KwetuKwanza
Senior Member
- Mar 13, 2023
- 121
- 218
Tumelalamika sana, tumefikia hatua hadi ya kuandika barua kwa Mamlaka ya TARURA, kila tunapofanya hivyo wanakuja kupiga picha kisha wanasema watashughulikia, wakiondoka hawarudi hadi twende tena, tukienda kama kawaida wanakuja kupiga picha na kuondoka.
Makazi yetu yanazidi kuharibika, usalama wa nyumba na miundombinu mingine ni mdogo kutokana na maji kupita juu ya Barabara kutokana na njia ya Kalavati kuzidiwa na maji.
Kama mnavyojionea kwenye picha na video hyo ndio adha tunayopitia, wakati huu wa mvua mambo ndio huwa mabaya zaidi.
Barua yetu kwa Mamlaka husika