Waufukweni
JF-Expert Member
- May 16, 2024
- 5,174
- 17,635
Kupanda kwa bei ya mafuta hususani petroli, makali yameanza kung'ata jijini Mbeya baada ya usafiri wa daladala kuweka 'mgomo' kutoa huduma huku wananchi wakilia na nauli za bajaji zilizofikia Sh2,000 kutoka Sh800 za awali.
Mbali na wananchi, wapiga debe nao wamepaza kilio chao wakieleza kuwa hawaelewi hatima ya maisha yao kwa kuwa riziki zao zinategemea zaidi uwapo wa daladala wakiomba Serikali kukaa na wamiliki wa vyombo vya moto kulimaliza ili shughuli ziendelee.
Bei ya lita moja ya mafuta kwa Jiji la Mbeya Machi iliuzwa Sh2,996 na sasa imefika Sh3,952 kwa lita moja, hali ambayo imeonekana kutesa wananchi ambao leo baadhi yao wameamua kutembea kutokana na daladala kutotoa huduma na kiwango kipya cha nauli.
Kutokana na huduma ya usafiri wa daladala kukosekana, baadhi ya usafiri uliotumika ni gari dogo aina ya Noah, guta huku bajaji nazo zikitumika kutoa huduma kwa bei zaidi ya ilivyokuwa awali.
Wakizungumza leo Aprili 2,2026 baadhi ya madereva wa bajaji wamesema wamefikia hatua ya kupandisha bei ya nauli kutokana na bei ya mafuta kupanda tofauti na ilivyokuwa awali , huku madereva wa daladala wakiomba kupandisha hadi Sh1,500.
Akizungumzia changamoto hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Solomon Itunda, amesema anaendelea na kikao cha wadau wote wa usafirishaji jijini humo, akifafanua kuwa baada ya mazungumzo ya pande zote Serikali itatoa msimamo na utaratibu kwa ujumla.
"Nipo kwenye kikao na wadau wote wa usafirishaji wakiwamo daladala, bajaji, gari kubwa na wengine wote, hivyo tukimaliza Serikali itatoa utaratibu kumaliza tatizo hili" amesema Itunda.
Mbali na wananchi, wapiga debe nao wamepaza kilio chao wakieleza kuwa hawaelewi hatima ya maisha yao kwa kuwa riziki zao zinategemea zaidi uwapo wa daladala wakiomba Serikali kukaa na wamiliki wa vyombo vya moto kulimaliza ili shughuli ziendelee.
Bei ya lita moja ya mafuta kwa Jiji la Mbeya Machi iliuzwa Sh2,996 na sasa imefika Sh3,952 kwa lita moja, hali ambayo imeonekana kutesa wananchi ambao leo baadhi yao wameamua kutembea kutokana na daladala kutotoa huduma na kiwango kipya cha nauli.
Kutokana na huduma ya usafiri wa daladala kukosekana, baadhi ya usafiri uliotumika ni gari dogo aina ya Noah, guta huku bajaji nazo zikitumika kutoa huduma kwa bei zaidi ya ilivyokuwa awali.
Wakizungumza leo Aprili 2,2026 baadhi ya madereva wa bajaji wamesema wamefikia hatua ya kupandisha bei ya nauli kutokana na bei ya mafuta kupanda tofauti na ilivyokuwa awali , huku madereva wa daladala wakiomba kupandisha hadi Sh1,500.
Akizungumzia changamoto hiyo, Mkuu wa Wilaya ya Mbeya, Solomon Itunda, amesema anaendelea na kikao cha wadau wote wa usafirishaji jijini humo, akifafanua kuwa baada ya mazungumzo ya pande zote Serikali itatoa msimamo na utaratibu kwa ujumla.
"Nipo kwenye kikao na wadau wote wa usafirishaji wakiwamo daladala, bajaji, gari kubwa na wengine wote, hivyo tukimaliza Serikali itatoa utaratibu kumaliza tatizo hili" amesema Itunda.