Wamefanikiwa kwenye sekta Binafsi kwanini hawaitwi kuiokoa serikali?

Pamoja na mengi yaliyosemwa mimi bado naona tatizo la watanzania tulio wengi ni TIME MANAGEMENT,tuanze tukijiuliza sisi wenyewe hapa ni kwa jinsi gani tunatumia masaa yetu 8 ya kazi tuwapo maeneo yetu ya kazi?
na hii aijalishi ni kipato gani mtu anapata kwa mwezi kwa sababu utakuta mtu hayuko serious na kazi yake ukijaribu kumwuliza nini sababu atakwambia "aha mshahara wenyewe mdogo". OK sawa unajaribu kucheki yule anaelipwa mshahara ambao unaridhisha ukijaribu kucheck uwajibikaji wake ndo zero kabisa yaani yeye kaingia kazini saa mbili asubuhi saa mbili na nusu ameshatoka ofisini tena si mmoja karibia wahusika wote wa hiyo ofis wanaongozana kwenda kutafuta supu.
Na jaribu kuangalia hapo ukifika ofisin kwao unaambiwa wametoka kidogo utawaona wanarudi kila mmoja na chupa ya maji mkononi na meno wanachokonoa.
Hapo atashika kazi kidogo saa nne hao tena msururu eti kwenye chai mpaka saa tano watagusa tena kidogo.
Wakitoka hiyo ndo inayoitwa lunch atarudi saa tisa kufunga ofisi na kwenda nymbani na ndio daily routine hiyo.
Sasa kama kweli kwa siku unawajibika hardly masaa matatu kweli ni jinsi gani tutaweza kupima watanzania tunaweza au lah.

Wito wangu kwa watanzania wenzangu wakati umefika wa kubadilika kama tlivyokuwa na shauku ya kuona serikali yetu ikiwajibika ipasavyo nadhani ni vyema mabadiliko haya yakaanzia kwangu mimi na wewe kwani sisi ndio serilkali yenyewe.
 
  • Thanks
Reactions: ral
Sekta ya umma na sekta binafsi ni tofauti sana katika malengo, na hivyo mbinu za utendaji kazi nazo ni tofauti. Viongozi wa makapuni binafsi ni kutoa huduma ama kuendesha biashara ama shughuli kwa ajili ya kipato. mashirika ya umma, ni kutoa huduma hii kwa bei ambayo wananchi wake wataimudu - bei nafuu. Sasa kiongozi bora ni yule ambaye ataweza kupambanua gharama za huduma na kubuni vipato zaidi ya toza kwa wateja wake ili kuimarisha hiyo huduma.

Kwahiyo tusiwe wepesi kusema viongozi wa sekta binafsi wataweza zaidi - labda kama kila huduma lengo lake kuu itakuwa kutengeneza faida. Halafu hao walala hoi wanaenda wapi?
 
Wakiletwa serikalini wataharibu ulaji wa wakubwa hii ndo shida wakubwa walisha set mambo yao na mtu anapokuja na kujifanya yeye anataka kuleta mageuzi hawakawii kumuwajibisha kwa kulinda masilahi yao. Mashirika binafsi wanaweza kuleta mafanikio na mageuzi kwa sababu kule wanajali deliverance ya mtu mmoja 1 watu hawawezi wakakaa nawe kwenye kampuni na wakulipe hela ambayo mwezi mzima umefanya kazi na hukuingiza wao wanakuuliza sisi tuitoe wapi lakini serikali unalipwa hata kama hujafanya kazi hakuna sera ya uwajibikaji ila kuna sera ya kujali maslahi basi
 
One of the best threads of recent times, mimi sio wa muda mrefu JF lakini nimefarijika sana kuona old JF members wakichangia, wengine nilikuwa sijawahi hata kuona majina yao, MMKJ nakushukuru sana kwa kuleta hii thread, these are the intellectuals we need here in JF cheers!
 
I think EMT SAID IT ALL...
Ila mi naongezea,tatizo si utaalamu. Sisi na serikali iliyopo madarakani sasa kwa NUSU KARNE,tuna vichwa na tumeona vichwa,tumesomesha vichwa,na kusoma na vichwa ambavyo ni karibu sawa na genious yeyote kwa viwango vya IQ.. Kuna wakati nasema hatuwekezi kwenye akili za watu..

