Wakati Mapinduzi yanafanyika, mzee Karume alikuwa wapi?

Wakati Mapinduzi yanafanyika, mzee Karume alikuwa wapi?

mkorobwe

Member
Joined
Sep 28, 2018
Posts
38
Reaction score
32
Habari zenu wakuu.
ukimsoma Harith Hasan kwenye" kwaheri ukoloni kwaheri uhuru" unaona kua wakati wa mapinduzi ya Zanzibar Jemedari mzee Karume alikuwa Dar- es Salam kwa ajili ya usalama wake na wa kimkakati. baada ya mapinduzi kufanikiwa alirudi zanzibar kupitia bandari ya Kizimkazi na kupokelewa na hayati ubwa Mwaboya ambae alikuwa ni mwalimu wa shule zama hizo.

kwa upande mwengine ukisikiliza simulizi ya mjane wa jemedari Karume anasema wakati mapinduzi yanaendelea mumewe alikua ndani na kufika saa karibu ya alfajir walikuja watu (wanamapinduzi) kumchukua Jemedar hadi studio za Radio ya taifa.

suali kwenu wajuzi wa historia ni upi ukweli katika haya?
 
Sisi waafrika Hata Historia ya miaka ya 1960s hatuna na kama zipo nyingi za kudanganyana .. Ndo mana bado Utaskia hadi MTU wa kwanza kuungundua(kuona) mlima Kilimanjaro ni mzungu ili kuonekana si so kitu... Mkuu kila LA heri kwenye swali lako hilo wajuzi waje
 
hili jambo limegubikwa na propaganda nyingi sana,yaani kuanzia mwanzo mpaka mwisho wake ni propaganda tupu.,yalotokea zanzibar sio mapinduzi ni mavamizi,kabla ya mavamizi haya wazanzibari walikuwa wanaishi maisha ya furaha zaidi kuliko maada ya mavamizi,hakuna historia ya waarabu wa zanzibar kuua au kutesa watu kama ilivyotokea wakati na baada ya mapinduzi.
masultani wa zanzibar walikuwa wazanzibari waliokuwa na mila na asili ya waarabu kama ilivyo saivi zanzibar

huyu hapa sultan sayyid khaliffa mtazame kama ni mwarabu, alikuwa sultan kuanzia 1879 mpaka 1960
Makerere-at-90-HH-Sultan-Zanzibar-Sir-Khalifa-II-bin-Harub-Mosque-30thApr1954.jpg
 
Nchi za Afrika tuna mambo/historia ya matukio mengi ya kale kuvutia au kuleta morali ya uzalendo,tatizo hatutunzi historia sahihi.Wenzetu wamefunza historia zao Kwa ajili ya vizazi vijavyo bila kujali historia hizo zilikuwa mbaya au nzuri.
 
hili jambo limegubikwa na propaganda nyingi sana,yaani kuanzia mwanzo mpaka mwisho wake ni propaganda tupu.,yalotokea zanzibar sio mapinduzi ni mavamizi,kabla ya mavamizi haya wazanzibari walikuwa wanaishi maisha ya furaha zaidi kuliko maada ya mavamizi,hakuna historia ya waarabu wa zanzibar kuua au kutesa watu kama ilivyotokea wakati na baada ya mapinduzi.
masultani wa zanzibar walikuwa wazanzibari waliokuwa na mila na asili ya waarabu kama ilivyo saivi zanzibar

huyu hapa sultan sayyid khaliffa mtazame kama ni mwarabu, alikuwa sultan kuanzia 1879 mpaka 1960View attachment 926678
Salute Mkuu. "Mavamizi sio Mapinduzi "
 
Habari zenu wakuu.
ukimsoma Harith Hasan kwenye" kwaheri ukoloni kwaheri uhuru" unaona kua wakati wa mapinduzi ya Zanzibar Jemedari mzee Karume alikuwa Dar- es Salam kwa ajili ya usalama wake na wa kimkakati. baada ya mapinduzi kufanikiwa alirudi zanzibar kupitia bandari ya Kizimkazi na kupokelewa na hayati ubwa Mwaboya ambae alikuwa ni mwalimu wa shule zama hizo.

kwa upande mwengine ukisikiliza simulizi ya mjane wa jemedari Karume anasema wakati mapinduzi yanaendelea mumewe alikua ndani na kufika saa karibu ya alfajir walikuja watu (wanamapinduzi) kumchukua Jemedar hadi studio za Radio ya taifa.

suali kwenu wajuzi wa historia ni upi ukweli katika haya?
Mkuu mkorobwe, simulizi ya Harith Ghassany ni urongo!, simulizi ya ukweli wa mahali alipokuwepo Karume, ni hiyo iliyotolewa na mjane wa Karume, ila hao wanapinduzi walipomfuata, sio kumpeleka Studio za Raha Leo, bali kwenda kumhifadhi mahala salama just incase Mapinduzi hayatafanikiwa!. Ndipo akaja bara na wanae Amani na Ali, akawaacha kwa Kawawa, yeye akarejea Zanzibar kupitia bandari ya Kizimkazi na kupokelewa na hayati ubwa Mwaboya ambae alikuwa ni mwalimu wa shule zama hizo.
Nawatakia maadhimisho mema ya kumbukumbu ya Mapinduzi ya Matukufu ya Zanzibar.
P
 
Mkuu mkorobwe, simulizi ya Harith Ghassany ni urongo!, simulizi ya ukweli wa mahali alipokuwepo Karume, ni hiyo iliyotolewa na mjane wa Karume, ila hao wanapinduzi walipomfuata, sio kumpeleka Studio za Raha Leo, bali kwenda kumhifadhi mahala salama just incase Mapinduzi hayatafanikiwa!. Ndipo akaja bara na wanae Amani na Ali, akawaacha kwa Kawawa, yeye akarejea Zanzibar kupitia bandari ya Kizimkazi na kupokelewa na hayati ubwa Mwaboya ambae alikuwa ni mwalimu wa shule zama hizo.
Nawatakia maadhimisho mema ya kumbukumbu ya Mapinduzi ya Matukufu ya Zanzibar.
P
Nakusalimia kaka paschal
 
Andika makala uishauri serikali iwe inawaalika ndugu wa John Okelo kwenye sherehe za mapinduzi.Jokes!Usijaribu.Utaitwa na bunge ujieleze.😝😝😝😝
Ha... haa!.
ila hili niliwahi kulizungumza hapa
Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar: Kumbe Waarabu Hawakufukuzwa! Walikimbia Wenyewe - Mzee Sukari nilisema

Siku ya kilele, kutatolewa nishani maalum za Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, sijui kama yule shujaa halisi wa Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar, Field Marshal John Okello, atakumbukwa!.
Paskali

P
 
Back
Top Bottom