Just Pray
JF-Expert Member
- Nov 7, 2023
- 2,142
- 4,779
Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam, Albert Chalamila ametoa wiki mbili kwa wafanyabiashara ndogondogo walio katika barabara za kuingia soko kuu la Kariakoo kuondoka.
Hatua hiyo inakuja ikiwa ni kuelekea ufunguzi wa soko hilo, lililokuwa katika ukarabati tangu Julai 10, 2021 baada ya kuungua.
Kutokana na tukio hilo, Serikali ilitoa zaidi ya Sh28 bilioni kwa ajili ya kulikarabati, ukarabati ulioenda sambamba na ujenzi mpya wa soko dogo.
Katika kipindi chote hicho wafanyabaishara waliokuwa wakifanya shughuli zao sokoni hapo, walihamishiwa katika masoko ya Kisutu, Karume na Machinga Complex.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumatano Mei 28, 2025 kuhusu maendeleo ya soko hilo, Chalamila amesema tayari limeshakamilika kwa asilimia 98 na kinachofuata ni maandalizi ya kulifungua japo hakuweka wazi tarehe rasmi.
Kati ya maandalizi hayo amesema ni pamoja na kuwaondoa Wamachinga waliopo barabara za kuingia sokoni hapo, na tayari wameshawapa maagizo viongozi wao.
“Mpaka sasa ninapozungumza soko limeshakamilika kwa asilimia 98 na kubakia matengenezo madogo madogo ikiwemo uzio.
“Baada ya hapo kinachosubiriwa ni Waziri mwenye dhamana wa Tamisemi, kufanya ziara ya mwisho kukagua na kujiridhisha ukamilifu wake kabla halijaja kuzinduliwa, uzinduzi unaotarajiwa kufanywa rasmi na Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema Chalamila.
Hata hivyo ameleleza kuwa pindi soko hilo litakapofunguliwa kuna utaratibu umewekwa wa kuwapa baadhi ya maeneo wamachinga, ambapo kuna maduka madogo watawekwa ili kupunguza adha hiyo ya wao kukaa barabarani.
Wakati Chalamila akisema hayo, Makamu Mwenyekiti wa Wamachinga Tanzania na Mwenyekiti Soko la Kariakoo, Stephen Lusinde,amesema kazi ya kuwaondoa si kubwa kwao kwa kuwa hata wamachinga wenyewe wanajua maeneo hayo wameyavamia.
Lusinde amefafanua kuwa tangu awali wakati wanawapanga maeneo hayo ya Kariakoo, kuna barabara za mitaa walikubaliana waziache wazi na nyingi ndio hizo zinazoingia katika soko hilo.
Ametaja barabara hizo kuwa ni pamoja na ile ya Mtaa wa Nyamwezi -Mkunguni, Nyamwezi-Tandamti, Tandamti-, Sikukuu -Mkunguni na Mkunguni – Congo (Bigborn).
“Katika maeneo hayo wafanyabiashara wanaelewa kuwa tulishakubaliana pawe wazi ila kwa wale wakaidi waliamua tu kuvamia na wengine maeneo wanayo walishapangiwa, hivyo ikifika muda tutafanya kazi yetu na hakutakuwa na wa kumlaumu,” amesema Lusinde.
Kuhusu na wao kupata maeneo ya kufanya biashara ndani ya soko hilo la kimataifa, Mwenyekiti huyo amesema ni taarifa njema kwao ukizingatia ni kilio chao cha muda mrefu, huku akieleza vipaumbele vitakuwa kwa wale ambao hawakuwa na maeneo na tayari wapo katika kanzidata yao.
Mmoja wa machanga ambaye hakutaka jina lake liandikwe, ameshauri wangeachwa mpaka hapo uhakika wa soko litakapofunguliwa, kwa kuwa ni sehemu ambayo wanategemea kupata rizki kwa sasa.
Chanzo Mwananchi
Hatua hiyo inakuja ikiwa ni kuelekea ufunguzi wa soko hilo, lililokuwa katika ukarabati tangu Julai 10, 2021 baada ya kuungua.
Kutokana na tukio hilo, Serikali ilitoa zaidi ya Sh28 bilioni kwa ajili ya kulikarabati, ukarabati ulioenda sambamba na ujenzi mpya wa soko dogo.
Katika kipindi chote hicho wafanyabaishara waliokuwa wakifanya shughuli zao sokoni hapo, walihamishiwa katika masoko ya Kisutu, Karume na Machinga Complex.
Akizungumza na waandishi wa habari jana Jumatano Mei 28, 2025 kuhusu maendeleo ya soko hilo, Chalamila amesema tayari limeshakamilika kwa asilimia 98 na kinachofuata ni maandalizi ya kulifungua japo hakuweka wazi tarehe rasmi.
Kati ya maandalizi hayo amesema ni pamoja na kuwaondoa Wamachinga waliopo barabara za kuingia sokoni hapo, na tayari wameshawapa maagizo viongozi wao.
“Mpaka sasa ninapozungumza soko limeshakamilika kwa asilimia 98 na kubakia matengenezo madogo madogo ikiwemo uzio.
“Baada ya hapo kinachosubiriwa ni Waziri mwenye dhamana wa Tamisemi, kufanya ziara ya mwisho kukagua na kujiridhisha ukamilifu wake kabla halijaja kuzinduliwa, uzinduzi unaotarajiwa kufanywa rasmi na Rais Samia Suluhu Hassan,” amesema Chalamila.
Hata hivyo ameleleza kuwa pindi soko hilo litakapofunguliwa kuna utaratibu umewekwa wa kuwapa baadhi ya maeneo wamachinga, ambapo kuna maduka madogo watawekwa ili kupunguza adha hiyo ya wao kukaa barabarani.
Wakati Chalamila akisema hayo, Makamu Mwenyekiti wa Wamachinga Tanzania na Mwenyekiti Soko la Kariakoo, Stephen Lusinde,amesema kazi ya kuwaondoa si kubwa kwao kwa kuwa hata wamachinga wenyewe wanajua maeneo hayo wameyavamia.
Lusinde amefafanua kuwa tangu awali wakati wanawapanga maeneo hayo ya Kariakoo, kuna barabara za mitaa walikubaliana waziache wazi na nyingi ndio hizo zinazoingia katika soko hilo.
Ametaja barabara hizo kuwa ni pamoja na ile ya Mtaa wa Nyamwezi -Mkunguni, Nyamwezi-Tandamti, Tandamti-, Sikukuu -Mkunguni na Mkunguni – Congo (Bigborn).
“Katika maeneo hayo wafanyabiashara wanaelewa kuwa tulishakubaliana pawe wazi ila kwa wale wakaidi waliamua tu kuvamia na wengine maeneo wanayo walishapangiwa, hivyo ikifika muda tutafanya kazi yetu na hakutakuwa na wa kumlaumu,” amesema Lusinde.
Kuhusu na wao kupata maeneo ya kufanya biashara ndani ya soko hilo la kimataifa, Mwenyekiti huyo amesema ni taarifa njema kwao ukizingatia ni kilio chao cha muda mrefu, huku akieleza vipaumbele vitakuwa kwa wale ambao hawakuwa na maeneo na tayari wapo katika kanzidata yao.
Mmoja wa machanga ambaye hakutaka jina lake liandikwe, ameshauri wangeachwa mpaka hapo uhakika wa soko litakapofunguliwa, kwa kuwa ni sehemu ambayo wanategemea kupata rizki kwa sasa.
Chanzo Mwananchi