Simulizi za Okello na Mapinduzi ya Zanzibar n Fitna tupu. Ikiwa historia ya Mapinduzi imejaa ukakasi, basi hata ushujaa anaovikwa Okello nao si lolote si chochote, ila binafsi Okello alipenda kutambulika kama shujaa na wakat mwingine akijiweka katika hadhi ya mithili ya Comrade Che Guavara. Ila kwa ufupi huyu bwana alikuwa mamluki na mwenue mitazamo hasi mno. Fuatilia masimulizi ya moja kwa moja kwa waliokuwepo kabla ya Mapinduzi, kisha fuatilia kutimuliwa mara mbili kwa John Okello, moja ikiwa Tanganyika uwanja wa Ndege mara ya kwanza akishinikizwa kuondoka Tanzania na Oscar Kambona 1963, na mara ya pili kufukuzwa kwake kwa amri ya Sheikh Karume baada ya Karume kuikataa rai ya kuuliwa kwa Okello. Alikuwa Mfitini, mrongo na mwenye kasumba ya kupenda ukuu!!