Wakenya na Passpoti za Tanzania

Wakenya na Passpoti za Tanzania

Je unajua kwamba sehemu kubwa ya watu waishio Tanzania waliozaliwa na kukulia hapa hawana Cheti cha kuzaliwa? Sasa unathibitisha vipi Utanzania wao? Vipi kuhusu Wamasai ambao hawana karatasi yoyote ile? Je ni Watanzania au Wakenya?
Kila mtanzania anajua historia ya mtanzania mwengine,wanajua babu,bibi au mama kazaliwa wapi, kabila gani nk,kuhusu wasai tangu hapo mwanzo serikali za Kenya na Tanzania walikubaliana kwa hawa watu hawana nchi maalumu,hawana passpoti...

Turudishie passport yetu,mkuu
 
Lkini haujajibu swali, Mtanzani ni yupi? Ni nini maana ya Utanzania?
hilo la Utanzania ungelianzishia mada. alieyeleta mada alitaka tujue kuna watu wananunua pas za Tz vijiweni pengine hawakustahili..pia wanaowauzia kinyume na utaratibu
 
hilo la Utanzania ungelianzishia mada. alieyeleta mada alitaka tujue kuna watu wananunua pas za Tz vijiweni pengine hawakustahili..pia wanaowauzia kinyume na utaratibu


Kama hata maana ya Utanzania hatuijui, hakuna haja hata ya kujadili mambo ya kuwa na Hati ya kusafiria, ilipaswa tuanzie hapo kwanza kwenye kutoa maana ya Utanzania!
 
Kama hata maana ya Utanzania hatuijui, hakuna haja hata ya kujadili mambo ya kuwa na Hati ya kusafiria, ilipaswa tuanzie hapo kwanza kwenye kutoa maana ya Utanzania!
kuna mtu ameshapost huku nyuma.. pia sio maana ya mleta mada, ebo! unaanzisha mada juu ya mada
 
Wanajamvi
Hili suala linatisha. Mimi ni member wa sehemu moja maarufu hapa Jijini. Ni sehemu ya Kula. Mnamo tarehe 31 May 2017 jioni, nilikaa meza Jirani na wakenya kama watano hivi wanaume wanne na mwanamke mmoja. Mara baada ya dakika kadhaa, alikuja jamaa mmoja aliyejumuika nao. Takriban dakika 30 baadae Yule jamaa kufika, alitoa rundo la Pasi ZA kusafiria ZA kitanzania ambazo hawa wakenya waligawiwa. Bila kupoteza muda, wakenya walitoa mfuko mweusi wa plastiki na kumkabidhi hawa jamaa na ghafla kuondoka. Nilitamani kujua kwamba zile pasi mpya zilikuwa za nini?

Sikufanikiwa ila, nilifanikiwa kuongea na mmoja wa hawa wakenya, ambaye pamoja na lafudhi yake aliniambia yeye ni mchaga wa Tarakea. Hawa Jirani zetu wananunua ardhi kwa kasi ya kutisha kutumia vitambulisho vya kitanzania. Wanajiita watanzania. Wanyarwanda pia hivyo hivyo. Ofisini kwetu kuna mdada mnyarwanda pia mwenye Pasi ya Tanzania anajiita muangaza. Nadhani kuna tishio kubwa mbeleni utakaotokana na watu kujizolea hizi passport za kutanzania
Hao ni watanzania tu. Nini kinakusababisha useme siyo watanzania?
 
Tanzania kuna wanyamwezi hao unaosema wanajiita wanyamwezi ni wahamiaji haramu wenzako.