Ama tunatumia vibaya hivyo vichwa vilivyojidevelop vyenyewe.. Angalia ni vichwa vingapi hata hapo UDSM,na colleges nyingine.. Angalia vichwa vilivyoko abroad na jinsi huko wanavyoviheshimu... Baadhi vinaombwa hata vipewe uraia wa nyongeza,ili vitumike kudevelop nchi za ughaibuni..

CV ya Daudi Ballali kwa mfano,au hata huyu Omar Nundu,ama Haruna Lipumba,na vingine vingi... Pwenti yangu ni kwamba, hatuna UTASHI!!
Na tukiviita kwa ushawishi mkubwa vije kufanya kazi nchini kweye public sector,then tunavimisuse in one way or the other kwa siasa zetu zenye chembe ya unafikinafiki hivi...

No wonder vingine havitaki,kutokana na mfumo uliopo. Kwa pure scholars,au academicians,na baadhi ya watu wenye principles zao... Fedha,au mali,si kitu cha msingi kwao kuliko legacy. Kwamba nililitoa shirika fulani pale nilipolikuta hadi hapa sasa hivi unapoliona.. Wao wanajua,self esteem is unreachable..
Sasa hapa siasa zetu ndizo zinatuangusha..
 
Hakuna kitu kibaya duniani kama kuchanganya Siasa na Itifaki katika maswala ya UCHUMI...Tumeshindwa sehemu zote kutokana na mapungufu haya makubwa ktk jamii Kiutawala tulipoingia Ubepari.

1. Hatukuwahi kuunda mfumo wa ukombozi wetu kiuchumi - Tanzania Economic Liberalization Policy , hivyo kuweka umuhimu zaidi ktk mageuzi ili kujenga na kukuza Commanding Heights za Uchumi - Hadi leo hii hatuna viongozi ambao wana better understanding globalization na economic liberalization kutoka mfumo tuloutumia enzi za mwalimu. Nchi zote zilizotoka Ujamaa zilijenga misingi hii kwanza lakini sisi tulifanya nini?.. hakuna zaidi ya Azimio la Zanzibar ambalo linaondoa miiko na maadili ya uongozi na sii mageuzi ya Kiuchumi. Hivyo hadi leo hii tunashindwa kutambua wala kupanga forces, values, events na Ideas ambazo zinaenda sambamba na dunia ya leo kiuchumi (Global economic system) maana hatuna malengo.
- Mikataba mibovu ni ushahidi tosha kabisa ya uwezo wa viongozi wetu kufikiri.

2. Hatuna Necessities bali tuna Scarcities. Ukiona mahala palipo na ukosekanaji mara nyingi hapakuwa na umuhimu ndio maana kimekosekana. Hii inatokana na kukosekana kwa msingi bora wa Kiuchumi ktk kufikia malengo ya kuondokana na UKOSEKANAJI wa vyanzo vya kiuchumi. kwa mfano leo hii ni miaka zaidi ya 18 hatuna reli na maadam hatuoni UMUHIMU wake ndio maana hata shirika hilo halipewi kipaumbele.
- Kufa kwa mashirika ya Umma ni ushahidi tosha kwamba hatuoni UMUHIMU wa vyanzo.

3. Kifo cha Azimio la Arusha:- Baada ya kufa kwa Azimio la Arusha tumeshindwa kuweka AZIMIO jingine ambalo ndilo dira ya Kitaifa. Enzi za mwalimu tulijua vizuri tunataka kulijenge Taifa la aina gani lakini leo hii hatufahamnu zaidi ya neno UBEPARI..Sasa hata sisi ktk maisha yetu huwa tunaweka malengo, na mtu yeyote anayeishi pasipo malengo ni sawa na kuishi maisha ya Mbangaizaji ambayo hayana miiko wala maadili isipokuwa tumbo kwanza. Siku kwa siku na kuomba, Utapeli na ufisadi sio dhambi.
- Ufisadi uliopo ni uthibitisho wa kukosekana Miiko na maadili.


