Mwanafunzi wa darasa la nne huko kijijini alikuwa akisafiri na baba kwenda mjini kwa shangazi yake. Basi lilipoanza kuingia mjini mtoto wa watu alikodoa jicho dirishani si kidogo, na alionekana kuwa anatafakari jambo. Mara akamgeukia baba yake na kumwuliza:-
Mtoto:- Baba, walimu wa mjini wana akili sana kuliko wa kijijini?
Baba:- Hapana mwanangu, wote wako sawa.
Mtoto:- Baba, walimu wa kijijini ni wavivu na wana upendeleo kuliko wa mjini?
Baba:- Hapana mwanangu, wote wako sawa. Kwa nini unauliza hivyo mwanangu?
Mtoto:- Baba, walimu wetu usahihisha kwenye daftari zetu tu na unaweza kupata vema au kosa, lakini huku mjini ni kosa tu tena mpaka majumbani na vibaoni barabarani.
Mtoto:- Baba, walimu wa mjini wana akili sana kuliko wa kijijini?
Baba:- Hapana mwanangu, wote wako sawa.
Mtoto:- Baba, walimu wa kijijini ni wavivu na wana upendeleo kuliko wa mjini?
Baba:- Hapana mwanangu, wote wako sawa. Kwa nini unauliza hivyo mwanangu?
Mtoto:- Baba, walimu wetu usahihisha kwenye daftari zetu tu na unaweza kupata vema au kosa, lakini huku mjini ni kosa tu tena mpaka majumbani na vibaoni barabarani.