Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Tunashukuru kwa matusi Mungu atatulipia yani Leo hii mama yangu anipe nauli Mimi mwane alafuyeye apande bure kweli akutukanae hakuchagulii tusi
 
Mkuu Simiyu Yetu ni vema ukafikiri kabla ya kulaumu!! Niambie walimu wangap kule simiyu wananufaika na pendekezo hilo, lakini pia nauli ni kwa mwalm siyo tatizo. Malimbikizo makubwa ya madeni ya walimu, miundombinu mibovu, na mazingira magumu kwa walimu ndo matatizo sugu yanayotukabili! Me naona ingeleta mantiki kama wangeanza kutatua kero moja baada ya nyingine kuliko kumlaghai na kumdhalilisha mwalimu wa dar kwa kumlipia nauli. Kutoa huduma hii kwa magari mahsusi ya serikali kwa nchi nzima ingeleta maana kuliko hzo Porojo za mkuu wa wilaya na hao wamiliki.
 

KAMA NAWAONA WALIMU WATAVYONYANYASWA NA MAKONDAKTA WA DALADALA,
TENA BORA HATA WANAFUNZI WATATHAMINIWA KWA KUWA WANALIPA 200/=
KULIKO WALIMU WATAKAOPANDA BURE.
______
NAUONA MTITI ZAIDI PALE KONDA ANAPOONDOA GARI PALE MAWASILIANO AU MAKUMBUSHO KUELEKEA MBEZI, TEGETA, GONGO LA MBOTO
NA
MBAGALA AKIAMINI AKIAMINI KABISA KUWA BASI LIMESHAJAZA ABIRIA ZAIDI YA 40,

KUMBE WOTE NI WAALIMU!
____________
TASWIRA MPYA NAIONA PALE 97.8% YA WABONGO TUTAVYOGEUKA WAALIMU KWA KUTEMBEA NA VITABU VYA KEMIA NA CIVICS WAKATI NI WAMACHINGA TU WA PALE mtoni KWA AZIZI ALLI,

NA
IKIZINGATIWA HATUONI KAZI KUFOJI VITAMBULISHO VYA KAZI YA UALIMU ILI TUPUNGUZE MAKALI YA NAULI.
_____

INGAWA SIJAJUA KAKA'ANGU @KAKA_MAKONDA AMEANDAA STRATEGIES ZIPI,
ILA
NASUBIRI KUSHUDIA VICHWA VYA UTOSI NA MAKONZI WATAYOPIGWA NDUGU WALIMU KWENYE DALADALA.

NIMEMALIZA!
Ha ha ha mkuu bhana
 
Tanzania nchi yetu imejaa viongozi wajinga kuliko waelevu! hivi kuna utafiti umefanywa wa kisayansi kuwa walimu kusafiri bure utasaidia ufanisi wa elimu bure? walimu wanahitaji motisha katika vipato vyao kama wafanyakazi wengine.maswala ya matumizi waachiwe wao wajipangie.
 
Kama wamiliki wa magari wameridhia, Kondakta au dereva atakataa vipi?

Mmiliki yeye anataka hesabu yake tu,,namuona hapo mwenyekiti wa wamiliki wa daladala,Huyo jamaa tangu mi namiliki daladala mwaka 2000 had Leo mwenyekiti yeye tu,ivi hamnaga uchaguzi kuchagua Mwenyekiti mwingine wakuwaongoza wamiliki wa daladala
 
Ruttashobolwa said:
Hivi we Bavicha madereva wana mamlaka kuzidi Maboss wao wamiliki wa hayo magari? Hivi Bavicha mnashida gani?
Yaani wewe kila mwenye mawazo tofauti na yako ni bavicha! Sijawahi kuona mhaya hopeless kama wewe
 
Watanzania hamna shukrani...mara mia umfadhili punda atakubebea mzigo.
 
Uzalilishaji kwa walimu waongezewe maslai wapewe ela za nauli waweze kusafiri kwa Uhuru huku ni kufanya walimu waonekane ni wafanyakazi Wa chini katika jamii yeye angesema wanafunzi wasafiri bure
Yes, wakiongezewa maslahi watajisafirisha wenyewe kma wafanyakazi wengine na hii itaondoa msuguano na makondakta.
 
Bado sijaona mantiki ya huu mpango. Embu wadau husika kaeni chini na mtafakari zaidi juu ya huu mpango kwani mnaweza mkaona mtawasaidia walimu wetu kumbe ndio ikawa kinyume chake.
 
