Wakuu hivi kuna tofauti gani kati ya GDP na budget ya serikali?

Bajeti ya serikali huwa ni andiko linaloonesha mapato na matumizi ya serikali. GDP ni pato ghafi la taifa. Linahusisha matumizi ya serikali, watu binafsi, uwekezaji na mizania ya biashara (hasa tofauti ya thamani ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi na zile zinazoagizwa kutoka mataifa ya kigeni). Kwa kifupi GDP ni pana kuliko bajeti ya serikali, japokuwa vina uhusiano kwa vile matumizi ya serikali ni sehemu ya GDP.
 
Bajeti Ya Serikali
= Makadirio ya mapato na matumizi ya serikali/nchi

Gross Domestic Product (GDP)
= kwa kifupi ni pato la taifa ama thamani ya uzalishaji katika nchi
 
kwa lugha rahisi kabisa, GDP ni thamani ya uchumi wa nchi ambazo huwekwa ktk pesa ni kama vile mtaani tu tunasema mwenye pesa zaidi ndo ana gdp kubwa (tunaeza sema mwenye v8 ana gdp kubwa kuliko mwenye ist, mwenye gdp kubwa ndio mwenye mkwanja mrefu, lakini unaweza kua na mkwanja mrefu lakini ukawa unaishi vibaya na ndugu zako wakawa bado masiki, yaani una pesa ila hazikusaidii=nigeria, pia unaweza kua na mkwanja wa wastani tu lakini ukala bata kuliko mwenye hela zaidi yako na ndugu zako ukawasaidia vizuri na wakaenjoy maisha na kua na furaha kulkiko ndugu wa yule tajiri zaidi=south africa) ,

bajeti ya serikali ni sawasawa na bajeti yako unayojipangia kila siku mwezi huu au siku ya leo nitatumia kiasi flani cha pesa kununua hiki hiki na hiki vitanitunza mpaka siku flani ntapopanga bajet nyingine , tofauti ni kwamba ni moja ni ya serikali na nyingine ni yako!
 
🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾🙌🏾👍🏽

Bajeti ya serikali huwa ni andiko linaloonesha mapato na matumizi ya serikali. GDP ni pato ghafi la taifa. Linahusisha matumizi ya serikali, watu binafsi, uwekezaji na mizania ya biashara (hasa tofauti ya thamani ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi na zile zinazoagizwa kutoka mataifa ya kigeni). Kwa kifupi GDP ni pana kuliko bajeti ya serikali, japokuwa vina uhusiano kwa vile matumizi ya serikali ni sehemu ya GDP.
 
Bajeti ya serikali huwa ni andiko linaloonesha mapato na matumizi ya serikali. GDP ni pato ghafi la taifa. Linahusisha matumizi ya serikali, watu binafsi, uwekezaji na mizania ya biashara (hasa tofauti ya thamani ya bidhaa zinazouzwa nje ya nchi na zile zinazoagizwa kutoka mataifa ya kigeni). Kwa kifupi GDP ni pana kuliko bajeti ya serikali, japokuwa vina uhusiano kwa vile matumizi ya serikali ni sehemu ya GDP.
Kuongezea GDP ni pato ghafi la ndani, na Bajeti ni mchangako wa Pato la ndani na nje, misada, mikopo na ruzuku.
 
Back
Top Bottom