Wakazi wa Dar Es Salaam wanakwamisha Mageuzi Tanzania.

Lima shamba ukishavuna utapata nauli ya kuja Dsm kisha tuone utakuwa na msimamo gani? Sasa hivi upo kijijini huko umepauka na udongo mwekundu kama kituko utaongea hayo. Karibu Dar mji wa wajanja.

you speak like The Don and yet you call yourself Mnyanyaswaji!anyway kama unanyanyaswa na mkeo ni bora kabisa lakini kama unanyanyaswa na maisha unahitaji kujitambua!
 
Dar hakuna maendeleo - kuna msongamano wa watu tu! Miaka 3 mbele Mwanza mtaisoma namba!

Wewe kweli unachekesha Mwanza inaweza kuishinda Dar? Mwanza yenyewe mjini kuna barabara mbili Nyerere na Kenyata... Ukizunguka na baiskeli siku mmoja unaumaliza mji wote.
 
Umekosea sana ndugu. vyama vingi vya siasa chimbuko lake Dar es Salaam. Dar ndiyo chimbulo la mageuzi Tanzania. Mkutano wa kwanza wa mageuzi ulifanyika Motel Agip Dar es Salaam, siyo Arusha. Mtei, Mareale, Makani na timu yake walianzisha chadema Kisutu Dar es Salaam.

Magazeti kama Shaba, Watu, Family Mirror, Majira ndiyo vyombo vya habari vya mwanzo kutoa elimu ya uraia kuhamasisha watu kufikiri kimageuzigeuzi ndipo wewe ukapata elimu inayokupa werevu katika siasa.

Hawa watu wote wanakaa Dar es Salaam. Dar es Salaam ndiyo msingi wa mageuzi Tanzania. Kwa sasa ni kama baba ambaye kajichokea kwa mahangaiko ya muda mrefu na umri kwenda sana, wanae wameshakuwa wakubwa ndio wanahangaika sasa huko pembezoni kumsaidia baba.

Nina hakika baba huyu akiitazama Arusha leo, na Mwanza, na Mbeya, Tandahimba, na Songea, Iringa mjini nasikia eti hata Dodoma? moyo wake unapata faraja! Ipe Dar es Salaam sifa inayostahili.

Ni kweli vijana wana nguvu sana sasa. Lakini halikuanza jana Arusha, mkuu!

Chonde jamani, hiyo ni sumu kwa umoja unaohitajika. Kwanini tuanze kujiona bora kwa kanda zetu? Harakati ziwe zimeanzia kokote pale Tanzania, ni kwa ajili ya watanzania kwani nani ni bora zaidi ya mwenzie? Hiyo ni sumu mbaya sana! La msingi ni kudumisha umoja na si kulumbana. Mungu wetu mmoja, anaita sasa!
 
Ni kweli kabisa.Dar waoga sana.wanashida kibao lakini wanakufa na tai shingoni.
 
Wakazi wa Dar wanaelewa vizuri kuwa wanasiasa ni sawa na wafanyabiashara tu, wote wanatafuta pesa, umaarufu na sifa. Tofauti ni kuwa mfanyabiashara anauza bidhaa na huduma, mwanasiasa anauza maneno, ahadi na uongo.

Tumekataa kuwa wateja wa wanasiasa. Tofauti ya CCM, Chadema, CUF, TLP, UDP n.k ni sawa na tofauti ya biashara ya mafuta, vifaa vya ujenzi, duka la mapambo, saloon n.k Chapa kazi, hakuna mwanasiasa atakaekuletea maendeleo kwa hapa kwetu. Ndio ajira zao hao

Saluti mkuu! Umenena mkuu ila tunahitaji actions, na isiwe Dar pekee, na iwe hivyo nchi nzima. Ukombozi wetu u mikononi mwetu wenyewe, umoja wetu na kuthubutu kwetu, ndiko kutakapotupeleka kwenye furaha ya kweli.
Mungu wetu anaita!
 
Dar Jimbo ambalo bado litaendelea kusumbuwa mabadiliko ni jimbo la Ilala lililojaa Wahindi na Waswahili kama Faiza Foxy na jimbo la Kinondoni lililojaa makahaba, mafuska, mateja, wezi, Matapeli, Wasanii na kila aina ya machukizo machoni pa Mungu.

Jimbo la Kinondoni wengi wao hawaoni hata umuhimu wa kuwepo Serikali na ingewezekana kwa amri yao basi Rais wa Ngwasuma ndiyo huyo huyo angekuwa Rais wa Nchi.

