Wakristo tunashambuliwa, tujitetee!

Wakristo tunashambuliwa, tujitetee!

Wakristo tunashambuliwa, tujitetee!
  • Gwajima
  • Kitima
Nahisi sio sawa kusema Wakristo, kwani kila mtu bila kujalisha dini yake anaweza kupatwa na lolote, na isitoshe walionyuma ya yote hayo ni wakristo,.Kikubwa ni kusema watanzania kwa pamoja, kwani kuanza kutetea mtu kwa kujinasibisha na dini ni mbaya zaidi. Tuache mambo ya udini bali tupange mambo ya kitaifa kama watanzania bila kuweka udini. Kuna watu wanapambani haki kama akina sheh Ponda, ivyo ukisema wakristo ilihali yeye sio mkristo lakini anasakamwa unakuwa ujabalance taarifa.

NK: Utanzania kwanza mengine baadaye. Tukisema ukristo, basi ujue viongozi wote wakiwa wakristo litakuja swala la ni dhehebu gani( ili nalo lipo kimya kimya wanaojua mambo watanielewa), baada ya hapo litakuja la kwanini kabila flani ni wengi sehemu flani. Mwisho wa siku utakuwa ugomvi wa maisha.

Kikubwa tujadili mambo ya kuunganisha watanzania wote bila kujali dini ili tuwe na Taifa liliobola.
 
Tuamke watanzania tuwe wakali, huu upole na kutochukua hatua ni upumbavu. Wale tunao wamudu tumalizane nao tusimwachie Mungu, wakati wa ukombozi ni sasa.
Niliandika humu siku Moja kwamba kati ya watu wajinga Duniani ni watanganyika.
Walio mpa KESI ya UHAINI Lissu ni watanganyika

Walio saidia Bandari za Tanganyika ziuzwe ni watanganyika.

Walio ratibu wa kumuua Padre Dr Kitima ni watanganyika.
Walio panga mipango ya kuua na kuteka ni watanganyika.

Wanao saidia mambo yote haya mabovu ni WATANGANYIKA.
 
makamu alijua huu upuuzi akajiweka pembeni naona wanamzonga tu angeshakaa pembeni
 
Wakristo watazidi kuonewa Sana TANZANIA kutokana viongozi wenyewe kujiona ni wasomi sana..
Ingekuwa msikiti umefungwa Leo akina mwaipopo na wenzake wangekuwa mtaani kupinga na haitakuja kutokea msikiti kufungiwa Tanzania
Ila kuna mashekhe waliyokwa gerezani kwa miaka kumi bilq ya hukumu
Kuna mashekhe waliopigwa risasi misikitini
Na yote hayo hatujasikia waislamu au misikitini kukienezwa chuki au kuhutubiwa siasa hiyo ndio tofauti , kinachokusumbua wewe ni udini na lack of exposure, hapo rwanda tu makanisa zaidi ya 100 yamefungwa , ukitaka kuharibu amani ya nchi na kwenda tofauti na leseni yako utafungiwa tu bila ya kuangalia sura
 
Ila kuna mashekhe waliyokwa gerezani kwa miaka kumi bilq ya hukumu
Kuna mashekhe waliopigwa risasi misikitini
Na yote hayo hatujasikia waislamu au misikitini kukienezwa chuki au kuhutubiwa siasa hiyo ndio tofauti , kinachokusumbua wewe ni udini na lack of exposure, hapo rwanda tu makanisa zaidi ya 100 yamefungwa , ukitaka kuharibu amani ya nchi na kwenda tofauti na leseni yako utafungiwa tu bila ya kuangalia sura
Bado umekimbia hoja ya kufunga kanisa, Mimi naongelea ufunguji wa kanisa hii haijawahi kutokea Tanzania.
Wenye Akili hawana muda wa kijadili dini Sisi tunaangalia kufunga kanisa
 
Wakristo wa dhehebu gani wanaoshanbuliwa?

Au Gwajimanize?
 
Bado umekimbia hoja ya kufunga kanisa, Mimi naongelea ufunguji wa kanisa hii haijawahi kutokea Tanzania.
Wenye Akili hawana muda wa kijadili dini Sisi tunaangalia kufunga kanisa
Kama likikiuka taratibu litafungwa tu hakuna namna , yani tusifuate sheria kwakuwa haikuwahi kutekelezwa? Kila kitu kina mara yake ya kwanza , hakuna uhuru usiokuwa na mipaka ,pamoja naunga mkono reforms ila siungi mkono huu upuuzi wa gwajima, yani uharibu amani ya nchi kisa maslahi yako binafsi , lifungwe tu hilo kanisa
 
Kama likikiuka taratibu litafungwa tu hakuna namna , yani tusifuate sheria kwakuwa haikuwahi kutekelezwa? Kila kitu kina mara yake ya kwanza , hakuna uhuru usiokuwa na mipaka ,pamoja naunga mkono reforms ila siungi mkono huu upuuzi wa gwajima, yani uharibu amani ya nchi kisa maslahi yako binafsi , lifungwe tu hilo kanisa
Kama amehatarisha amani akamatwe yeye tena ushahidi mnao juu ya uvunjifu wa Amani sasa kanisa Lina kosa gani ? Kipindi cha vurugu za mwembechai pale magomeni ule msikiti uliendelea kutumika japokuwa viongozi wao walikamatwa.

Umewahi kuona wapi kosa ufanye wewe alafu wafungwe ukoo wako wote?
 
Kama amehatarisha amani akamatwe yeye tena ushahidi mnao juu ya uvunjifu wa Amani sasa kanisa Lina kosa gani ? Kipindi cha vurugu za mwembechai pale magomeni ule msikiti uliendelea kutumika japokuwa viongozi wao walikamatwa.

Umewahi kuona wapi kosa ufanye wewe alafu wafungwe ukoo wako wote?
Inavyoonyesha hujui hata sheria, hujui kama ukikiuka dhumuni la leseni yako hiyo ofisi yako inafungwa? Kama hujui jambo dogo kama hilo basi ungerudi tu shule
 
Ongeza na shekhe ponga kupigwa risasi Kisha ondoa neno wakristu,Tuache uchochezi wa kidini.
to me iko hivyo!
shekhe ponga ni nani? alipigwa risasi ka sababu gani?
 
Back
Top Bottom