Sijaribu kujustify chochote bali nimeuliza, Mtanzania ni nani? Unatumia kigezo gani kusema huyu ni Mtanzania, yule siyo? Kama ni cha kuzaliwa Je, Mmasai ni nani? Kwa maana amezaliwa kwenye Manyata huko hana karatasi yoyote ile ya kusajiliwa mahali, leo yuko Kenya kesho yuko Tanzania, sasa huyu unamuitaje? Yaani kigezo cha Utanzania ni kipi?
Bado naamini unajaribu ku-justify jambo kwa sababu swali lako hapa sio pahala pake!!! Sio pahala pake kwa sababu mada haihusiani na Mtanzania wala Watanzania bali Wakenya na pasi za kusafiria za Kitanzania!!!
Anzia hapo!!!
Lakini kukujibu swali lako, kwa mujibu wa Sheria ya Uraia ya Tanzania ya Mwaka 1995 Sura ya 357 pamoja na kanuni zake za mwaka 1997, kuna uraia wa aina tatu: Uraia wa Kuzaliwa, wa Kurithi na Kujiandikisha.
Kama mtu alizaliwa kabla ya uhuru wa Tanganyika na mzazi wake mmoja alizaliwa Tanganyika na mzazi huyu alitokana na ama raia wa Uingereza, makoloni yake au nchi zilizokuwa British Protectorates, basi mtu huyo alihesabika raia wa wa kuzaliwa wa Tanganyika.
Aidha, mtu aliyezaliwa Tanganyika baada ya uhuru nae alitambulika raia wa Tanganyika wa kuzaliwa provided mmoja wa wazazi wake alikuwa Mtanganyika!
Vile vile, mtu aliyezaliwa Zanzibar kabla na baada ya mapinduzi alitambulika ni raia wa Zanzibar wa kuzaliwa provided wazazi wake hawakutokana na wale wakoloni waliokuja Afrika except German & UK! Vile vile wazazi wao hawakutokana na US, Canada, Ireland, South Africa, Sri Lanka na Australia.
Raia hao wa Tanganyika na Zanzibar ( wa kuzaliwa) hapo juu automatically walikuja kuwa raia wa Tanzania baada ya muungano wa Tanganyika na Zanzibar.
Likewise, mtu aliyezaliwa siku ya na baada ya muungano huyu alitambulika kama raia wa Tanzania provided mmoja wa wazazi ni raia wa Tanzania!
Tafuta mwenyewe sheria niliyotaja hapo juu ili ufahamu ni kwa namna gani mtu anatambuliwa kama Raia wa Tanzania wa kurithi na kuandikishwa...
Hivyo basi, huyo Mmasai hata kama amezaliwa Manyata kama ulivyosema na kesho yupo Kenya na mtondogoo Tanzania bado anaweza kuhesabika ni Mtanzania provided anakidhi vigezo hivyo hapo hapo juu (uraia wa kuzaliwa) au ni raia wa kurithi au kuandikishwa!
Haya, rudi kwenye mada sasa; hususani hati za kusafiria kutolewa mgahawani hali inayoibua shaka kwamba inawezekana kabisa hao watu hawana haki KISHERIA kupata hati za kusafiria za Tanzania!!!