Wamiliki silaha kinyume na sheria kusamehewa

Wamiliki silaha kinyume na sheria kusamehewa

Hii misamaha kipindi hiki inapaswa kuangaliwa kwa makini.. Kuna walengwa wake pengine
Au kuna hofu kwamba ni nyingi mno, hakuna takwimu sahihi ya idadi/aina na huenda zikawa ni kishawishi zikatumika na wanoko siku isiyojulikana na kuitatiza amani yetu.
 
Jeshi la Polisi kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Innocent Lugha Bashungwa(Mb) kwa mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 66 cha Sheria ya Udhibiti wa Silaha na Risasi ya Mwaka 2015, Sura ya 223 na marejeo ya mwaka 2023 ametoa msamaha wa kutoshitakiwa kwa wamiliki wa silaha kinyume cha Sheria endapo watasalimisha silaha haramu kwa hiari kuanzia Septemba 1, 2025 hadi Oktoba 31, 2025

Kupitia Taarifa iliyotolewa leo Septemba 1, 2025 na Msemaji wa Jeshi la Polisi Msamaha huo ni moja ya juhudi na mikakati inayotekelezwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa ikiwemo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni utekelezaji wa Mikataba, Itifaki, Maazimio na Makubaliano mbalimbali ya Kuzuia Uzagaaji wa Silaha Ndogo na Nyepesi.

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa mtu yeyote atakayepatikana na silaha baada ya kipindi cha msamaha yaani baada ya Mwezi Septemba na Oktoba, 2025 atakamatwa na kuchukuliwa hatua zingine za kisheria.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi wote wanaomiliki silaha kinyume na Sheria kuhakikisha kuwa wanatumia fursa hiyo ya msamaha wa kutoshitakiwa uliotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pia, linawasisitiza wananchi wote ambao ndugu zao walikuwa wanamiliki silaha kihalali na wamefariki wahakikishe wanazisalimisha silaha hizo kulingana na masharti yaliyotajwa.View attachment 3462067
Je ikiwa ulimilikishwa kihalali na vibali vyote ila kwa kutolipia kila mwaka kwa mwaka mmoja hivi nayo inakuwa Silaha Haramu?
 
Jeshi la Polisi kupitia Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mhe. Innocent Lugha Bashungwa(Mb) kwa mamlaka aliyopewa chini ya Kifungu cha 66 cha Sheria ya Udhibiti wa Silaha na Risasi ya Mwaka 2015, Sura ya 223 na marejeo ya mwaka 2023 ametoa msamaha wa kutoshitakiwa kwa wamiliki wa silaha kinyume cha Sheria endapo watasalimisha silaha haramu kwa hiari kuanzia Septemba 1, 2025 hadi Oktoba 31, 2025

Kupitia Taarifa iliyotolewa leo Septemba 1, 2025 na Msemaji wa Jeshi la Polisi Msamaha huo ni moja ya juhudi na mikakati inayotekelezwa na nchi wanachama wa Umoja wa Mataifa ikiwemo Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ikiwa ni utekelezaji wa Mikataba, Itifaki, Maazimio na Makubaliano mbalimbali ya Kuzuia Uzagaaji wa Silaha Ndogo na Nyepesi.

Aidha taarifa hiyo imeongeza kuwa mtu yeyote atakayepatikana na silaha baada ya kipindi cha msamaha yaani baada ya Mwezi Septemba na Oktoba, 2025 atakamatwa na kuchukuliwa hatua zingine za kisheria.

Jeshi la Polisi limetoa wito kwa wananchi wote wanaomiliki silaha kinyume na Sheria kuhakikisha kuwa wanatumia fursa hiyo ya msamaha wa kutoshitakiwa uliotolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Pia, linawasisitiza wananchi wote ambao ndugu zao walikuwa wanamiliki silaha kihalali na wamefariki wahakikishe wanazisalimisha silaha hizo kulingana na masharti yaliyotajwa.View attachment 3462067
Wazifuate kwa watu waliotajwa na Mange sio kubweta barabarani kwa sababu mbwa koko hamsumbui mpita njia kuendelea na safari yake
 
Huu ni ubunifu katika mkakati wa kuondokana na uhalifu! Toa msamaha kwa mhalifu. Kutatua tatizo la ubakaji, toa msamaha kwa wabakaji; kadhalika, kutokomeza rushwa na wizi wa mali ya umma, toa msamaha kwa wahusika nk nk. Haijakaa sawa
 
Aisee kumiliki Tu silaha naogopa naiogopa naona km inaweza kufyatuka yenyewe ikanikula
 
Back
Top Bottom