Unajua Historia ya wanaojiita Wanyamwezi? Ngoja nikusaidie kidogo, mwanzoni kulikuwa hakuna kundi la Wanyamwezi bali watu waishio Unyanyembe (Tabora) walibatizwa jina hilo wkt wa Biashara ya Utumwa, ambapo karavani lilikuwa linatokea Kigoma kupitia Unyanyembe (Tabora) mpaka Dar- Bagamoyo, Tanga- Zanzibar, sasa wale Wafanyabiashara wa ktk Pwani (Bagamoyo, Zanzibar na Tanga) ambao walikuwa wanakwenda kukununua Watumwa huko Unyanyembe waliwapenda watu wa eneo hilo kwa sababu walikuwa ni hodari wa kufanya kazi yaani walihilimi kubeba mizigo mizito kama Pembe za ndovu hivyo wakawaita ,,Watu kutoka Mwezini", na hivyo basi ilikuwa ili uweze kupata kazi ya kubeba mizigo ni lazima uwe unatoka hili eneo na ndipo wengi wakaanza kujiita Wanyamwezi ili wapate kazi ya kubeba mizigo ktk Bara mpka Pwani, na ndipo Unyamwezi ulipozaliwa!!

Na ndiyo maana kama ukienda Zanzibar mpaka leo hii kuna Wahamiaji wanaitwa Wanyamwezi, hata msemo wa ,,Mzigo mzito mpe Mnyamwezi abebe", umetokana na hii Historia, hivyo ndiyo maana nasema wanajiita Wanyamwezi kwa maana ni jina waliliopewa na Wamiliki Watumwa akina Tip Tipu &Co., kabla ya hiyo Biashara walikuwa hawaitwi Wanyamwezi, bali hilo eneo liliitwa Unyanyembe Tabora ya leo na sehemu kubwa yao wametokea Unyarwanda na Baganda (Uganda ya leo)
 
kuna mtu ameshapost huku nyuma.. pia sio maana ya mleta mada, ebo! unaanzisha mada juu ya mada


Mada haiwezi kubakia kama ilivyo ni lazima itabadilika kulingana na wingi wa uchangiaji unavyoongezeka hilo ni kawaida!
 
Mtanzania ni nani? Tuanzie hapo kwanza, usisahahu hii Nchi tunayoiita Tanzania ina miaka 55 tu, hivyo ina maana mtu yoyote aliyezaliwa kabla ya hapo, Uraia wake una utata, na hii inaweza kukugusa hata wewe au ndugu zako wa karibu!
Huko lumumba kuna mijitu kibao uraia wao una utata

Ova
 
Huko lumumba kuna mijitu kibao uraia wao una utata

Ova


Kama ni hivyo hata Mlm.Nyerere an Familia yake Uraia wao una Utata kwa maana asili yao ni Unyarwanda/Baganda, hapo walipo walihamia tu!
 
Unajua hii nchi watu wamefundishwa chuki,fitina na uhasidi,hii nchi haitiendelea tusipo badilika,ukifika namanga upande wa kenya mtanzania unagongewa miezi tatu hata sita ukitaka ,kwetu mkenya anapewa mwisho siku saba mimi sielewi tuliingia E.A.C kwa nini,toka mwalimu kulikuwa na kipindi maalum ya majungu ilikuwa inaitwa Mikingamo,sasa vizazi vilivyo fuata vimekuwa ni chuki,wivu,fitina na uhasidi dhidi ya walionacho,kwani ardhi wakinunua na wewe siununue kama unaweza?penda usipende dunia inabadilika na kama mnataka viwanda sheria ya ardhi lazima itabadilika kama dunia ingine,hivi ardhi ya tanzania inathamani kuliko dunia ingine?mbona marekani,canada,uk nk watu wanaruhusiwa kununua ardhi,hii ni chi pekee watu wanakaa kwenye kahawa kubishania mpira,siasa na mali ya watu.
Kama unasubiria tulegeze kamba mnunue ardhi yetu hamta pata hiyo nafasi. Nyie hangaikeni na Kenyatta kwanza awagaie hizo ekari million moja afu ndo muongee
 
Je unajua kwamba sehemu kubwa ya watu waishio Tanzania waliozaliwa na kukulia hapa hawana Cheti cha kuzaliwa? Sasa unathibitisha vipi Utanzania wao? Vipi kuhusu Wamasai ambao hawana karatasi yoyote ile? Je ni Watanzania au Wakenya?
Hilo la watanzania kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa sio hoja, watanzania tunajuana. Hata ukijiita mhaya au muha na kuongea lugha zao bado tutakujua tu. Familia zimejengwa katika misingi ya koo, na muunganiko wa koo ndio unatengeneza kabila na muunganiko wa makabila ndio unazaa utaifa, sasa wewe jifanye mtanzania utaulizwa kabila lako ukisema kabila lako utaulizwa koo yako na baada ya koo utaulizwa familia ulikotoka na hapo utakuwa umejulikana kwa sababu makabila yetu na koo zote zimetapakaa nchi nzima, hakuna mtanzania asiyemjua mwenzake hata wewe mnyarwanda watu wamekujua mtandaoni ingawa hawakuoni sasa hao unaoishi nao wanakujua nje ndani, cheza na watu wengine sio watanzania.
 
Unajua hii nchi watu wamefundishwa chuki,fitina na uhasidi,hii nchi haitiendelea tusipo badilika,ukifika namanga upande wa kenya mtanzania unagongewa miezi tatu hata sita ukitaka ,kwetu mkenya anapewa mwisho siku saba mimi sielewi tuliingia E.A.C kwa nini,toka mwalimu kulikuwa na kipindi maalum ya majungu ilikuwa inaitwa Mikingamo,sasa vizazi vilivyo fuata vimekuwa ni chuki,wivu,fitina na uhasidi dhidi ya walionacho,kwani ardhi wakinunua na wewe siununue kama unaweza?penda usipende dunia inabadilika na kama mnataka viwanda sheria ya ardhi lazima itabadilika kama dunia ingine,hivi ardhi ya tanzania inathamani kuliko dunia ingine?mbona marekani,canada,uk nk watu wanaruhusiwa kununua ardhi,hii ni chi pekee watu wanakaa kwenye kahawa kubishania mpira,siasa na mali ya watu.
Duuh ! Mkuu umefunguka kimantiki kweli kweli. Mwenye kuelewa ataelewa.
 
Wanajamvi
Hili suala linatisha. Mimi ni member wa sehemu moja maarufu hapa Jijini. Ni sehemu ya Kula. Mnamo tarehe 31 May 2017 jioni, nilikaa meza Jirani na wakenya kama watano hivi wanaume wanne na mwanamke mmoja. Mara baada ya dakika kadhaa, alikuja jamaa mmoja aliyejumuika nao. Takriban dakika 30 baadae Yule jamaa kufika, alitoa rundo la Pasi ZA kusafiria ZA kitanzania ambazo hawa wakenya waligawiwa. Bila kupoteza muda, wakenya walitoa mfuko mweusi wa plastiki na kumkabidhi hawa jamaa na ghafla kuondoka. Nilitamani kujua kwamba zile pasi mpya zilikuwa za nini?

Sikufanikiwa ila, nilifanikiwa kuongea na mmoja wa hawa wakenya, ambaye pamoja na lafudhi yake aliniambia yeye ni mchaga wa Tarakea. Hawa Jirani zetu wananunua ardhi kwa kasi ya kutisha kutumia vitambulisho vya kitanzania. Wanajiita watanzania. Wanyarwanda pia hivyo hivyo. Ofisini kwetu kuna mdada mnyarwanda pia mwenye Pasi ya Tanzania anajiita muangaza. Nadhani kuna tishio kubwa mbeleni utakaotokana na watu kujizolea hizi passport za kutanzania
kwa nini hukupiga simu polisi kama unajitambua na kuwapiga picha bila wao kujua ili kuisaidia nchi yako katika upelelezi?
 
