Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Kuna Walimu wengine wana magari yao wenyewe au wenza au marafiki wana magari kwa nini Serikali isiwape posho ya usafiri kama Wabunge wanavyopatiwa ili waweze kugharamia usafiri kwa namna wanayoifahamu wao? Ki ukweli huu ni uzalilishaji na hasa ukizingatia ukweli kwamba pamoja na Wamiliki hao kuridhia mpango huo wa kumtafutia Mkubwa Fulani umaarufu wa bei nafuu, sithani kwamba wamepiunguza kiasi cha fedha ambacho kinapaswa kuwasilishwa kwa siku na waendeshaji wa vyambo hivyo vya usafiri kwa maana ya Dereva na Kondakta. Sipati picha majina na maneno watakayopewa Walimu na Wakondakta wa Daladala.

Ni v ema chama cha Walimu kingepinga udhalilishaji huu wa kidiplomasia
 
serikali italeta magari ya walimu kama tunayoona idara nyingine kama mahakama, mem, bot etc? kama ni huu usafiri wa umma haitawezekana

Nakumbuka mwanzoni mwa miaka ya 1990 wamiliki wa daladala jijini Dar waliunda umoja wao ulioitwa Muungano wa Wamiliki wa Daladala (MUWADA) uliokuwa chini ya uenyekiti wa George Ndaombwa. Na ndio wakati walitoa ruhusa kwa askari kupanda bure - uamuzi ambao uliigwa na wasafirishaji wa daladala kote nchini.
 
Ivi mnao kubaliana na makonda mnaona kafanya kwa ajili ya walimu au kujipendekeza kwa mkubwa ili apate kitu? nani aliyesema bure inalipa mtoto alipe nauli mwalimu asilipe wasiwachezee walimu wetu wawape fedha kwa kulipia nauli hii ni kuwadhalilisha walimu.
 
hao ni walimu wa serikali au private kama wanataka kufanya hivyo wangefanya utafiti wa kutosha lakini machi 7 sidhani kama watakuwa wamekamilisha taratibu zote
 
Kutakuwa Na Changamoto Nyingi Sana Katika Hili, Nayeye Mkuu Wa Wilaya Ndi Msemaji Wamkoa? Mbona Sielewilewi Limekaaje Hili Tusubiri Tuone
 
Changamoto ni kubwa sana kwa madereva na makonda hasa katika swala la hesabu ya tajiri. Kumbuka mda huo wa asubuhi na jioni ndio mda wa kupata nyomi la uhakika. Na hawa waalimu watakua hawana sare kama wanafunzi na askari hivyo basi unaweza kukuta nusu ya basi ni waalimu hapo ni hasara kwao. Maaskari kidogo ni afadhali sio shida kuwabalance wakishaingia wawili au watatu akija mwingine akielezwa na konda anaelewa. Sasa hawa waalimu na vitambulisho kimyakimya si kuna siku dereva atajikuta ameenda patupu. Suluhisho ni kuwanunulia mabasi yao kama ilivyo kwa wanajeshi. Mengine ni kujaza maji pipa kwa kisoda.
 
Tatizo awa jamaa wanakurupuka tu awaangalii baadae inakuaje sasa hapo sijui Na madereva Na makondakta wataupunguziwa pesa za kupeleka kwa ma boss wao mana uwaga wanaviwango vya kupeleka kwa wamiliki wa magari mana isije kua wamiliki magari wamepanga pasipo kuweka sawa kwa upande wa madereva wao
 
Wamekubali kwa roho nyeupe, ila ningeshauri waweke namba zao za simu kwenye vitambulisho au magari husika ili itokeapo vinginevyo walimu husika wawajulishe
 
