Wale wa BITCOIN wameshatapeliwa

Wale wa BITCOIN wameshatapeliwa

BABA TUPAC

JF-Expert Member
Joined
Sep 30, 2015
Posts
1,533
Reaction score
3,837
Wakuu,

Jamaa wa Bitcoin walikuwa wakijitapa sana kuwa wamekuwa matajiri, yale leo wamepokea taarifa mbaya ambayo hawajawahi kuipata.

Mwanzilishi wa Bitcoin Bw. Quadriga CX amefariki dunia na wanasema yeye ndio alikuwa na password ya kuingia kwenye hiyo account iliyokuwa na dollar milioni mia mbili ambayo ni sawa na bilioni mia mbili hamsini.

Hivyo watu wengi duniani wakiwepo watanzania wenzetu wamepigwa pesa zao. Namaliza kwa kusema kuwa ''UKIITWA KWENYE FURSA BASI UJUE WEWE NDIO FURSA''
 
"Usichokijua ni sawa na usiku wa Giza" mleta mada umejaribu kuelezea kitu ambacho hukijui hata robo. Yule zile zilikuwa hela zake yeye na sio eti hela zote za Bitcoin. Haina tofauti na mtu akafa na password za M-Pesa yake hii itamaanisha ni zile peza zake pekee ndio zitakuwa zimepotea na sio pesa zote za Tanzania zilizoko kwenye mzunguko wa M-Pesa. Huyo jamaa amekufa na mabilion yake bila kumpa mtu password yake na kwenye Bitcoin hakuna central place ya kufanya retrieval ya hiyo password, hivyo ni pesa zake tu ndio zimepotea kwa kuwa hakuna namna ya kuzirudisha na sio pesa zote za Bitcoin.
Mimi bado natumia Bitcoin kwenye kudeposit hela kwenye account yangu ya skrill very swiftly and conveniently.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Jamaa wa Bitcoin walikuwa wakijitapa sana kuwa wamekuwa matajiri, yale leo wamepokea taarifa mbaya ambayo hawajawahi kuipata.

Mwanzilishi wa Bitcoin Bw. Quadriga CX amefariki dunia na wanasema yeye ndio alikuwa na password ya kuingia kwenye hiyo account iliyokuwa na dollar milioni mia mbili ambayo ni sawa na bilioni mia mbili hamsini.

Hivyo watu wengi duniani wakiwepo watanzania wenzetu wamepigwa pesa zao. Namaliza kwa kusema kuwa ''UKIITWA KWENYE FURSA BASI UJUE WEWE NDIO FURSA''

Dah nilishafanywa fursa na kitu inaitwa D9.

Awali nilikataa kuwa hakuna kuwin maisha kiurahiurahisi tu, ilasijui nilibadilishwa vipi akili.

Kweli "ukiitwa kwenye fursa basi juu wewe ndio fursa yenyewe" yaani unafanywa ngazi ya watu kufikia malengo.

INGAWA Bitcoin ni ngumu kudondoka, na kwa sasa ni sarafu kubwa...haiwezekani iwe mtu mmoja ndio awe na password.
 
Watanzania tusome tuache uvivu . Huyu bwana hajui hata nini ni bitcoin kaja kukimbilia habari ya watu. Huyo sio mwanzilishi wa BITCOIN (mwanzilishi/waanzilishi wake hawafahamiki hadi Leo)
Na huyo kafa na password ya account iliyokua na bitcoin za watu

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wakuu,

Jamaa wa Bitcoin walikuwa wakijitapa sana kuwa wamekuwa matajiri, yale leo wamepokea taarifa mbaya ambayo hawajawahi kuipata.

Mwanzilishi wa Bitcoin Bw. Quadriga CX amefariki dunia na wanasema yeye ndio alikuwa na password ya kuingia kwenye hiyo account iliyokuwa na dollar milioni mia mbili ambayo ni sawa na bilioni mia mbili hamsini.

Hivyo watu wengi duniani wakiwepo watanzania wenzetu wamepigwa pesa zao. Namaliza kwa kusema kuwa ''UKIITWA KWENYE FURSA BASI UJUE WEWE NDIO FURSA''

Tuwekane sawa hapa

Mwanzilishi wa bitcoin ni mtu ambaye alijulikana kama Satoshi Nakamoto , pia haijawahi kufahamika huyu mtu ni nani na yupo wapi

Bitcoin haimilikiwi na mtu yoyote, mfano pesa ya tanzania inamilikiwa na serikali lakini bitcoin haimilikiwi na mtu wala taasisi

Bitcoin haisimamiwi na taasisi yoyote wala mtu na itaendele kuwepo hivyo

Mtoa mada fanya utafiti kabla ya kutoa thread
 
Ngoja niende zangu kuweka mkeka tu, hapa michosho tu
 
Mtu hata akifa, kuna namna ya kuover ride system kwa kibali maalum cha mahakama na wahusika (warithi) kupatiwa pesa za muhusika.
 
Kwanza niseme kwamba nimekuquote sababu naamini hauna mihemko na ni mtu mwenye open mind.

Naomba ujaribu kugoogle ni nani mwanzilishi wa bitcoin, then ulinganishe utakachokiona na hii habari iliyoletwa hapa!

Wasalaam.

- KANA -
Asante sana... Nimejikuta najiona mpumbavu, sikuwa makini kwenye kuchangia.... Isingewezekana kitu kikubwa kama hicho taarifa zake za siri awe nazo mtu mmoja tuu...
Kuna lose ends nyingi zinazohitaji clarification


Jr
 
Mtu hata akifa, kuna namna ya kuover ride system kwa kibali maalum cha mahakama na wahusika (warithi) kupatiwa pesa za muhusika.
Kwa bitcoin ukipoteza passphrase(kama password) basi bitcoin zako zimepotea na hamna namna yoyote ya kuzirudisha na haitokuja kutokea kuzirudsha
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom