Nimekaa porini Mimi asikwambie mtu kuna mambo mawili yanayotumika kupumbaza wanyama Hata awe Mkali namna gani:
1.Dawa za kienyeji-Asilimia zaidi ya 90,dawa hutumika kupumbaza wanyama na hufanya kazi (Hii Ni sehemu ya uchawi)
2.Mbinu za kiakili-Kuna mazingira inatokea huna dawa na Uko msituni,unafanyaje,
Hawa jamaa pia wanafahamu tabia za kila mnyama na namna ya kumhandle Hata kama anataka kukudhuru,mbinu zote zime egemea kwenye ujasiri
Mfano.Ukikutana na Simba hurusiwi kutetemeka Wala kuonesha hofu yeyote Hata kama anabweka sentimita chache toka kwako,ukitikisika au kuonesha hofu tu usoni imekula kwako,
Ili Ku survive roho ya ujasiri inahusika,zipo mbinu nyingi tofauti tofauti kulingana na aina ya mnyama na Tabia yake