Kama watatengenzewa kitambulisho ambacho kinawekeka mfukoni au kwenye handbags sioni Kama kutakuwa na manyanyaso mana mwalim ataingia kwenye Gari bila hata kujulikana Kama ni mwalim ila wakat wa konda anadai chake ndo pale anaonyeshwa kitambulisho, pia nafkiri iwekwe sheria kali kwa konda yoyote atakae mnyanyasa mwalim.mbona hatujawah kuskia wanajeshi wananyanyasika kwenye madaladala? Hii nchi sheria zikisimamiwa vizuri kila mtu atakuwa na adabu na hata mwanafunzi anaweza kusafiri bure tuache ujinga ujinga
Tumewaangalia walimu.... Makondakta na Madereva nao wako kazini, ikiwa bure kwa walimu nani atakayewalipa vizuri hawa wenzetu amabao kila siku inatakiwa hesabu ya bosi...."tumewafikiria kwenye mikataba na haki zao je, hili nalo si litabadilisha maslahi yao pia? nafikiri serikali iangalie namna ya kutoa ruzuku ili wasiwaumize wengine. au la magari ya serikali yatumike kutekeleza utaratibu huo"
 
.....

Muda wa kuwasafirisha bure ni saa 11.30 hadi 2 asubuhi na saa 9 hadi 11 jioni.
Unakaa foleni masaa matatu...ruhusa ya kitambulisho ni masaa 2...kwa konda ninavyowajua atasubiri muda huo upite ndiyo akusanye nauli vinginevyo ushuke njiani kabla muda wa kusafiri bure mwalimu haujaisha.

Hivi hapa mbona Mh. M. Saddiq hausishwi...na au Makonda ndiye mkuu wa mkoa wa Dar siku hizi.
 
Tangazo hi kalitoa kwa upande wa Kinondoni au Dar mzima Hivi mkuu wa mkoa kastaafu?
Kuna jamaa walilalamika kuwa Makonda anaigilia kazi zao... Usikute na Mkuu wa mkoa nae analalamika kimoyomoyo! Hahahahahaaaa
 
Hiyo nauli bure kwa walimu itakuwwa endelevu
??? where is the source of funding hiyo nauli bure???
 
Walimu bure, wanafunzi wao wanalipa nauli sh 200.

Angalia kitakachotokea:
1. Mwanzoni makonda (wa daladala, siyo Paulo) na madereva watakuwa wanawagundua walimu baada ya kuonyeshwa vitambulisho wakati walimu wameshapanda.

2. Baada ya muda makonda & madereva watawakariri walimu wa njia/route/vituo vyao na watakuwa wakiwakimbia na kupaki mbele zaidi au nyuma zaidi, na kuchukua abiria juu kwa juu ili mradi kuwakwepa walimu. Wenzangu tuliosomea Dar Form One to Six tunajua issue za daladala na madenti, sembuse walimu wasiolipa hata senti tano?
Kumbuka hesabu ya tajiri ipo palepale, haijalishi walimu wanalipa au hawalipi.

3. Matokeo ya walimu kukimbiwa na daladala (baada ya kukaririwa sura) ni kwamba ndio watachelewa zaidi kufika kazini/shuleni kuliko ilivyo sasa.
 
Yaani walimu na askari wanaolipwa mishahara hata kama ni kidogo wasafiri bure halafu mwanafunzi asiyekuwa na ajira wala mshahara alipe 200. Hivi kama mwalimu utasikiaje uko kwenye basi pamoja na wanafunzi wako wao wanalipa wewe hulipi? Mimi naona ni bora kungekuwepo na ka alawansi fulani hata kama ka 20,000 kwa mwezi kwenye ka mshahara ka mwalimu au huyo askari ili walipe nauli na sio kwenda bure. Hivi baadaye makonda wakiwataka walimu hao kusimama kama wanafunzi kwakuwa hawalipi nauli si watadhalilika sana? Bure nyingine zina gharama jamani! Sasa na daktari na manesi nao wanafikiriwa vipi? Maana nao ni watu muhimu sana katika kuokoa maisha yetu? Daktari na nesi wanakwenda kumhudumia mgonjwa ambaye hata ndugu wanaogopa kumshika halafu alipe nauli? Na mhudumu wa chumba cha maiti je?! Yeye anakaa na kuhudumia maiti ambazo wengine wanazikimbia. Huyo si muhimu? Bora wangesema wanafunzi wasilipe lakini sio walimu. Sasa mwalimu akiwa na mwanae ndani ya basi mwanae analipa halafu yeye halipi? Konda akianza masimango anawasimanga wote wawili. Wapeni transpoti alawansi!
 
Back
Top Bottom