Wakenya, Waganda na Warundi Serikalini

Wakenya, Waganda na Warundi Serikalini

Hivi kwa mfano sasa hivi ukiulizwa wewe ni Mtanzania utaleta uthibitisho gani wenzetu Kenya wana vitambulisho tangu zamani.
 
naiman64 I agree, hata kwetu Kenya tunapitia hizo changamoto.....lakini msiseme waTz mwadharauliwa kwa hilo, ukija Nairobi vilabu vingi ni miziki ya kibongo na watu wanapenda. Hutosikia hata mkenya mmoja akisema hii miziki ya Tz inaharibu soko la miziki ya kikwetu
 
Shida ya waTz wengi ni chuki na wivu, kulaumu majirani wenu kwa masaibu yenu
Tizama ndugu, Tanzania haitaweza kuendelea hata siku moja sababu haina control na raia wake. Sasa unapopanga maendeleo unakisia una watu millioni arobaini kumbe idadi ni milioni hamsini ndani yake kuna Warundi, Wanyarwanda, Wakongo, wamalawi, Waganda, Wamakonde kibao, kila leo wanahamia nchini kwa kisingizio cha wakimbizi, siku zote budget itakuwa deficit. Mimi nafundisha chuo kikuu kimoja hapa Tanzania, juzi tulikuwa na kesi za wanafunzi kwenye disciplinary committee, huwezi kuamini tuligundua kwamba pale chuoni kuna wanafunzi kibao kutoka Burundi na Kenya wana mikopo kutoka loan board ya Tanzania yaani wanapewa mikopo wakijulikana ni Watanzania.Baada ya kuwahoji wakasema sio wao tu ila wapo wengi tu hapo chuoni na vyuo vingine. Wanachofanya Wakenya wanawaleta watoto wao kusoma hapa Tz Primary school basi wataendelea mpaka chuo kikuu, vyuo vya ualimu na vyuo vya Udaktari na Unesi wakijulikana Watanzania. Na hii elimu bure tutalia sana tu.
 
naiman64 I agree, hata kwetu Kenya tunapitia hizo changamoto.....lakini msiseme waTz mwadharauliwa kwa hilo, ukija Nairobi vilabu vingi ni miziki ya kibongo na watu wanapenda. Hutosikia hata mkenya mmoja akisema hii miziki ya Tz inaharibu soko la miziki ya kikwetu
Umechanganya habari mazee
 
Wa mabere sisi waKenya tumekuwa na wakimbizi wa Somalia miaka mingi...hivi sasa wako kwa top 5 most populous ethnic community in Kenya na kumbuka bado tuna tishio la al shabab...wako Eastleigh ambapo wana mabiashara makubwa makubwa but hutowahi sikia wakenya tukisema wafukuzwe coz si wakenya. Kumbuka wengi ni wakimbizi lakini polepole wameanza kutangamana na jamii
 
Kwa jinsi ulivyoandika inaokekana unaandika kichuki chuki tu na ukiambiwa wataje au waonyeshe sidhani utaweza, ijapokuwa inawezekana kweli wapo, kila mwananchi anatakiwa awe na uchungu na nchi yake na kuilinda, kama kweli umefanya utafiti na unauhakika na unayoyasema na unajua athari za watu kama hao, kwanini usiende kutoa taarifa idara zinazohusika na uwape ushahidi wako.
mbona ameandika kwamba amewaripoti wengi....vipi amekugusa pabaya
 
By Hute
''.....hapa juzi, Arusha walionekana wakenya na waganda wakiandikisha watoto wao kwenye vizazi na vifo.
...''
Mkuu, zoezi hilo ni muhimu sana hata nje ya nchi watanzania wakizaliwa pia huandikishwa ofisi ya vizazi na vifo.

Ila ofisi ya vizazi na vifo wawe makini wakati wa kutoa vyeti hivyo kwa kuweka taarifa sahihi za mtoto na wazazi wake.

Pia Ofisi za Vizazi na Vifo ndiyo chimbuko la data kwa ajili ya Ofisi za Takwimu, Uhamiaji n.k suala ni kuwa zoezi la kuandikisha watoto Vizazi na Vifo lifanywe kwa umakini.
 
WAKUU, katika utafiti wangu nimegundua kuna raia wa kenya wengi sana wameajiriwa katika public service, waganda pia wapo wengi, warundi na wanyarwanda wapo wengi sana. binafsi kufanya kazi katika private sector najua kuna sheria inayowaruhusu kama wakitimiza vigezo, lakini imefika kipindi wanaajiriwa serikalini wakiwa wamefoji vyeti vya kuzaliwa na passport na kujifanya watanzania. usalama wa nchi upo wapi hapo? mtu akifanya kazi serikalini na yeye sio mtanzania anaweza kupeleka siri zote nchini kwake, na akibadilisha vyeti, ndi kabisaa, watoto wake watahesabika watanzania hata bila kuwa naturalized, naiomba serikali ifanye hivi:

  1. serikali ikague vyeti vyote vya wafanyakazi serikalini, kuanzia vyeti vya kuzaliwa, vyeti vya shule na vyuo, passport etc na wafanye check up na RITA, uhamiaji na shule wanazosema wamesoma etc.
  2. wananchi wa Tanzania watoe siri, ukiona unamtilia shaka raia yeyote anayefanya kazi kwenye public sector, peleka siri hiyo uhamiaji ili uahmiaji waje wamkague kujiridhisha.
  3. wengine wengi ni wanawake walioolewa na watz lakini bado hawajachukua uraia.
hapa juzi, Arusha walionekana wakenya na waganda wakiandikisha watoto wao kwenye vizazi na vifo.

kuna wafanyakazi wengi tu mimi nimeshawaripoti, wengine wanafanya kazi sector muhimu kabisa za serikali, wamefoji vyeti vya kuzaliwa, passport, na vya shule ili waonekane walizaliwa hapa na kusoma hapa, lakini nyuma ya pazia wana vyeti na pass za nchi zao. ni lazima tushirikiane kufichua suala hili.

nchi inayokaa na wageni wa namna hii ni hatari sana kwa usalama wa nchi, no wonder hata kagame alikuwa na guts za kututishia kuwa atatupiga, kwasababu kuna wanyarwanda wengi wanaojifanya watanzania na wengine hata ukiwaangalia kwa sura tu hauulizi mara mbili. siwabagui lakini usalama wa nchi kwanza, uafrica mashariki baadaye. mtaniwia radhi. wakenya ndio wengi sana, mrundi mmuja nakumbuka alikamatwa anafanya kazi tume ya sayansi na technolojia, mwignine alikamatwa mkenya akifanya kazi tanzania investment centre, mwingine alikamatwa mganda akifanya kazi uhamiaji, kuna wengi sana hawajakamatwa lakini usalama wa taifa sijajua kama wamefanya shughuli yao vya kutosha. MUNGU IBARIKI TANZANIA.

Acha kulalamika humu JF, peleka majina hayo kwenye vyombo vya dola. Peleka TISS. Kila wilaya ina ofisi za TISS. Peleka majina hayo kwa DSO au hata RSO yaani yule wa mkoa. Uwe na ushahidi usipeleke majungu. Ukifanya hivyo hoja yako itafanyiwa kazi, tena mara moja.
 
Wewe nilikujua ni mkenya pale kwenye post yako ya kwanza tu, ulijitambulisha vizuri sana

Ujuaji Ujinga ndiyo huu uliouonyesha.
Big up Mkenya
Chuki peleka huko===================================>> meffi ya mbwa ww
 
Back
Top Bottom