Acha kelele uzembe umeufanya mwenyewe ulikuwa wapi kwenda kutoa taarifa??? Umeniudhi ningekuwa karibu na wew ningekupiga na kibao. Yani watanzania sijui tumeumbwaje wew umeliona tukio live ukaacha umekuja kulalamikia mtandaoni na hii tabia ya kukosa uthubutu ndiyo inayotumaliza...!!!
Mbona ameshatoa njia? huyo Mkenya si amesema anatoka Tarakea uhamiaji wafatilie passport zilizotoka hv karibuni kumpata huyo mtu then wakibaini ni kweli wambane awataje na wenzake
 
Hilo la watanzania kutokuwa na vyeti vya kuzaliwa sio hoja, watanzania tunajuana. Hata ukijiita mhaya au muha na kuongea lugha zao bado tutakujua tu. Familia zimejengwa katika misingi ya koo, na muunganiko wa koo ndio unatengeneza kabila na muunganiko wa makabila ndio unazaa utaifa, sasa wewe jifanye mtanzania utaulizwa kabila lako ukisema kabila lako utaulizwa koo yako na baada ya koo utaulizwa familia ulikotoka na hapo utakuwa umejulikana kwa sababu makabila yetu na koo zote zimetapakaa nchi nzima, hakuna mtanzania asiyemjua mwenzake hata wewe mnyarwanda watu wamekujua mtandaoni ingawa hawakuoni sasa hao unaoishi nao wanakujua nje ndani, cheza na watu wengine sio watanzania.


Sasa huo ndiyo ujinga wenyewe, ni wapi Dunia hii Utaifa utambulika kwa watu kusikilizana kilugha? Vipi Mjaluo wa Kenya na wa Tanzania wanasikilizana pia, Watu wa Mara na Waluya wa Kenya wanasikilizana pia, au Wahaya/Waganda/Wanyarwanda wanasikilizana pia, ukienda Kilimanjaro Wataita wa Kenya na Wapare wa Tanzania wanasikilizana pia, Wadigo wa Tanga na wa Mombasa Kenya wanasikilizana pia, Wamasai wote wa Kenya na Tanzania wanasikilizana pia, sasa Utanzania ni upi?
 
Wanajamvi
Hili suala linatisha. Mimi ni member wa sehemu moja maarufu hapa Jijini. Ni sehemu ya Kula. Mnamo tarehe 31 May 2017 jioni, nilikaa meza Jirani na wakenya kama watano hivi wanaume wanne na mwanamke mmoja. Mara baada ya dakika kadhaa, alikuja jamaa mmoja aliyejumuika nao. Takriban dakika 30 baadae Yule jamaa kufika, alitoa rundo la Pasi ZA kusafiria ZA kitanzania ambazo hawa wakenya waligawiwa. Bila kupoteza muda, wakenya walitoa mfuko mweusi wa plastiki na kumkabidhi hawa jamaa na ghafla kuondoka. Nilitamani kujua kwamba zile pasi mpya zilikuwa za nini?

Sikufanikiwa ila, nilifanikiwa kuongea na mmoja wa hawa wakenya, ambaye pamoja na lafudhi yake aliniambia yeye ni mchaga wa Tarakea. Hawa Jirani zetu wananunua ardhi kwa kasi ya kutisha kutumia vitambulisho vya kitanzania. Wanajiita watanzania. Wanyarwanda pia hivyo hivyo. Ofisini kwetu kuna mdada mnyarwanda pia mwenye Pasi ya Tanzania anajiita muangaza. Nadhani kuna tishio kubwa mbeleni utakaotokana na watu kujizolea hizi passport za kutanzania
Usishangae, kwa hapa kwetu Tz hiki ni kitu kinachowezekana kabisa maana tumeshaipuuza misingi ya usalama wetu kama taifa. Kama tuliweza kuwa na Afisa wa ngazi ya juu katika jeshi letu ambaye ni mnyarwanda, kwenye pasipoti itashindikanaje? Hata hivyo, wewe kama raia mwema, umechukua hatua yoyote kutoa taarifa kwa vyombo husika?
 
Back
Top Bottom