Kama Haujui Jambo, Ni Vizuri Kuuliza Kwanza, Ndipo Uje Jukwaani!!! Kwa Taarifa Yako Kama Haujui Hili, Ila Ikiwa Mbishi Sawa!! Madereva Wa Daladala Hawana Mikataba Ya Ajira, Yaani Hawalipwi Mishahara, Posho, Hawalipiwi Bima Ya Afya(Treatments ) Hawana Likizo N.k. Kifupi Wao Ni Vibarua Tu, MATAJIRI Wanawapangia HESABU Yao Ya Siku Tu, Madereva Na Makondakta Wanapambana Kutwa Nzima Kutafuta Pesa Ya TAJIRI, Ya Mafuta Ya Kuamshia Gari Siku Inayofuata, Kiasi Ambacho Kinabakia Ndio Chakula Yao Wao!!! SASA Hao Matajiri Hata Walikubali Au Walikubaliana Na DC Makonda, Hilo Halitawaathiri Wao, Bali Wale Wanaotembeza Hayo Magari, MATAJIRI Wao Wataendelea Kupanga Hesabu Zao Tu Na Watawataka Madereva Na Makondakta Wao Wawaletee Kama Walivyokubaliana!!!! UGOMVI Utakuwa Kati Ya Madereva Na Makondakta Wa Hayo Magari, Si Matajiri Wa DC Makonda!!! Hilo Suala Ni Mtambuka, Lazima Woote Wakubali Kugawana Hiyo Gharama Ya Kuwasafirisha Hao WAALIMU Wetu Bure, Wakutane Matajiri, DC Makonda, Wawakilishi Wa Madereva / Makondakta Na Wale CWT, Wakubaliane Namna Watakavyofanya, Matajiri Wapunguze Hesabu Zao Na Mambo Mengine, Na Serikari Itoe Walau Ruzuku Kwa Wale Matajiri Walizokubaliana Nao Kufanya Hilo Zoezi, Na Magari Hayo Yawe Selected Na Kuwekewa Alama Maalum Na CWT Waelekezwe Utaratibu Wa Kufuata Ktk Zoezi Hilo, Kama Idadi Inayotakiwa Kupanda Ndani Ya Mabasi Hayo Na Utambulisho Wao Kwa Wanatembeza Hayo Magari!!! Si Suala La Kukurupuka Tu Na Kutafuta Umaarufu!!! Ni Suala Mtambuka!!