Majimbo yaliyobaki kama Kawe na Ubungo hapa somo linaeleweka vyema, Temeke na Kigamboni, wakazi wake wengi ni wandengereko na wamatumbi, Uislamu na uswahili ni sehemu ya advatage ya kushinda jimbo hili.

Ukonga na Segerea ni majimbo ambayo yapo kibla ni Chadema tu inayopaswa kujenga mtandao imara ili kuyachukuwa majimbo haya mawili, hakuna tatizo lolote kwenye haya majimbo.

Ukonga na Segerea ni Dar es salaam? Nadhani hata nyumba na viwanja vya huko havijapimwa ni Squat ni sehemu za wageni wa Dar es salaam ndio maana magereza yapo huko...wapo wakurya wanauza mayai, Wahaya, Waha na polisi na wanajeshi waliyochoka.
 
Wakazi wa Dar wanaelewa vizuri kuwa wanasiasa ni sawa na wafanyabiashara tu, wote wanatafuta pesa, umaarufu na sifa. Tofauti ni kuwa mfanyabiashara anauza bidhaa na huduma, mwanasiasa anauza maneno, ahadi na uongo.

Tumekataa kuwa wateja wa wanasiasa. Tofauti ya CCM, Chadema, CUF, TLP, UDP n.k ni sawa na tofauti ya biashara ya mafuta, vifaa vya ujenzi, duka la mapambo, saloon n.k Chapa kazi, hakuna mwanasiasa atakaekuletea maendeleo kwa hapa kwetu. Ndio ajira zao hao

Maelezo yako ni uthibitisho wa uhakika kwamba wewe na hao watu wa Dar unaowasemea hamna uelewa wowote juu ya siasa, biashara, kazi na maendeleo ya nchi. Uboreshaji wa huduma za jamii na maendeleo katika nchi ni matokeo ya wanasiasa makini ambao wanaweka mipangilio au policy au sera sahihi na kuzisimamia kwa ufanisi, huwezi kuwa na sera asi kwa jamii na legelege kama ccm halafu utegemee nchi iendelee kwa vile tu wananchi wake wanachapa kazi sana! ni sawa na kuzaja maji kwenye ndoo iliyotoboka. Kati ya mambo manne ambayo mtumishi wa umma na baba wa taifa mwl JKN alisema ni lazima yawepo ili tuendelee ni SIASA SAFI na UONGOZI BORA. Waambie hao wachapa kazi wa Dar kwamba pamoja na huo uchapaji kazi wao ambao ni jambo jema lakini pia wanahitaji kuwepo kwa siasa safi na uongozi bora vitakavyo wapatia sera thabiti za kuboresha shughuli zao za kimaendeleo. Ni sawa na nyumba ya thamani kubwa, kama imejaa vumbi, takataka na furniture zimetapakaa ovyo ovyo kila mahala na vyoo havi - flush haitafaa kuishi binadamu hadi pale itakaposafishwa, furniture kupangiliwa na vyoo kuzibuliwa. Dar huu ni muda wa kusafisha siasa na uongozi katika taifa letu tunalo lipenda, siyo kulala na kudai kushoshwa.
 
Ni ukweli usiopingika kuwa wakazi wa jiji la Dar Es Salaam ndo wanaokwamisha mageuzi ya kweli hapa Tanzania kwani Dar kila mtu anajifanya yuko bize na mambo yake eti wanatafuta hela! Kwani mikoani watu hawajui kutafuta hela?

Wakazi wa Dar wanapenda kufuatilia sana mambo ya UDAKU kama mambo ya Kanumba, Lulu, Wema, Diamond, Johari, Jokate. UBITOZI NA USHAROBARO kwa kwenda mbele.

