Walianza nzi kisha wakafa wote, kisha akaingia panya naye akafa pasi na kuuawa.

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
Kwema Wakuu!

Moja ya matukio ambayo mpaka leo sijayapatia majibu ni pamoja na tukio lililotokea mwaka jana katika chumba changu(kwani nimepanga chumba kimoja)
Nimeamka asubuhi nakuta kwenye mapazia nzi wametanda, ni wale nzi wakubwa wa chooni. Yaani ni wengi haswa.
Wametoka wapi sijui.

Sasa shemeji yenu kuamka, naye akakuta jambo hilo. Kama mjuavyo wanawake wanavyojishaua. Hofu, kinyaa na utatanishi vikatusonga.
Shemeji yenu akapendekeza tuwafukuze, nikamwambia achana nao. Kukawa na ubishi wa hapa na pale kwani ukipita walikuwa wanaruka ruka na kuna wakati wanagusa vyombo(si unajua tena chumba kimoja kimejaa mavyombo tele) nikamwambia achana nao.
Hiyo ilikuwa jumapili.

Kama kawaida tukawa tunaomba. Ni utaratibu wa nyumba yetu kuomba kila asubuhi na jioni. Na pia jumanne na Ijumaa ni siku ya maombi ikiwa ni pamoja na kufunga.
Basi bhana, ratiba zinaendelea. Jumatatu wakazidi zaidi. Shemeji yenu hofu ikaongezeka kuwa hiyo inasababishwa na nini na pia kuhofia ishu ya kiafya ukizingatia yeye kitaaluma ni Tabibu.

Jumanne tukaomba maombi ya maji ambayo huwa ni maombi yenye nguvu Sana. Tuliamka usiku saa saba kuelekea sàa nane. Tulipomaliza kuomba, tukamwagia yale maji pande zote cha chumba kama ilivyo kawaida. Kisha tukalala. Kesho yake tunaamka tunashangaa nzi wote wapo chini wamekufa.
Nini kimetokea hata sisi hatujui.

Alhamisi tukamuona panya akiwa anarandaranda, ni wale panya warefu alafu wembamba. Kaingiaje wakati sisi mlango hatufungui fungui.
Hatukuwaza mambo ya kishirikina au kichawi kama ilivyo kwa wale nzi. Haikuwa tishio sana.
Basi tukafanya mpango wa kununua dawa ya panya.
Cha ajabu wapitisha dawa za panya ukiwa na shida nao hawapiti mtaani kwako.
Jumamosi tunamkuta yule panya amekufa.
Nini kimemuua mpaka leo najiuliza.

Jambo moja la uhakika ni kuwa Maombi hata kama wapo wasio haamini lakini maombi yanafanya kazi.
Shahidi ni mimi mwenyewe.
Ingawaje siamini katika kuombewa hasa na mtu nisiyemjua kwa undani lakini naamini maombi ya mtu binafsi yananguvu zaidi kuliko maombi ya kuombewa.


Visa vingine kwa ajabu ajabu ninavileta hivi punde.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
kuna wakat stori ya kawaida una anza hangaika kufungua code, kuwaza makubwa kumbe ni nzi na panya wa kawaida
 
Kwema Wakuu!

Moja ya matukio ambayo mpaka leo sijayapatia majibu ni pamoja na tukio lililotokea mwaka jana katika chumba changu(kwani nimepanga chumba kimoja)
Nimeamka asubuhi nakuta kwenye mapazia nzi wametanda, ni wale nzi wakubwa wa chooni. Yaani ni wengi haswa.
Wametoka wapi sijui.

Sasa shemeji yenu kuamka, naye akakuta jambo hilo. Kama mjuavyo wanawake wanavyojishaua. Hofu, kinyaa na utatanishi vikatusonga.
Shemeji yenu akapendekeza tuwafukuze, nikamwambia achana nao. Kukawa na ubishi wa hapa na pale kwani ukipita walikuwa wanaruka ruka na kuna wakati wanagusa vyombo(si unajua tena chumba kimoja kimejaa mavyombo tele) nikamwambia achana nao.
Hiyo ilikuwa jumapili.

Kama kawaida tukawa tunaomba. Ni utaratibu wa nyumba yetu kuomba kila asubuhi na jioni. Na pia jumanne na Ijumaa ni siku ya maombi ikiwa ni pamoja na kufunga.
Basi bhana, ratiba zinaendelea. Jumatatu wakazidi zaidi. Shemeji yenu hofu ikaongezeka kuwa hiyo inasababishwa na nini na pia kuhofia ishu ya kiafya ukizingatia yeye kitaaluma ni Tabibu.

Jumanne tukaomba maombi ya maji ambayo huwa ni maombi yenye nguvu Sana. Tuliamka usiku saa saba kuelekea sàa nane. Tulipomaliza kuomba, tukamwagia yale maji pande zote cha chumba kama ilivyo kawaida. Kisha tukalala. Kesho yake tunaamka tunashangaa nzi wote wapo chini wamekufa.
Nini kimetokea hata sisi hatujui.

