Wakili Mwabukusi ni Mchanganyiko wa Mdude + Lissu. Je Alikuwa Wapi Wakati wa Hayati Magufuli?

Huihui2

JF-Expert Member
Jan 5, 2012
5,277
8,003
Ni wazi hakuna ubishi Man of The Moment (MOTM) kwa sasa ni Wakili Boniface Mwabukusi kutokana na namna alivyolibeba suala la Bandari/DP WORLD kwa mabega mawili. Wanasiasa na Wanaharakati wengi wameongea kama kina Lissu, Mbowe, Slaa, Tibaijuka, Shivji, Binti Sarungi, Madeleka na Nshala.

Lakini ni Wakili Boniphace Mwabukusi ndiyo maneno yake na haiba yake yana mvuto kuliko mtu yeyote. Mwabukusi ana uwezo wa kuwasilisha mada kwenye hadhara kama Wahubiri wa Kilokole akina Mwamposa/ Gwajima, ana maneno makali kama Mdude na ana uwezo kuchambua sheria kama Lissu.

Swali:
Je, huyu Bwana alikuwa wapi wakati wa Dikteta Magufuli 2015-21? Alipobana kabisa uhuru wa maoni na kukanyaga katiba

Je, kwa huu ubingwa wake, nini ingekuwa hatma yake kipindi cha Magufuli?
 
Mipango ya Mungu ni tofauti na yawanadamu maisha yetu tunayoishi tunayoishi tukipata shida wanaokuja kuwa msaada ni watu usio wategemea

Mungu huwa anainua watu ambao anaona yeye akiwapa jukumu akilibeba ataliweza na atakuwa msaada kwa watu wengi turudi kwenye kitabu kitakatifu biblia utaona ni namna gani kila kitabu kilikuja na nabii wake
 
Rasilimali za Tanganyika zimetolewa bure kwa mwarabu milele, hii ndio sababu inayomfanya Adv. Mwabukusi na wengine kina Dr. Nshalla kujitokeza hadharani kupinga uovu huu usiokuwa na kifani kwa mtanganyika.

Sasa ukiuliza alikuwa wapi wakati wa Magufuli, ikiwa umeshasema Mwabukusi ndie man of the moment, hapo naona umeshapata jibu la swali lako, muda wake ndio sasa kama ulivyoandika.
 
Back
Top Bottom