Wajumbe wengine bodi ya Vodacom Tanzania watangaza kujiuzulu

dubu

JF-Expert Member
Oct 18, 2011
3,496
3,461
vodacom+pic.jpg


Leo Jumatatu Desemba 23, 2019 Kampuni ya Vodacom Tanzania imetangaza kujiuzulu kwa wakurugenzi wawili Andries Delport na Till Streichert kuanzia Mei na Juni 2020.

Wakurugenzi wawili wa bodi ya kampuni ya Vodacom Tanzania; Andries Delport na Till Streichert wametangaza kujiuzulu.

Tangazo lililotolewa na kampuni hiyo leo Jumatatu, Desemba 23, 2019 imesema Delport atajiuzulu Mei 14, 2020 wakati Sreichert akitarajiwa kujiuzulu Juni 30, 2020 au muda wowote kabla ya tarehe hiyo.
Kabla ya kuingia Vodacom Novemba 2017, Till alikuwa mjumbe wa bodi ya kampuni ya Safaricom ya Kenya kuanzia Agosti 2017.

Wakurugenzi hao wote walikuwa wafanyakazi wa Vodacom Group ya Afrika Kusini. Wakati Till akiwa ofisa mkuu fedha wa kampuni hiyo kuanzia Februari 2014 Delport alikuwa mkuu wa kitengo cha teknolojia.

Akiwashukuru kwa mchango walioutoa kwa muda waliohudumu, katibu wa Vodacom Tanzania, Caroline Mduma amesema: “Bodi inawashukuru na kuwatakia mafanikio mema katika shughuli zao.”

Wajumbe hao wametangaza kujiuzulu ikiwa ni miezi mitano tangu aliyekuwa mwenyekiti wao, marehemu Ali Mufuruki kufanya hivyo.

Chanzo: Mwananchi
 
Kwa dhambi yenu ya ubaguzi na chuki mlimgomea dada Mkenya na kumkatalia asije kurekebisha, haieleweki kwanini wanabodi wanajitoa mmoja mmoja, kaanza marehemu Mfuruki, sasa naona na wazungu pia wanafungasha wenyewe...
------------------------------

Two more members of Vodacom Tanzania Board of Directors have tendered letters of resignation. According to a statement issued Monday December 23, 2019 by the company secretary Ms Caroline Mduma, members who tendered their resignation from the board include Mr Andries Delport and Mr Till Streichert.
The statement says the duo would resign as non-executive directors of the company next year.
 
Kwa dhambi yenu ya ubaguzi na chuki mlimgomea dada Mkenya na kumkatalia asije kurekebisha, haieleweki kwanini wanabodi wanajitoa mmoja mmoja, kaanza marehemu Mfuruki, sasa naona na wazungu pia wanafungasha wenyewe...
------------------------------

Two more members of Vodacom Tanzania Board of Directors have tendered letters of resignation. According to a statement issued Monday December 23, 2019 by the company secretary Ms Caroline Mduma, members who tendered their resignation from the board include Mr Andries Delport and Mr Till Streichert.
The statement says the duo would resign as non-executive directors of the company next year.
Da we jamaaa acha unafiki, hapo kwenu CEO wa safari com, Bob, alikuwa mwingereza, alipofariki, CEO wa muda akawekwa mzungu! Kama mpo vzr kwanini hamkuweka mkenya? Acha kudandia treni kwa mbele jombaaa
Kujiuzulu kwa wanabodi ya Vodacom hakuna uhusiano na kukataliwa kwa huyo bi shost wa Kenya

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Da we jamaaa acha unafiki, hapo kwenu CEO wa safari com, Bob, alikuwa mwingereza, alipofariki, CEO wa muda akawekwa mzungu! Kama mpo vzr kwanini hamkuweka mkenya? Acha kudandia treni kwa mbele jombaaa
Kujiuzulu kwa wanabodi ya Vodacom hakuna uhusiano na kukataliwa kwa huyo bi shost wa Kenya

Sent using Jamii Forums mobile app

Sio sisi tuliofanya maamuzi ya nani wa kumuweka pale Safaricom, ila bodi yenyewe. Sasa nyie huko bodi inafanya maamuzi ya kumuweka mtu mnamkatalia kisa Mkenya kisha mnaweka mzungu, nilitegemea mtaweka Mtanganyika mweusi maana ndio kigezo mlitumia cha kumkataa Mkenya, kwamba mpo wengi wenye uwezo huo.
 
Kwa dhambi yenu ya ubaguzi na chuki mlimgomea dada Mkenya na kumkatalia asije kurekebisha, haieleweki kwanini wanabodi wanajitoa mmoja mmoja, kaanza marehemu Mfuruki, sasa naona na wazungu pia wanafungasha wenyewe...
------------------------------

Two more members of Vodacom Tanzania Board of Directors have tendered letters of resignation. According to a statement issued Monday December 23, 2019 by the company secretary Ms Caroline Mduma, members who tendered their resignation from the board include Mr Andries Delport and Mr Till Streichert.
The statement says the duo would resign as non-executive directors of the company next year.
majizi hayatasalia mbele ya Jiwe, rasilimali zetu zitalindwa kwa nguvu zote.
 
Back
Top Bottom