa kwa Waislam kwani wakati wa ukoloni ni Ukristo pake yake ndiyo ulikuwa na fursa ya kupata misaada kutoka nje.
Ushirikiano huu wa Aga Khan na Waislam wa Tanganyika uliendelea vizuri sana.
Aga Khan kupitia EAMWS alijenga shule nyingi hadi kufikia sasa kutaka kujenga Chuo Kikuu cha Kiislam chini ya usimamizi wa Mufti Sheikh Hassan bin Amir, Tewa Said Tewa na Aziz Khaki aliyekuwa mwakilishi wa Aga Khan Tanzania.
Hii ilikuwa mwaka 1968 baada ya Tanganyika kuwa huru.
Aga Khan na EAMWS kutaka kujenga chuo kikuu hapo ndiyo matatizo yakaanza baina ya Nyerere na uongozi wa EAMWS.
Kisa hiki ni maarufu hapana haja ya kukirejea.
Sasa tuingie kwenye kisa chenyewe.
Miaka mingi ikapita na mwishowe Nyerere akatoka madarakani na serikali ikashikwa na Ali Hassan Mwinyi.
Kwa takriban miaka 20 Aga Khan hakupata kutia mguu Tanzania.
Katika utawala wa Mwinyi Aga Khan akaja Tanzania.
Katika mazungumzo na Rais Mwinyi, Rais Mwinyi akaomba msaada wa Aga Khan katika nyanja tatu - Elimu, Kilimo na Afya.
Aga Khan akamueleza Rais Mwinyi kuwa Aga Khan walikuwapo Tanzania miaka ya nyuma wakisaidia katika elimu kupitia EAMWS.
Hili suala la elimu likamgusa sana Aga Khan kiasi cha yeye alipomaliza mazungumzo na Mwinyi akamwamrisha Katibu wa Elimu wa Aga Khan Tanzania, Riyaz Gulamani awakaribishe viongozi wa Waislam wa iliyokuwa EAMWS pamoja na viongozi wa BAKWATA katika chakula cha jioni ili wajadili maendeleo ya Waislam.
Katika viongozi wa EAMWS walioalikwa katika hafla ile alikuwa Tewa Said Tewa.
Kutoka BAKWATA walioalikwa walikuwa Sheikh Mkuu wa BAKWATA Hemed bin Jumaa, Adam Nasibu aliyekuwa katibu wa BAKWATA, Mustafa Songambele mzee wa CCM na mwanakamati katika BAKWATA na Waislam wengineo.
Kutoka EAMWS aliyealikwa alikuwa Tewa Said Tewa.
Baada ya chakula Aga Khan akawaeleza nia yake ya kuwaita na akawataka watoe wanachotaka wafanyiwe na Aga Khan katika elimu.
Hapa ndipo ''drama,' ilipoanza.
Akasimama kiongozi mmoja wa BAKWATA na mzee wa CCM, Mustafa Songambele, akamwambia Aga Khan, ''Serikali ya Tanzania inawatosheleza Waislam katika elimu na hawahitaji msaada kutoka kokote.''
Mustafa Songambele
Naomba nisimame hapa.
Mkasa huu kwa mara ya kwanza alinihadithia Riyaz Gulamani.
Sikuamini kama inaweza kuwa kweli.
Kisa hiki nikaja kuhadithiwa tena na Tewa Said Tewa kama vile alivyonihadithia Riyaz Gulamani.
Hapo ndipo nikaamini kuwa kisa kile hakika kilitokea na Mzee Tewa akanipa na jina la huyo aliyesema maneno yale.
Tuendelee.
Aga Khan kwa upole kabisa akajibu kuwa jana yake alikuwa na Rais na yeye kaomba msaada wa elimu.
Hapo sasa ndipo likazuka zogo baina ya viongozi wa BAKWATA na Waislam wengine mbele ya mgeni Aga Khan.
Kufupisha mkasa.
Kabla hajaondoka kufuatia yale aliyosikia na aliyoshuhudia, Aga Khan akamwambia Riyaz, ''Inaelekea hawa ndugu zetu bado hawajawa tayari lakini ushauri wangu ni kuwa uache mlango wetu wazi.
Siku yoyote watakapokuwa tayari basi tutatoa msaada.''Picha: Aga Khan na Songambele.