Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Walimu Dar kusafiri bure kwenye daladala

Pre paid cards ndiyo jawabu la hiyo changamoto. Ina maana sekali itagharamia kwa kutambua umhimu wa Mwalimu.
 
...hao walimu ndio watakaoanza kuchelewa shuleni badala ya wanafunzi sasa,ni bora kubeba mwanafunzi mwenye shs 200 kuliko mwalimu wa bure!!
 
Kwanini wasiwaongezee hela ya mshahara
 
Yan awa wameona matatizo ya waalimu ni kupanda daladala to ngo wakasimangwe na makonda
 
Wataanza kunyanyaswa sasa Na makondakta wa daladala.
Naona daladala nyingi pia zitaanza ruti zao baada ya muda huo wa kusafirisha walimu bure. Kwa nini wasingetafuta mabasi ambayo yangekuwa yanawasafirisha bure? Serikali iingie tu gharama ya kuyaendesha haya magari??
 
Mgema akisifiwa, tembo hulitia maji. Yangu macho na masikio - tutasikia na kuona mengi awamu hii ya 'KICK'
 
Kama watatengenzewa kitambulisho ambacho kinawekeka mfukoni au kwenye handbags sioni Kama kutakuwa na manyanyaso mana mwalim ataingia kwenye Gari bila hata kujulikana Kama ni mwalim ila wakat wa konda anadai chake ndo pale anaonyeshwa kitambulisho, pia nafkiri iwekwe sheria kali kwa konda yoyote atakae mnyanyasa mwalim.mbona hatujawah kuskia wanajeshi wananyanyasika kwenye madaladala? Hii nchi sheria zikisimamiwa vizuri kila mtu atakuwa na adabu na hata mwanafunzi anaweza kusafiri bure tuache ujinga ujinga
Serikali ikumbuke na kuwapatia mafuta wamiliki wa daladala walau 500 lts kwa mwezi hapo serikali itakuwa imewaweza makondakta wakorofi
 
Hivi kweli na hao wazee waliokaa nae hapo pembeni wanamchukuliaje huyu kijana?? Kwa kweli ni fedheha kufanya kazi na kijana mkurupukaji kama huyu
 
Okay! Ameongea na makondakta pia? madereva je? ...Wangenunua mabasi special ya walimu ingekua poa sana. Vinginevyo wanataka kuleta ugomvi!
Kama wamiliki wa magari wameridhia, Kondakta au dereva atakataa vipi?
 
Ugomvi/tatizo la walimu na serikali, hili ni janga la bara zima la afrika na baadhi ya nchi zilizo endelea lazima tulijue hilo
Hizo Nchi Ambazo Zimeendelea Zenye Hilo Tatizo Ni Zipi!!?? Au Ukiona Ama Uganda Ndio Unaelewa Bara Zima La Africa!!! Weka Evidence Zako Sio Porojo!! Humu Jf Ni Great Thinkers Mkuu!! Evidence Ndio Mtaji Wako!!
 
Je, Waalimu wenye vyombo vyao vya usafiri wamefikiriwaje kwenye mpango huu
Sawa na kusema unaenda kwenye sherehe unapewa unakaribishwa chakula we unasema umeshiba ila wakupe hela utanunua chakula ukiumwa njaa wanasaidiwa ambao wanashida ya usafiri wenye magari wao wana nafuu..basi wapaki magari wapande bure.
 
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paul Makonda kwa kushirikiana na wamiliki wa vyombo vya usafiri Dar es salaam wametangaza kuanzisha mpango wa kuwasaidia Walimu wa Shule za Serikali kwa kuwapatia huduma za usafiri bure katika daladala.

Akieleza mbele ya waandishi wa habari Makonda amesema ‘Nilianza kuongea na vyama vya usafirishaji kisha kujenga hoja dhidi ya changamoto za Walimu wetu, na nikawaomba viongozi hao tuonane kulijadili hili na kisha tukafika muafaka

Na muafaka huo ningependa kuwatangazia Walimu na Watanzania, yakwamba sasa kuanzia tarehe 7/3/2016 Walimu wa Shule za msingi na wasekondari watasafiri bure kwenye vyombo vyetu vya usafiri kwa Mkoa wa Dar es salaam

Tumeweka utaratibu, Walimu watalazimika kutengenezewa vitambulisho maalum ambavyo kila Shule itatengeneza vitambulisho vyake, huku kukiwa na mambo manne ya kuzingatia ambayo ni 1. Picha ya Mwalimu husika, 2. Jina la shule 3.Namba ya Mkuu wake wa shule 4. Kuwe na sahihi ya Mkuu wa Wilaya Paul Makonda

source:MILLARDAYO.COM
Huyu dogo akipewa huu mkoa hakika mtaona mengi msiyoyatarajia
 
haiwezekani..kwani wao ni askari.kwani swala ni nauli au swala ni foleniya dar
 
Walimu wa shule za msingi na sekondari za umma mkoani Dar es Salaam wataanza kusafiri bure kwenye daladala kuanzia tarehe 7 Machi 2016.
Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Paulo Makonda na viongozi wa vyama vya usafirishaji abiria jijini Dar wanazungumza na wanahabari hivi sasa.
Walimu wstatengenezewa vitambulisho maalum ili kuwaondolea usumbufu.
Huduma hiyo ni katika kuwapunguzia adha ya usafiri na ugumu wa maisha ikiwa ni pamoja na kuunga mkono juhudi za serikali za kutoa elimu bure.
Muda wa kuwasafirisha bure ni saa 11.30 hadi 2 asubuhi na saa 9 hadi 11 jioni.
Nawa mikoani muwape pikipiki na baiskeli kuongeza tija, bila hivyo mtakuwa mnaleta utengano kwenye kada ya ualimu.
 
Back
Top Bottom