Kwa hiyo Mkuu Mwanakijiji, hakuna njia yoyote ya kusema hawa watu wakipewa madaraka ktk mashirika ya Umma wataleta mabadiliko - nasema - HAWAWEZI kuleta mabadiliko yoyote maadam mfumo mzima umetanguliwa na ukosekanaji wa kutambua tulipo na tunataka kwenda wapi?.
Na kumbuka tu hao waliofanikiwa ktk biashara zao wamecheza msondo ngoma ya ukae kama kawa!.. Yaani wamefanikiwa kupitia njia hizi hizi zilizopo ambazo hazina haramu. Haya ya CV ya mtu hayana sababu kabisa maana watu wanafikria ili uwe waziri wa Afya au naibu lazima uwe daktari! sii kweli kabisa, kwani ukiwa daktari ndio utajua vizuri madaktari wanatakiwa kulipwa mshahara na posho kiasi gani?

Binafsi naamini kabisa hakuna mfanya biashara hata mmoja aliyeweza kufanikiwa nchini bila kufanya haramu kwa sababu nchi nzima imekosa Miiko na Maadili..Na maadam biashara ni shughuli inayowahusisha watu wengine ni lazima utaifanya haramu kutokana na kukosekana kwa vitu hivyo hapo juu. Mashirika mengi ya nje yameingia nchini na kujaribu kufuata sheria za vitabuni WAME FAIL - yamefunga Ofisi zao na kuondoka wakilaani, isipokuwa yale yaliyokwenda na mfumo wa Ufisadi ndio yaliyofanikiwa.
 
Serikalini ni shamba la bibi, unaweza ukawa successful kwenye private sector kwa sababu kule kuna wenyewe so hauwezi kufanya upuuzi ila vitu vya serikali ni kama havina mwenyewe kwa hy unakula uwezavyo.

Ndo hali hakisi ya Tz yetu
 
Mkuu Eliahkamwela, sijakuelewa hata kidogo, nadhani MM Mwanakiji ametumia hekima zaidi kutokujibu. He is right.
Back to the point.
Kwa maoni yangu tatizo la Tanzania ni katiba mbovu. Huko Serikalini mtu ye yote akianza kuchapa kazi anakatishwa tamaa na bosi wake, ambaye naye ameshakata tamaa siku nyingi kutokana na yeye pia kukatishwa tamaa. kukatishana tamaa huko kunaanzia ngazi ya kitongoji kwenda juu hadi kwa mawaziri na bosi wao Rais. Ndo maana hali mbaya ktk sekta ya umma imeanzia kipindi cha Mwinyi hadi leo. Ifahamike kuwa serikalini hakuna check and balance and there is no accountability ambayo ilipaswa kuwepo kama tungekuwa na Bunge imara na mahakama imara. Kwa hiyo, waziri anafanya atakavyo as long as Rais hajui kumfuatilia au hawezi, at the same time anajua wabunge hawawezi kumfanya kitu cho chote. Na Waziri akiwa mchapa kazi anawafanya waliochini yake wizarani hadi ngazi ya chini yake wawe kama yeye, na akiwa vise versa (mla rushwa) the opposite is true (Bahati mbaya sekta ya umma haina watu wa jinsi hiyo).
Kwa upande Sekta binafsi top management ikiwa safi ina maanisha kuwa kila mtu lazima achape kazi na taasisi hiyo itasonga mbele daima.

Tupo pamoja mkuu,na nafarijika kwenye comments watu wamejaribu kutoa mifano;nilicho kuwa nikiuliza ni kwa nini MMM Hakutoa mfano wowote katika hayo aliyo yazungumzia...hilo tu!
 
Mwanakijiji hiyo hoja yako ni muhimu na kwa taarifa tu nasikia ilishawahi seculate serikali baada ya Msechu kuonekana kafanya vizuri kwenye shirika la nyumba (NHC), kuna watu walipropose serikali ifanye mabadiliko kuencourage watu ambao wanaonekana wanafanya vizuri kwenye mashirika binafsi waje serilakini kwa malipo mazuri, lakini kuna hardliners ndani ya system walipinga kwa nguvu na kufanikiwa kupachi issue. Kati ya watu ambao ajira zao ziliandaliwa ni bwana Mafuru aliyekuwa Voda, kabla ya watu wenye mtizamo tofauti kupindua hilo zoezi. Mimi naamini kuna Watanzania wapo wengi wanaweza ipaisha Tanzania, ila kuna watu wanafaidika na mfumo huu uliopo kamwe hawataki kuingiliwa kwenye masilahi yao
 
Kwa serikali ya hii ya awamu ya nne, nadhani labda mpaka Yesu atakaporudi duniani ndo ukiwaleta hao unaowataja hali inaweza badilika. Wengi waliamini Pinda angeleta mambo ya maana, angalia anakoenda!

