Wakenya hawajui Magufuli naona!

Wakenya hawajui Magufuli naona!

Uzalendo huanzia nyumbani, kwanini mnashabikia vyombo vya nje vinavyomkebehi rais wetu ? Hii tabia kamwe haivumiliki na inakera. Rais ni wetu hata kama ni vipi acha sisi wenyewe tukosoane, na sio kushabikia watu wa nje, punguzeni ujuha
Kwani hiyo cartoon ni uongo.Mnajificha kwenye uzalendo feki.
 
Uzalendo huanzia nyumbani, kwanini mnashabikia vyombo vya nje vinavyomkebehi rais wetu ? Hii tabia kamwe haivumiliki na inakera. Rais ni wetu hata kama ni vipi acha sisi wenyewe tukosoane, na sio kushabikia watu wa nje, punguzeni ujuha
Vipi alipokuwa anasifiwa na hivyo vyombo vya nje?
 
Huu ni ushabiki maandazi Magufuli anafanya kazi na wao washaona soon tunawapiga bao hzo ni propaganda chafu na wanajua mwaka huu Uchumi wetu utakua uko stable zaidi kuliko wao.
ukifungia radio ndiyo uchumi unakua??
 
hao hao wakenya walipokuwa wanamsifia na kujiita magufuli lumumba mlitokwa na mapovu kwa kushangilia,ukishangiliwa sana jukwaani basi jiandae na kuzomewa jukwaani ndio kawaida hiyo
Kwa maana nyingine wewe una shabikia rais wako kukashfiwa na raia wa nchi nyingine ? Hata kama baba yako ana mapungufu, wewe utashabikia unaposikia jirani yako wana mkashifu ?
 
washughulike na ya kwao ya Tanzania watuachie wenyewe
Huwezi kuacha kuzungumzia jambo ambalo linawagusa jirani zako, watu wengi wanadhani Magufuli akiharibu au akiboresha nchi yetu, wanao athirika au kunufaika ni Watanzania peke yao, hapana!! inawagusa watu wengi ukanda mzima wa EA utaguswa kwa namna moja au nyingine, wewe unadhani Kesho Tarehe1 Sept2016 Mvututano wa Polisi na wananchi wanaodai utawala wa kisheria yakitokea mauaji Kenya haitawagusa? Uganda haitawagusa? Ndiyo maana yale yanayoendelea Burundi huwa yana madhara hata kwetu hasa changamoto zitokanazo na wakimbizi, jifunze kufikiria mbali kidogo.
 
Kwa maana nyingine wewe una shabikia rais wako kukashfiwa na raia wa nchi nyingine ? Hata kama baba yako ana mapungufu, wewe utashabikia unaposikia jirani yako wana mkashifu ?

bila kufanyahivyo hawezi kujielewa,hata kama baba yangu kwakuwa namtakia mema nitashabikia ili abadilike
 
Wizara ya mambo ya nchi za nje iombe maelezo toka balozi wa kenya.Na imwandikie kulaani hicho kitendo cha hilo gazeti kutudhalilishia Raisi wetu.Wakati waziri wa habari na utangazaji alifungie kukanyaga Tanzania
Hahaha dawa inaingia taratibu hakuna namna.
 
Kwa maana nyingine wewe una shabikia rais wako kukashfiwa na raia wa nchi nyingine ? Hata kama baba yako ana mapungufu, wewe utashabikia unaposikia jirani yako wana mkashifu ?
Ndio kiwango chake.
 
Utendaji wa Raisi Magufuli unaharibiwa na chuki na ukandamizaji mkubwa wa demokrasia kuanzia bungeni, media, mpaka kwa raia. Ngoja tuone mwisho wake. Sijui kama hayo ndo mageuzi alohubiri wakati wa kampeni
Straight up mkuu
is just remaining to be seen
 
Back
Top Bottom