Mara nyingi mageuzi yanaanzia kwenye majiji makubwa kama Dar, wakazi wa Dar badilikeni.....!!!!
Tuombe radhi bwana... si kila mtu anajifanya, si wengine hatujifanyi, tuko bize kweli... tuombe radhi lol
 
uliyosema ni sawa, ila kwa sasa Dar ni watetea ufisadi. Wanazidiwa hata na Kigoma. Waamshe wenzako ambao joto limeathiri uwezo wa kufikiri


Umeongea vizuri sana mkuu. Labda tatizo tu ni kwamba mimi si mwanasiasa, ingawa uelewa wangu ni kwamba haya mambo si tofauti sana na mbio za kupokezana kijiti. Waliokuwapo miaka ya 90 wakati vuguvugu la mageuzi linaanza kazi yao kubwa ilikuwa kuandaa ambacho unakiona sasa: kuelimisha watu juu ya alternative thinking, na kuwaelimisha wajue inawezekana. Hawa vijana kina Zitto, kina Mnyika, Kina marehemu Regia, na huyu kijana wa CUF namsahau jina lake hapa lakini mwenye uwezo mkubwa sana kujenga hoja sijui nani anaitwa yule, walikuwa watoto wa shule za msingi na sekondari wakati huo. Ni hizi jitihada za awali ndiyo ziliwapa ufahamu wa haya yanayotendeka sasa, ukichanganya na mpango-mkakati kabambe wa vyama fulanifulani kulenga vyuo vya elimu ya juu. Kwa hiyo mimi ninapowaona hawa vijana moyo wangu unafarijika sana nikiamini kwa moyo wangu wote yaliyofanywa mwanzo yalikuwa mema.

Wamechukua kijiti cha mageuzi kutoka kwa hao walioanza nacho katika hizo mbio za kupokezana, wapo mbioni, na kazi ni nzuri sana. Elimu na msisimko wa awali kiini chake kilikuwa Dar es Salaam. Upe sifa inayostahili mji huu kwa kazi nzuri ya awali.:yo:
 
vipi wewe uliyeko mkoani mbona umeshindwa kuleta mabadiliko kwenye jimbo lako na sasa unaongonzwa na mbunge wa CCM mwenye elimu ya Darasa la saba na toka aingie madarakani mpaka leo hajawahi hata kulisemea jimbo lake Bungeni, iwe kwa kuonngea hata kwa maandishi. Ungekuwa na mwamko ungeanzia jimboni kwako na kuwaelewesha kuhusu hasara ya kumchagua mtu yule kwa kisingizio tu alitumia pesa zake nyingi kuhonga wananchi ili achaguliwe kwa maslahi ya kulinda biashara zake hasa zilizoko Mwanza. Na wote kwenye jimbo lako wanafahamu fika kwamba Mbunge wenu ana historia mbaya ya kujihusisha na wizi wa mifugo huko nyuma na hilo watu wengi wanalifahamu, hasa pale alipoamua kununua ng'ombe na kurejesha kwenye baadhi ya kaya aliyowaibia huko nyuma.

Wito kwako; Anza mabadiliko kwako kwani jimbo lako linahathirika kwa kiasi kikubwa sana na matatizo ya kiuchumi na hata kiafya, kwani wananchi walio wengi hawana uelewa kuhusu UKIMWI na hivyo wengi wanaangamia huku wewe na mbunge wako mnaendelea na biashara zenu bila kuwa na mipango mbadala wa kuwasaidia wananchi wa jimbo lenu.

Bora Dar kuna maendeleo na hata watu wanauelewa kuhusu mambo ya kiafya kuliko jimbo lako.

TELO.



:A S shade::yo::lying: :lying::lying: Nimekugongea lying 3 mkuu na shade, na inaelekea wewe ndio mtu wa yo kwa sana. Infact umeongopa halafu umesema kwa upuuzi. Humjui aliyepost thread anatoea wapi umekimbilia kuongea utafikiri hujui kuwaza. hapa ni mahali pa great thinkers bwana.

coming back to Dar. Ukiangalia kwa makini mji kama A-town wanaopenda mageuzi ni vijana, tena hawa haijalisha wana elim gani au fedha kiasi gani wako front line kutafuta mageuzi ya kweli, jambo ambalo ni kinyume sana na hapa Dar. Wengi wa vijana ambao wangependa kuleta mageuzi kwa hapa Dar ni wahanga wa hal ngumu ya maisha, kazi hawana, riziki ya siku inagomba,maisha yanabana kila kona. Kwa hili hata hiyo nguvu ya kwenda front kijana huyu anakosa. Ndani ya kundi hili ndimo wapo wale wafuga ndevu na wavaa pedo pusher ambao wao zaid ya kufundis jihad hawana jingine. ila hili kundi ni hatari kwani siku hizi mtoto mdogo wa 7-9 yrs anaweza akakutoa nishai kwa karate na hili wanafundishwa kwenye chuo. wao wanajihami tu kwa lolote lile.