Acha tu, kwa sasa hakuna atakayeweza kuubadili mfumo huu ulojengwa na mkuu wa kaya na genge lake!
 
Mfumo mpya wa ajira serikalini

Na Pascal Mayalla

Serikali haitaajiri watumishi wa umma wa kuanzia ngazi za maofisa waandamizi, bali sasa nafasi za kazi katika ngazi hizo, zitakuwa ni za uteuzi na zitagawiwa kwa watu wenye sifa walio ndani ya utumishi wa umma kinyume na ule utaratibu wa kuzitangaza kwa ushindani wa uwazi kwa kila mtanzania mwenye sifa kuwa na haki ya kuomba.
Uamuzi huo, umetangawa na Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bibi Hawa Ghasia, katika hafla ya kumuaga Mwenyekiti mstaafu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Jaji msataafu, Lameck Mfalila, makamishina wa tume hiyo na wafanyakazi waliostaafu, iliyofanyika mwishoni mwa wiki katika viwanja viwanja vya Leaders Club, Kinondoni jijini Dar es Salaam.
Waziri Ghasia emesema, uamuzi huo wa serikali, unafuatia mabadiliko ya Sheria ya Utumishi Namba 7 ya Mwaka 2002, yaliyofanywa na Bunge hivi katika kipengele cha ajira katika utumishi wa umma kwa ngazi za maofisa waandamizi sasa sio za ushindani wa wazi.
Waziri Ghasia amesema, lengo la mabadiliko hayo ni kuipunguzia serikali mzigo wa kuendesha mafunzo ya mara kwa mara kwa maofisa wanaoajiriwa toka nje ya serikali, na kusisitiza kuwapandisha vyeo maofisa wa serikali wenye sifa na utendaji wao unajulikana kutaleta tija zaidi kuliko kuajiri watanzania wenye sifa ambao utendaji wao haujulikani.
Hata hivyo Waziri Ghasia amesema uamuzi huo hauna maana kuwa watanzania wenye sifa walio nje ya serikali sasa hawana nafasi tena katika uongozi wa utumishi wa umma, ila bado watanzania wenye sifa wataendelea kuajira katika utumishi wa umma pale ambapo hakutakuwa na watumishi wa umma wenye sifa zinazotakiwa.
Naye Katibu wa Tume ya Utumishi wa Umma, Bibi Thecla Shangali, amewasisitizia watumishi wa umma kuzingatia taratibu sheria na kanuni katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku ili utendaji wa serikali upate mafanikio yaliyokusudiwa na kuleta tija kwa maendeleo ya taifa.
Mwenyekiti mstaafu wa Tume hiyo, Jaji Mstaafu, Lameck Mfalila, amesema anajivunia sifa ya kuwa Mwenyekiti wa kwanza wa tume hiyo iliyoundwa mwaka 2002 na mafanikio makubwa ya tume hiyo iliyoyapata katika kipindi kifupi ambapo ni pamoja na kubadilisha sura na mitazamo ya watumishi wa umma toka utumishi wa zamani ambao ni utumishii tuu mpaka sasa kwenye utumishi wa umma unazingatia matokeo huku ukifanya kazi kibiashara kwa kufuata kanuni za mikataba ya huduma kwa wateja.
Jumla ya makamishna watano wa tume hiyo ewamestaafu na mwenyekiti wao sambamba na wafanyakazi 3 wa tume hiyo akiwemo, Naibu Katibu wa tume hiyo, Bibi Prisilla Ole Kambainei.

