Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Vipi kuhusu askari


Akili yako haijapishana sana na ya Makonda au Makondakta.
Askari kinachowasaidia ni Uniform wanazovaa.
Na huko Dsm tu lakini baadhi ya mikoa wanalipa nauli hasa wanapokwenda mbali.
Askari akivua gwanda anadaiwa nauli kama kawaida na akimzingua konda basi ni vurumai nguo kuchanika.

Hili la walimu litakua gumu sana kutekelezeka kwani hata askari hawalipi nauli kisheria bali ni ile hali tu ta makondakta kuwaonea aibu na mara nyingine ni kama wanabebana. Yaani mfano trafiki na madereva ni watu wanaofanya kazi pamoja barabarani na kila mmoja ananafasi ya kumpa mwenzake unafuu kwa kumsidia kwenye utafutaji wake.
Askari anaweza akamsamehe dereva wa daladala aliyefanya kosa na hivyo dereva huyo kunusuru hela yake iliyokuwa itoke kama faini hivyo dereva huyo atakuwa na nafasi kubwa ya kumbeba akari bure akiwa na uniform au akiwa anamfahamu.

Kwa walimu ile ni siasa tu lakini ni ngumu mno kutekelezwa bila kutungiw sheria .

Cha msingi ni kuwawekea walimu wote posho maalum ya Usafiri ,maji,umeme na kodi ya nyumba. Pia wajengewe nyumba karibu na Shule.
Makonda angehamasisha ujenzi wa nyumba za walimu ili waishi karibu na shule zao.

Ikimbukwe kuwa Wamilikibwa daladala ni wafanyabiashara na makondakta nao wanataka posho za kuendesha maisha yao ambayo ni duni sana.
Makonda aishawishi serikali yake iwalipe walimu posho usafiri ili kuwajengea heshma zaidi walimu na sio kuwaombea lift kwenye magari ya watu.
 
Kwa nini wasianze na magari yote ya serikali yawe yanatumika kuwabeba walimu popote yanapopita bila kuwaacha kama ilivyo sasa. Akianza na gari lake mwenyewe ambalo linagharamikiwa na kodi ya watanzania wote?
 
Toa suluhu ya hayo uliyoyahisi kuwa yatatokea. Mbona tu mafundi wa kulalamika na kufikilia kushindwa tu?
wadau wamejitahidi kutoka Mawazo chanya kama mbadala wa wazo la makonda,ni kweli walimu hawatazuiliwa kupanda daladala maana hawavai sare lakini watakutana na lugha ya kuudhi kutoka kwa makondakta tena mbele ya wanafunzi wao,hili wazo limekaa kisiasa zaidi ni ubunifu usiokuwa na tija yoyote ya maana
 
Ilikuwa bora kupigania posho ya nauli iwepo kwenye mishahara kuliko hili la kusafiri bure. Hilo litaleta usumbufu mkubwa sana.
 
Hapana wakopeshwe magari.Wanafunzi kwenye daladala wanaitwa wa kusoma je walimu wataiwaje?labda teacher au wakufundisha.
 
Jinsi inavyotangazwa imekuwa kama vile walimu wanaenda kupanda magari bure kabisa.Tunaelezwa hapa kuna mambo wamekubaliana na wammiliki wa vyombo vya usafiri.

Kuondoa hii hali ya kudhania walimu watakuwa burden wangeusema huo mpango wenyewe....

Wangesema kabisa hiyo hela italipwaje na kwa mechanism gani ili kuwapa confidence walimu ndani ya madaladala kuwa hawalipi kabisa.Yaani hata tangazo lao lingekuwa maybe 'halmashauri kugharamia nauli za walimu kinondoni'na hapo wakauweka wazi huo mpango wenyewe wa makubaliano.Haya mambo ya kuwafananisha walimu na wanafunzi wao yasingekuwepo.

