Mkuu haya maneno yamenikumbusha my bro alimuonyesha mchumba wake mdingi wetu. Mdingi akawa negative sana juu ya yule mdada mpaka mzee akanifuata na kuniambia kuwa yule dada hafai , mimi nilikua upande wa bro kwa hiyo nikamwambia baba ngoja nizungumze na bro kwanza . Nilimuuliza kaka yangu maswali ya msingi kuhusiana na yule mdada , maskini ya mungu kaka hakunielewa alijibu kisela , nilirudia mara nyingi kumuuliza kama anamjua mchumba wake kwa kina , akanidanganya hapo na kunipotezea. Basi nilimrudishia jibu mzee wetu kuwa maadam muoaji anasema binti anamfaa basi tumuachie aoe. Mkuu ile ndoa ina migogoro mpaka leo , yaani binti ni mshirikiana na kicheche tena anafanya laivu. So tusipuuze kila wakati wazai wanapokua negative na si kila wakati wawapo negative ni sahihi pia.