Mwisho wa kunukuu
 
Unasikitisha sana!! no research...no data...no right to speak!!!
Mwaikambo aliyekuwa Bima (N.I.C) ni kabila gani?? inajulikana alipoifikisha bima yetu...
Serikalini walikuwepo na bado wapo wengi kutoka Kyela mbona watu bado wanalalamika??
Acha ukabila...Lawama siyo ya mtu mmoja wala kabila au dini bali ni ya mfumo...ambao tulirithi
toka kwa wakoloni na tukashindwa kuukarabati ili utunufaishe. Mfano ni tafsiri ya maneno "MALI YA UMMA"
haikuwekwa katika hali ya kila mtu ahisi kuwa ni yake na anawajibika kuilinda. Utaona watu wanasifiwa mitaani
kutokana na utajiri walioupata kutokana na wizi wa mali ya umma. Wengine wamefanikiwa kuwa watunga sheria
kupitia chama tawala na hata upinzani. wezi na waharibifu wa miundombinu mfano nyaya za umeme na simu, vyuma vya
madaraja, mabomba, alama za barabarani na nyara za serikali tunawajua, tunaishi nao mitaani, ni rafiki zetu, dada zetu, kaka
zetu na wazazi wetu, hatujajitolea kwa dhati kuilinda mali yetu. Badala yake kila jambo tumeligeuza kuwa siasa. Hakuna ukombozi wa maana tutakaoupata hata tukibadili majina ya vyama vitakavyounda serikali endapo FIKRA zetu hazitabadilika.

kwa taarifa yako mwaikambo hajaua bima baada ya kuondoka ndio bima imekufa si mlikuwa mnadai kaweka wanyakyusa je hawakuwa na qualification? hawakuperform?. nitajie mafisadi kumi tu tanzania uone kama wanatoka mbeya! watetezi mnawapa sumu. ni watu wapo straight na focus na watu wa principles sio nyie esp kaskazini mmeifanyia nini hii serikali zaidi ya kuiba.

mwakyembe na mwandosya wataishi milele kwa nguvu za mola!

katafute mipaka ya konde ndio utawajua wanyakyusa. mi sio mtanzania ni mkonde tena mmalawi.
watanzania mnashindwa hata kuendesha serikali kila kitu dili kila kitu kuiba, mnabagaini mishahara midogo ili muingie muibe, kila kitu fasta fasta hakuna anaefata sheria kuanzia barabarani mpaka maofisini then useme ni mfumo

NO TATIZO NI WATANZANIA WENYEWE NA SI MFUMO WALA JK WALA CCM
 
[/COLOR]
Mpumbavu,mjinga na ms**ng****** mkubwa wewe!
Nani kakwambia watanzania hatuna akili?
Kweli sisi wanyakyusa kwetu ni Malawi?
*********** WEEEEEEEEEE;Acha niishie hapa nisije kula ban;ndio kwanza nimetoka jela!!!

Du akili hizi za watanzania! ujanja ujanja, fasta fasta, kuvunja sheria ndo ujanja, kutukana ndio ujuaji

sasa mimi na ww nani katukana!

ndio upewe shirika uliongoze! unategemea nini hapa! bora mimi mmalawi!!!
 
Mkuu Eliahkamwela, sijakuelewa hata kidogo, nadhani MM Mwanakiji ametumia hekima zaidi kutokujibu. He is right.
Back to the point.
Kwa maoni yangu tatizo la Tanzania ni katiba mbovu. Huko Serikalini mtu ye yote akianza kuchapa kazi anakatishwa tamaa na bosi wake, ambaye naye ameshakata tamaa siku nyingi kutokana na yeye pia kukatishwa tamaa. kukatishana tamaa huko kunaanzia ngazi ya kitongoji kwenda juu hadi kwa mawaziri na bosi wao Rais. Ndo maana hali mbaya ktk sekta ya umma imeanzia kipindi cha Mwinyi hadi leo. Ifahamike kuwa serikalini hakuna check and balance and there is no accountability ambayo ilipaswa kuwepo kama tungekuwa na Bunge imara na mahakama imara. Kwa hiyo, waziri anafanya atakavyo as long as Rais hajui kumfuatilia au hawezi, at the same time anajua wabunge hawawezi kumfanya kitu cho chote. Na Waziri akiwa mchapa kazi anawafanya waliochini yake wizarani hadi ngazi ya chini yake wawe kama yeye, na akiwa vise versa (mla rushwa) the opposite is true (Bahati mbaya sekta ya umma haina watu wa jinsi hiyo).
Kwa upande Sekta binafsi top management ikiwa safi ina maanisha kuwa kila mtu lazima achape kazi na taasisi hiyo itasonga mbele daima.