Waseme kwa mfano kuanzia tar 7 march walimu hawatatoa keshi kwenye daladala.Kwamba halmashauri itawapa vocha maalumu walimu ambazo zitajazwa na watu wa magari mwalimu akiwa kwenye gari.Ijazwe namba ya kitambulisho cha mwalimu,jina,namba ya gari pamoja na acount details za wenye gari.Kopi inabaki kwa watu wa gari kopi inarudi kazini ambako mwisho wa mwezi deni linalipwa kwa kiasi kinachoonekana kwenye kumbukumbu zilizopo halmashauri na kwao watu wa magari wenyewe.Kama hela italipwa kwa wakati kutakuwa hakuna dhalili kabisa na walimu hawatakataliwa na wenye magari.Hii ni postpaid lakini inaweza kubuniwa pia ikawa prepaid
 
Kama watatengenzewa kitambulisho ambacho kinawekeka mfukoni au kwenye handbags sioni Kama kutakuwa na manyanyaso mana mwalim ataingia kwenye Gari bila hata kujulikana Kama ni mwalim ila wakat wa konda anadai chake ndo pale anaonyeshwa kitambulisho, pia nafkiri iwekwe sheria kali kwa konda yoyote atakae mnyanyasa mwalim.mbona hatujawah kuskia wanajeshi wananyanyasika kwenye madaladala? Hii nchi sheria zikisimamiwa vizuri kila mtu atakuwa na adabu na hata mwanafunzi anaweza kusafiri bure tuache ujinga ujinga
Nimependa argument yako. Naunga mkono pendekezo kuwa waandae utaratibu wa Kondakta yeyote yule atakayetoa lugha ya kashfa, kejeli ama matusi kwa mwalimu kisa kapanda gari BURE basi na achukuliwe hatua KALI za kisheria. Maana kwa wanajeshi na askari polisi huwa hawanyanyaswi ila kwa kuwa walimu hawatumii silaha basi itakuwa kimbilio. Na OLE wao
 
Sema wilaya ya kinondoni, sio Dar es salaam. Kwa kusema dar es salaam unamaanjsha jiji zima, hivyo mkuu wa mkoa ndio angehusika hapo na si mkuu wa wilaya Paw makonda.
 
Hapana wakopeshwe magari.Wanafunzi kwenye daladala wanaitwa wa kusoma je walimu wataiwaje?labda teacher au wakufundisha.
watatukanwa
kudhalilishwa
kuchelewa maana watazongwa km wanafunzi
huyu makonda anaropoka tu kila analowaza bila kulifanyia utafiti mchewwwww
 
Kwani tatizo la walimu ni usafir?? Hii nchi bhna baada ya kuongeza posho na kuanda mazingira rafik eti usafir bre
 
That's why droped my teaching post past 10 years back due to this kind of misscalculations.Nimeamua kupiga debe stend tu.
 
Nnaona makonda ameshaanza kuifanyia kazi post yake mpya ya U -RC, maana anataka sahihi yake ionekane kwenye vitambulisho vya walimu wote wa Dar..
 
Mkuu wa wilaya ana nguvu kumzidi mkuu wa mkoa na raisi makonda hili kakurupuka
 
Du!!! kitambulisho tena....walimu wanastahili hadhi hii sijaipenda kabisa nikama mtu kusema njoo ule kwa brother angu bure... ukiwa mkwawa au Mirambo huwezi ipenda, the best waongezewe pesa ya usafiri kwenye mishahara yao .... bure inatweza.......kumbukeni behaviors za makonda wa daladala pia .... anyways twende tu
 
Kama watatengenzewa kitambulisho ambacho kinawekeka mfukoni au kwenye handbags sioni Kama kutakuwa na manyanyaso mana mwalim ataingia kwenye Gari bila hata kujulikana Kama ni mwalim ila wakat wa konda anadai chake ndo pale anaonyeshwa kitambulisho, pia nafkiri iwekwe sheria kali kwa konda yoyote atakae mnyanyasa mwalim.mbona hatujawah kuskia wanajeshi wananyanyasika kwenye madaladala? Hii nchi sheria zikisimamiwa vizuri kila mtu atakuwa na adabu na hata mwanafunzi anaweza kusafiri bure tuache ujinga ujinga
Hivi wanajeshi hawalipi nauli?
 
Watakuwa hawakai kwenye siti kama kama wanafunzi, ni mwendo wa kusimama tu
 
Back
Top Bottom