Alhamisi tukamuona panya akiwa anarandaranda, ni wale panya warefu alafu wembamba. Kaingiaje wakati sisi mlango hatufungui fungui.
Hatukuwaza mambo ya kishirikina au kichawi kama ilivyo kwa wale nzi. Haikuwa tishio sana.
Basi tukafanya mpango wa kununua dawa ya panya.
Cha ajabu wapitisha dawa za panya ukiwa na shida nao hawapiti mtaani kwako.
Jumamosi tunamkuta yule panya amekufa.
Nini kimemuua mpaka leo najiuliza.

Jambo moja la uhakika ni kuwa Maombi hata kama wapo wasio haamini lakini maombi yanafanya kazi.
Shahidi ni mimi mwenyewe.
Ingawaje siamini katika kuombewa hasa na mtu nisiyemjua kwa undani lakini naamini maombi ya mtu binafsi yananguvu zaidi kuliko maombi ya kuombewa.


Visa vingine kwa ajabu ajabu ninavileta hivi punde.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Mimi na hamu sana kumuona nzi kwa macho yangu (naked eyes) yani natamani sana. Wadudu wengine kila siku natamani na kuomba kuwaona ni chawa, viroboto na kunguni. Hasa kunguni jamani kumuona na kuning'ata. Nimechoka kuwaona butterfly na ladybirds.

mshamba_hachekwi
 
Mimi na hamu sana kumuona nzi kwa macho yangu (naked eyes) yani natamani sana. Wadudu wengine kila siku natamani na kuomba kuwaona ni chawa, viroboto na kunguni. Hasa kunguni jamani kumuona na kuning'ata. Nimechoka kuwaona butterfly na ladybirds.

mshamba_hachekwi

Njoo huku Tandale itawaona.
Huko kwenye kubeba boksi hizi mambo utakufa usizione
 
Kwema Wakuu!

Moja ya matukio ambayo mpaka leo sijayapatia majibu ni pamoja na tukio lililotokea mwaka jana katika chumba changu(kwani nimepanga chumba kimoja)
Nimeamka asubuhi nakuta kwenye mapazia nzi wametanda, ni wale nzi wakubwa wa chooni. Yaani ni wengi haswa.
Wametoka wapi sijui.

Sasa shemeji yenu kuamka, naye akakuta jambo hilo. Kama mjuavyo wanawake wanavyojishaua. Hofu, kinyaa na utatanishi vikatusonga.
Shemeji yenu akapendekeza tuwafukuze, nikamwambia achana nao. Kukawa na ubishi wa hapa na pale kwani ukipita walikuwa wanaruka ruka na kuna wakati wanagusa vyombo(si unajua tena chumba kimoja kimejaa mavyombo tele) nikamwambia achana nao.
Hiyo ilikuwa jumapili.

Kama kawaida tukawa tunaomba. Ni utaratibu wa nyumba yetu kuomba kila asubuhi na jioni. Na pia jumanne na Ijumaa ni siku ya maombi ikiwa ni pamoja na kufunga.
Basi bhana, ratiba zinaendelea. Jumatatu wakazidi zaidi. Shemeji yenu hofu ikaongezeka kuwa hiyo inasababishwa na nini na pia kuhofia ishu ya kiafya ukizingatia yeye kitaaluma ni Tabibu.

Jumanne tukaomba maombi ya maji ambayo huwa ni maombi yenye nguvu Sana. Tuliamka usiku saa saba kuelekea sàa nane. Tulipomaliza kuomba, tukamwagia yale maji pande zote cha chumba kama ilivyo kawaida. Kisha tukalala. Kesho yake tunaamka tunashangaa nzi wote wapo chini wamekufa.
Nini kimetokea hata sisi hatujui.

Alhamisi tukamuona panya akiwa anarandaranda, ni wale panya warefu alafu wembamba. Kaingiaje wakati sisi mlango hatufungui fungui.
Hatukuwaza mambo ya kishirikina au kichawi kama ilivyo kwa wale nzi. Haikuwa tishio sana.
Basi tukafanya mpango wa kununua dawa ya panya.
Cha ajabu wapitisha dawa za panya ukiwa na shida nao hawapiti mtaani kwako.
Jumamosi tunamkuta yule panya amekufa.
Nini kimemuua mpaka leo najiuliza.

Jambo moja la uhakika ni kuwa Maombi hata kama wapo wasio haamini lakini maombi yanafanya kazi.
Shahidi ni mimi mwenyewe.
Ingawaje siamini katika kuombewa hasa na mtu nisiyemjua kwa undani lakini naamini maombi ya mtu binafsi yananguvu zaidi kuliko maombi ya kuombewa.


Visa vingine kwa ajabu ajabu ninavileta hivi punde.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
kuna watu watabisha lakini nina imani na maombi mkuu

ila kujiombea ndio dili

hata Yesu alisema tujiombee wenyewe tukiwa na imani pasina shaka tutapata lakini mambo ya kuombewa na watu wengine hapana kwa kweli.
 
Oyaaa mtibeli naungana na ww maombi yana nafasi yake!

😄Naona umeanza pigo za wale wamama wa kwenye Eicher za mbagala kawe

Vuka na chako📈📈📈📈😂
 
kuna jamaa yangu hapa ofisini kanipa kisa eti jirani yake nyumba ya kupanga msimuu wa sikuku alikua akichinja kuku dirishani kwakwe

ikumbukwe jamaa anamtoto mchanga na mzazi ndani
 
Back
Top Bottom