Robert S Gulenga
JF-Expert Member
- Jan 3, 2013
- 2,161
- 1,493
Mtaji wa chama chochote kinacho taka kushika dola ni Imani ya Wananchi juu ya chama hicho inayojengwa na uwepo wa viongozi bora na wenye utashi. Chama cha Mapinduzi kwa namna kinavyoendesha siasa zake kwa sasa bila shaka wana nia ya dhati kuendelea kushika dola na hili linathibitishwakwa na namna wanavyoendesha uchaguzi wao wa ndani unaoendelea, CCM wameamua kuweka urafiki, udugu na mazoea pembeni, wameamua kuweka/kupitisha Wagombea ambao watakivusha chama na uchaguzi Mkuu wa 2025 na kuweza kuisimamia Serikali.
Kwa bahati mbaya wakati CCM wanaendelea na mipango hii ya kuhakikisha Wanaendelea kuwaelimisha Watanzania kuwa waendelee kukiamini chama hiki kwa namna kinavyoisimamia Serikali ili kuwaletea maendeleo yao, Vyama vingine mpaka sasa havina mpango wala muelekeo kuwa vinataka kweli kuwa chama dora, Vyama vimendelea kufanya kazi ya kila siku kukosoa mabehewa yaliyoletwa kupitia Twitter na mitandao mingine kama vile wapiga kura wako twitter, ikifika 2025 kwa sababu hawakujipanga vizuri ni watasusia uchaguzi au kusema wameibiwa kura.
Yaani mtu unaishi ughaibuni halafu ujenge chama kitakachoaminiwa na Watanzania ? Kaka yangu Lema, Tanzania kwa sasa ni salama na ina Demokrasia ya hali ya juu kuliko muda wowote, njoo umsaidie Mbowe kujenga chama ili msije lalamika baadaye mmeibiwa kura kumbe Watanzania wameamua kuiamini CCM.
Hongereni saana CCM kwa kuendelea kuisimamia Serikali ili kuwaletea Wanachi maendeleo, utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaonekana, sisi Watu wa kanda ya Kaskazini tunashukuru sana tumeanza kurudi kwetu kwa sikuku tunapita kwenye daraja jipya la WAMI. Hongera Serikali ya Awamu ya sita tumeona mabehewa kwaajili ya SGR yameshafika, kama kawaida wale wakubeza wameanza, lakini hata kipindi kile Ndege zinanunuliwa walibeza na kupinga lakini wamekuwa wa kwanza kuzitumia.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.
Kwa bahati mbaya wakati CCM wanaendelea na mipango hii ya kuhakikisha Wanaendelea kuwaelimisha Watanzania kuwa waendelee kukiamini chama hiki kwa namna kinavyoisimamia Serikali ili kuwaletea maendeleo yao, Vyama vingine mpaka sasa havina mpango wala muelekeo kuwa vinataka kweli kuwa chama dora, Vyama vimendelea kufanya kazi ya kila siku kukosoa mabehewa yaliyoletwa kupitia Twitter na mitandao mingine kama vile wapiga kura wako twitter, ikifika 2025 kwa sababu hawakujipanga vizuri ni watasusia uchaguzi au kusema wameibiwa kura.
Yaani mtu unaishi ughaibuni halafu ujenge chama kitakachoaminiwa na Watanzania ? Kaka yangu Lema, Tanzania kwa sasa ni salama na ina Demokrasia ya hali ya juu kuliko muda wowote, njoo umsaidie Mbowe kujenga chama ili msije lalamika baadaye mmeibiwa kura kumbe Watanzania wameamua kuiamini CCM.
Hongereni saana CCM kwa kuendelea kuisimamia Serikali ili kuwaletea Wanachi maendeleo, utekelezaji wa miradi ya maendeleo unaonekana, sisi Watu wa kanda ya Kaskazini tunashukuru sana tumeanza kurudi kwetu kwa sikuku tunapita kwenye daraja jipya la WAMI. Hongera Serikali ya Awamu ya sita tumeona mabehewa kwaajili ya SGR yameshafika, kama kawaida wale wakubeza wameanza, lakini hata kipindi kile Ndege zinanunuliwa walibeza na kupinga lakini wamekuwa wa kwanza kuzitumia.
Mungu ibariki Tanzania.
Mungu mbariki Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan.