Nilipoenda Tabora kumtembelea mdogo wangu, nilistaajabu kushuhudia ninayoyasimulia leo.
Bwana mdogo kaanza karibuni maisha ya kujitegemea, kapanga chumba kimoja na sebule maeneo ya chemuchemu.
Pale pia kuna jamaa mmoja mpangaji mwenziye kapanga chumba na sebule lakini akiishi na wanawake wawili mitala kwa kutumia chumba kimoja.
Wake zake hao wanaishi kwa upendo mkubwa huku wakiitana dada. Kazi na hadi kula wanakula pamoja!
Ndugu zangu wataalamu wa saikolojia, jambo hili sijawahi kuliona popote Tz.
Maana kama ni ukewenza, ni lazima mwanaume awajengee nyumba zao tofauti, ama kama ni kupanga atawapangia nyumba tifauti.
Ni maarifa gani yanayosaidia mwanamme kuwamudu, kuweza kuishi nao kwa ukitumia chumba kimoja na wanawake wakaelewana kama kulwa na doto, kiasi cha kuwa ni mfano wa kuigwa?