kibaya zaid wale wanaokula milo 7 kwa siku ni watoto wa vigogo au wa watumish wa umma wa kawaida ambao wao huwez kuwaambia kitu kuhusu magamba wakuelewe, hawa huwa wafuasi sana wa miziki kwenda club na kufuatilia filamu tena kundi hili linajumuisha na wasanii wenyewe ambao siku za kampeni watatunga nyimbo za kuisifu ccm na hata filamu wakiamni kuwa kuwakaribu na ccm ni faida kwao. Wengine ni hawa maponjoro na waarabu ambao wao wakiwa ghorofani basi wanajua serikali ya ccm ndo nzuri, na wanaogopa vyama vingine ka kuhofia kunyang'anywa rasilimali zao bazo wamepokonya wabongo.

kuna kundi kubwa sana la wabuya unga, na machangu hapa dar ambao wao serikali iwepo isiwepo ni sawa wao wanachojali ni stimu zao za mihadarati na urembo wawe kama majini wapate mabwana. hawa akili tu ya kujiwazia wao wenyewe hawana asembuse ya kuwaza juu ya taifa.

ushauri wangu: upinzani uliyaona haya na ukapuuzia mkoa huu lakin sasa inabidi wauamshe ili kuleta mapinduzi ya dhati.
 
Chonde jamani, hiyo ni sumu kwa umoja unaohitajika. Kwanini tuanze kujiona bora kwa kanda zetu? Harakati ziwe zimeanzia kokote pale Tanzania, ni kwa ajili ya watanzania kwani nani ni bora zaidi ya mwenzie? Hiyo ni sumu mbaya sana! La msingi ni kudumisha umoja na si kulumbana. Mungu wetu mmoja, anaita sasa!

Hatujapishana sana kauli mkuu. Nilikuwa namjibu muanzishauzi ambaye nadhani hajui mchango wa jiji hili katika haya mambo.
 
Umekosea sana ndugu. vyama vingi vya siasa chimbuko lake Dar es Salaam. Dar ndiyo chimbulo la mageuzi Tanzania. Mkutano wa kwanza wa mageuzi ulifanyika Motel Agip Dar es Salaam, siyo Arusha. Mtei, Mareale, Makani na timu yake walianzisha chadema Kisutu Dar es Salaam.

Magazeti kama Shaba, Watu, Family Mirror, Majira ndiyo vyombo vya habari vya mwanzo kutoa elimu ya uraia kuhamasisha watu kufikiri kimageuzigeuzi ndipo wewe ukapata elimu inayokupa werevu katika siasa.

Hawa watu wote wanakaa Dar es Salaam. Dar es Salaam ndiyo msingi wa mageuzi Tanzania. Kwa sasa ni kama baba ambaye kajichokea kwa mahangaiko ya muda mrefu na umri kwenda sana, wanae wameshakuwa wakubwa ndio wanahangaika sasa huko pembezoni kumsaidia baba.

Nina hakika baba huyu akiitazama Arusha leo, na Mwanza, na Mbeya, Tandahimba, na Songea, Iringa mjini nasikia eti hata Dodoma? moyo wake unapata faraja! Ipe Dar es Salaam sifa inayostahili.

Ni kweli vijana wana nguvu sana sasa. Lakini halikuanza jana Arusha, mkuu!

Mtazamo mzuri lakini kama kila kitu kipo hapo dar kwanini watu wengi wakazi wa hapo bado wamepinda! ie ilikuwa ni rahisi sana kwa watu wa dar kuzitambua haki zao pia nakuzidai haraka kwa kuwa na mijitaasisi yooote nchi kuwa hapo dar! "hata kama hawajui kusoma hata kutazama hawawezi"
 
Hiyo mikoa inayoshabikia siasa uoni wao bado ni mdogo. Wengi wao ni watu amabao hawajawahi kufika hata Dar, sikwambii kutoka nje ya Afrika. Maendeleo hawajui ni nini na wala hawajawahi kuishi nayo. Kitu ambacho hukielewi bali unakisikia tu, sio rahisi kuweza kujua yupi anaweza kukileta. Ni rahisi kudanganywa. Dar watu wameshaanza kuzibuka..... wanasiasa hawawezi tena kula kwa migongo yetu. Wanasiasa wengi wa Afrika ni Wasaka Tonge
 
You're absolutely right. Dar people are obsessed with nonsense issues like the likes of Kanumba and many more. They keep busy in the name of searching for money and yet they're poor.

