Walioingiza mabomu Arusha wakamatwa!

Walioingiza mabomu Arusha wakamatwa!

Chako hicho kinatwa kiherehere, kwani ukisubiri ukajua atakuja nalo, ungevunjika guu, tuwaache polisi wafanye kazi yao, sisi tutakuwa na usemi tukishapata habaro kamili. au kuna unalolijua na unataka kutupotezea dira. ama umetumwa na wanaohusikana huo ujangili na uuaji wa ndugu zetu, ili utatie wasiwasi na mashaka na kuiharibu kesi.

Kutumika bila kujijua ni jambo baya na hatari kwa mtu mwenye akili ambaye unaona kijani kisha unaita njano!!
 
Kuingiza mabomu mawili yenye ukubwa wa ngumi huwa kunakua na zabuni?
 
Kwa hiyo Mkuu wa Mkoa (Mulongo Muongo) ndio amekuwa mpelelezi na msemaji wa jeshi la polisi?
 
wanataka kutusahaulisha balozi wa china na kofia lake la ccm.
 
Mulongo alisema kwa sasa Polisi iko katika hatua za mwisho za mahojiano na watuhumiwa hao, ambapo mbali na kutaka kufahamu waliowatuma na malengo yao, pia wanatarajia kupata taarifa za waliorusha mabomu hayo.

Malengo mengine kwa mujibu wa Mulongo ni kuwafahamu watu wote waliopewa zabuni ya kuingiza mabomu hayo, ili hatua za kisheria zifuate.

Kuna watu wana zabuni za kuingiza mabomu nchini?? Kama walipewa zabuni kwa nini sasa wanawatafuta waliowatuma?? Ina maana hiyo zabuni siyo ya jeshi?? Kama ni zabuni ya watu binafsi, inawezekanaje??

Hivi lile bomu la kanisani si mwanzo walisema lilitengenezwa mtaani. Sasa mbona story inabadilika?? Au ndiyo kushindwa kazi huko kwajeshi la polisi na UWT??
 
Sijamwelewa aliposema "TUMESHAWAKAMATA WATU WALIOINGIZA BOMU NCHINI" Sasa hapa mbona huyu Mulongo anatuchanganya? amemkamata lini wakati juzi Mh. NCHEMBA NKULU aliposti post yake humu jamvini inayoeleza yupo USA kwa muda wa siku30 kwa shuhuli za kichama.
Sasa naomba kuuliza hiv Mwigulu amesharudi?
 
hofu yangu CCM isije ika plant watu wakaja kusema wameagizwa viongozi wa cdm ili kuiangamiza CDM! some one can be bought with millions so we must be keen and prepare for any that can happen saikologicaly
 
Taarifa zilizosomwa sasa hivi TBC ni kwamba wale wote waliolipua mabomu katika kanisa la Olasiti na mkutano wa CHADEMA na kuua watu na wengine wengi kujeruhiwa wote wamesha kamatwa na wako polisi kwa mahojiano zaidi.

Sasa ngoja tusubiri kama watapatikana na hatia au laa au itakuwa sinema kama ya kamanda Kova na mateso ya Dr Ulimboka.
 
Hongereni kwa kuwakamata hao watu ila bado mapema, tunataka haki itendeke kwa wafiwa na waliojeruhiwa isiwe nguvu ya soda
 
Taarifa zilizosomwa sasa hivi TBC ni kwamba wale wote waliolipua mabomu katika kanisa la Olasiti na mkutano wa Chadema na kuua watu na wengine wengi kujeruhiwa wote wamesha kamatwa na wako polisi kwa mahojiano zaidi
Sasa ngoja tusubiri kama watapatikana na hatia au laa au itakuwa sinema kama ya kamanda Kova na mateso ya Dr Ulimboka
Mbona unatoa hoja kwa kujishuku kama unaoga nje?
Acha vyombo vya dola vifanye kazi yake wewe subiri matokea maswala ya ulimboka yanatoka wapi waharifu hamjifichi.
 
Lakini tuwape hongera vyombo husika kama vimeweza kuwakamata wahusika.
 
Kuna uhusiano wowote tukio lililotokea zenj hivi karibuni? Hii timing inatia mashaka sana.

Tangu "waliposhindwa" kujua aliyeemuua Mwangosi na aliyemteka na kisha kumtesa Dr Ulimboka, sijapata kuwaamini tena polisi wetu.
 
Bidhaa feki - China
Wawekezaji - China
Gesi inaenda - China
Bomu & Risas - China
Baloz mwenez - China

Unahangaika nini kujua ukweli hapo..? CCM na China wapo vitani dhidi ya watanzania na rasilimali zao.
 
Back
Top Bottom