Unapoint tatizo ni watanzania wenyewe, hizo secta binafsi zinawafosi wabadilike kwa nguvu bila kupenda na ambao wameshindwa kubadilika wameishia kupoteza ajira, na walioweza kwenda na huo mchaka mchaka ndio wameweza kufanikiwa

Angalia watanzania kila kukicha wanalalama oh wakenya wengi oh wakenya watatumeza!! ahghaaaaaa inatia hasira wea are you guys mcompete nao muwashinde sio!!

onyesheni uwezo kuwashinda na automatically hawataweza kusurvive sio kulia lia tu huku hamko compintent
 
Nilikuwa nimepata nafasi ya kuzungumza na jamaa zangu kadhaa ambao kwa kweli wamefanikiwa katika sekta binafsi hapo nyumbani. Wengi wa hawa jamaa walikuwa serikalini na baadaye wakaenda uraiani wakashiriki kuanzisha makampuni au mashirika na wamekuwa very successful. Namkumbuka mmoja wao ambaye alipopewa kampuni kuiendesha wafanyakazi walianza kulalamika ati "amepewa Mswahili, kampuni itakufa". Miaka kama kumi baadaye ni mojawapo ya mashirika yanayofanya vizuri zaidi Tanzania na yakiwa yamefikia viwango vya kimataifa.
Sasa katika kufuatilia fuatilia nikagundua ni kweli wapo Watanzania wengi tu ambao wameweza kujionesha wanaweza kuwa viongozi, na wasimamizi vizuri na wana principles za utawala nzuri na wamefanikiwa. Yaani, unaweza kabisa kuona kazi zao kiasi kwamba wakati mwingine mtu akiambiwa anayefanya hivi ni "Mtanzania" watu wanaonekana kushangaa kana kwamba Mtanzania hawezikuwa meneja au mtawala mzuri.
Sasa, ni hapo ndio nimejikuta najiuliza hasa tukiangalia mashirika kama Reli, ATC n.k na hata taasisi nyingine ambazo zinaonekana kuwa na matatizo ya kiutawala (kama hospitali zetu). Sasa najiuliza kwanini watu hawa wenzetu waliofanikiwa katika sekta binafsi na wana rekodi za kugeuza mashirika au makampuni na kuwa bora hawapewi nafasi au kuitwa hata kwa mkataba mnono wa kugeuza mashirika yaliyoshindwa? Hivi ni kweli kabisa tunahitaji menejimenti toka nje?
Fikiria kwa mfano Chizi wa ATCL amepewa kuligeuza hilo shirika hivi ni kwa kiasi gani amejitofautisha kuwa ni mtawala na meneja mzuri? Hivi, kumpa mtu Reli wakati hajawahi kuendesha kampuni yoyote ya maana au kuonesha kuwa anaweza kugeuza a non-profitable company into a profitable one inaingia akilini kweli?
Au ni kweli hawa Watanzania waliofanikiwa kwenye sekta binafsi ni tishio kwa wanasiasa hasa kama wataletwa kuendesha mashirika ya umma? Na kama wapo ni kama watu gani ambao unafikiria wanaweza wakawa wazuri sana kwenye serikali kwa sababu wana rekodi nzuri uraiani?

Huyu si kashalimwa barua kwa kuagiza uniform china?
pia kuajiri watu wapya wakati wanatakiwa kupunguzwa?
Kuendesha seminar na Training kupitia makampuni wakati shirika lina chuo chake?
 
Hao wafanyabiashara binafsi ungewataji, labda nasi tungekua na wazo tafauti na lako.

Kilicho muhimu ni kuwa serikali imeshindwa kazi, hata kama ikiwaingiza wafanyabiashara binafsi kwenye makampuni ya serikali, bado hayo makampuni ni ya serikali na yapo chini ya serikali hiyo hiyo iliyoshindwa kazi miaka 50 imepita. Ninachosema ni kua hata kama kampuni ya serikali X itatengeneza faida na hiyo faida ikapelekwa HAZINA basi huko hiyo pesa itapangiwa majukumu kifisadi na kitaahira kama kununua VX ama kupeleka wabunge India kupima Afya. Angalia JK alivyoandaliwa kua raisi kwa miaka mingi, lakini mtoto wa CCM ni CCM tu hata angekuwaje. Mashirika yetu kushindwa ni kwa sababu system ya serikali ya CCM ndio tatizo, sio watu - sio watanzania.

Ondoa CCM lete chama ingine ama na serikali ya majimbo (naamini MAJIMBO) - anayezalisha na ndiye awe anaamua pesa yake itumiwe vipi.
 
Back
Top Bottom