They don't sit down and dig deep to know the sourse of their poverty. Up country people have known that and now they are eager for change. Once freedom comes then I think the capital city must be shifted to any of the serious region from these LAZY Dar dwellers.

ur wrong
 
Wakazi wa Dar ni sawa na wakazi wa mkoa wa Kagera ambao ujifanya wanamageuzi wakiwa mikoa ya wenzao lakini kwao Magamba yameshika hatamu majimbo yote,mnatia aibu na unshomile wenu,tatizo mko wabinafsi na opportunist mnalalia upepo unakoelekea,sitashangaa CHADEMA ikiingia ikulu 2015 mkoa mzima mkavaa magwanda.
 
Wengi wao linapokuja suala la kuchagua wanaangalia dini ila hili linafutika taratibu ndio maana chama kile kilichokuwa kinakuja juu chneye wengi waumini wanaotoka dar kilunganishwa maana kilikuwa tishio kwa chama tawala kwa kuwa kiliogopa kupoteza kura za hao wenye imani hiyo,

kuhusu kushabiukia udaku, mpira kila jumamsosi au siku za soka utawakuwta wamejazana mabaani wanshabiaia liverpool mwanangu!! machester, Newcastels etc makombe ya ulaya wote wana ndoto za kuona ya ulaya tu!!

hawana habari na kinchoendelea ndani ya nchi juu ya mstakabari wa maisha yao!

Siku moja katika pita pita zangu katika kijiwe cha magazeti ile siku moja tu baada ya kongamano la kigoda cha mwalimu pale mkapa alipojitetea kuhusu ubinafishaji, siku hiyo magazeti yaliandika habari muhimul lakini cha ajabu kulikuwa na vijana kama kumi hivi wao wapo hapo kijiweni wanaangalia magazeti ya dimba , sports na wengine walikuwa wanabishana eti KANUMBA AMEONEKANA TABATA NA KULIKUWA NA GAZETI LILIKOUWA LIMEANDIKA HIVYO LA UDAKU, WAKABISHANA MWNINGINE AKASEMA HILI GAZETI LINASEMA UONGO KANUMBA ALIKUFA HATA MAMA SALMA ALIHUDHULIA MAZISHI YAKE!!



MUDA WOTE NILIKUWA NIMEKAA KIMYA NINAWASIKILIZA KWA MAUDHI NA UCHUNGU MIE NILINUNUA GAZETI LA MWANANCHI KUOSMA HOT NEWS ZA MKAPA KUUZA KILA KILA KITU NA KUSABABISHA UPOTEVU WA AJIRA NA KUWA HALI YA MAISHA YETU NI MBAYA!!

NILIWAGEUKIA WALE WATU KUMI KWA UKALI WA MANENO HIVI ACHENI HAYO MAGAZETI YA UDAKU YAWADAGNAYE SI HAYO NDIYO MNAYAOTAKA NA KUFURAJ=HIA ! HEBU FIKIRA NYIE NYOTE HAPA HAMNA AJIRA LAKINI JANA MANENO YANAYOHUSU MSTAKABARI WA TAIFA HILI YAMEJADILIWA LAKINI HAKUNA HATA MMOJA WENU ANAETAKA KUYASOMA KATIKA MAGAZETI YA TANZANIA DAIMA, NIPASHE, NK, HIVI KWA NINI MKO VERY UNCONSCIOULS KIASI HIKI??? NCHI INAONDOKA NYIE KILA SIKU MASCHSTERS, LIVERPOOL, KANUMBA ETC!! HUKU HAMNA AJIRA!!! MTANYONYWA HADI KWISHA KWA UJINGA WENU!

HAKIKA NINAKIRI YALE MANENO YALIWACHOMA WOTE WALIKAA KIMYA!!!!!!!!!!!!! WAKAANZA KUANGAZIA HAYO MAGAZETI YA NIPASHE,

NIKAPANDA KATIKA GARI LANGU HUYOOOO!! ILA WAPINZANI HAWAJAFANYA KAZI KUBWA KUWAELIMISHA WANANCHI!!


BADO WANANCHI WANAJUA BILA CCM HAKUNA AMANI!!!
Hiyo red ndio ukweli wenyewe
 
Wachache wanalala na njaa Dar.

Watachangamka pale patakapo kuwa na uhaba wa misosi.

A HUNGRY MAN IS AN ANGRY MAN.
 
Back
Top Bottom