Nitaomba radhi kwa wote ambao wanaunga mkono hoja ya Makonda kuwaruhusu walimu wapande daladala Bure.

Nadhani makonda kama amesoma dar es salaam amesahau adha wanayo pata wanafunzi ambao hulipa nusu na jinsi ambavyo wanadharauliwa na makondakta wa daladala.

Kama wanafunzi wanao lipa nusu wanadharauliwa hata kushushwa watafute mabasi mengine, itakuwaje kwa walimu ambao watapanda bure.

Nauhakika kwa jinsi makondakta wanavyo kimbizana na hesabu hawata kua na muda wa kuwaheshimu walimu pamoja na elimu walizo nazo hata kupelekea walimu kuendelea kulipa nauli zao ili kukwepa adha mbalimbali kwenye daladala.

Nayaona matatizo kadha kwenye hii project.

1. Walimu kudharauliwa mbele ya abiria wengine kama kondakta kugoma kumpakia mwalimu .

2. Walimu kulazimishwa kusimama kama wanafunzi

3. Walimu kutolewa lugha chafu etc

Kama kweli Makonda ana dhamira safi ya kuwasaidia basi atafute njia nyingine .

Huu mpango unaweza kutekelezeka kwa kupitia DART na sio Daladala
 
Walimu wana hali ngumu wana mikopo kila benki bora wapande bure kama wanafunzi au watoto wa chekechea
 
Tuanzie hapa: Kwani walimu wao binafsi wanasemaje kuhusu hili? Je! Wanataka kupanda daladala bure?
 
Leo nimesikia na kuona taarifa ya habari mkuu wa wilaya ya Kinondoni akitangaza waalimu wa s/msingi na sek.kupanda vyombo vya usafiri bure bila malipo.

Huu ni udhalilishaji haiwezekani watu wanadai mishahara bora,Madai mbalimbali na mazingira mazuri halafu unawapa shukrani ya kudhalilishwa na makonda na madereva.

Mf.dereva mmoja kaulizwa akajibu kuwa waalimu wajitahidi kupanda wachache wasiwe kama askari ambao wanaweza kupanda wanne gari moja.

Lakini pia waalimu ni fadheha badala ya kuwapa mishahara bora unawaombea lift ya gari? Ili waendelee kuwanyonya.

Hata hivyo makonda na wafanyabiashara wanategemea neema kutoka kwa watumishi sasa serikali inawaombea kupanda bure hayo maslahi konda na dereva wanapataje?

Mkulima anamtegemea mfanyakazi na mfanyakazi vivyo hivyo sasa mmoja kaombewa lifti huyu ataishije?

Cwt na waalimu pingeni huu udhalilishaji.
 
Walimu msikubali kudhalilishwa namna hii! yaani muanze kuzuiwa mlangoni kama watoto wa shule?!

Ila haingii akilini..yaani wanaowafundisha wanajilipa nauli wakati wao tena walioajiriwa wanalipiwa nauli.🙂???
 
Mtoa hacha uchuro nenda Rwanda utaona kama walimu wanalipa nauli.Lakin najua wenye akili kama zako watasema hvyo
 
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda kwa kushirikiana na wamiliki wa vyombo vya usafiri Dar es salaam wametangaza kuanzisha mpango wa kuwasaidia Walimu wa Shule za Serikali kwa kuwapatia huduma za usafiri bure katika daladala.

Akieleza mbele ya waandishi wa habari Makonda amesema ‘Nilianza kuongea na vyama vya usafirishaji kisha kujenga hoja dhidi ya changamoto za Walimu wetu, na nikawaomba viongozi hao tuonane kulijadili hili na kisha tukafika muafaka

Na muafaka huo ningependa kuwatangazia Walimu na Watanzania, yakwamba sasa kuanzia tarehe 7/3/2016 Walimu wa Shule za msingi na wasekondari watasafiri bure kwenye vyombo vyetu vya usafiri kwa Mkoa wa Dar es salaam

Tumeweka utaratibu, Walimu watalazimika kutengenezewa vitambulisho maalum ambavyo kila Shule itatengeneza vitambulisho vyake, huku kukiwa na mambo manne ya kuzingatia ambayo ni 1. Picha ya Mwalimu husika, 2. Jina la shule 3.Namba ya Mkuu wake wa shule 4. Kuwe na sahihi ya Mkuu wa Wilaya Paul Makonda

source:MILLARDAYO.COM

Duuhh!!..hapo sijaelewa???
 
Back
Top Bottom