Nachukia hizi tabia za watu ambao wakiona jambo badala ya kuuliza na kulijua kiundani kutoka kwa wahusika badala yake wanakimbilia kwenye social network kutangazia udini. Its not fair kabisaaa!!!
Kwa kawaida Waislamu huwa wana ibada zao waachwe wafanye yao, kuna kipindi wanahamasishana kusaidia wasiojiweza misikitini, mahospitalini na hata mitaani. Watu hupewa mafurushi ya vyakula, fedha na hata madawa, hilo ni jambo la kawaida sana. Wengine wakiona hivyo tu tayari ni heading za udini...!!!
Mbona majuzi wamejikusanya na kuchangia bank ya damu na kwenye TV`s ikoneshwa na hakuna aliyesema ni udini??? Leo wachinje ngamia wao ili wawagawie wasiojiweza tayari ni swala la kuchinja jamani?? Mbona tangu tuko waadogo tunakula sana nyama za ngamia tunazogawaiwa misikitini na hakuna aliyehoji na raha zaidi hatukuwa na udini tulikuwa tunakusanya mpaka watoto wa dini zingine nao wanapeleka kwao!!!
Ngamia Waislamu wanaowafuga wanayama hawa nchini wakiamua kuchinja huwachinja kwenye maeneo ya misikitini na kugawa nyama bure kwa Waislamu wote waliopo pale msikitini, niwe mkweli sijawahi kusikia nyama ya ngamia inauzwa kwenye mabucha. Ingawa wakati mwingine hutokea Muislamu akasema mimi sadaka yangu kwa Mungu ni ng`ombe huyu achinjwe na agawanywe kwa Waislamu wote waliopo msikitini muda huo, ni mambo ya kawaida kwa Waislamu.
Tusiyafatilie haya mambo jamani, yatatupeleka pabaya sana, ni mtazamo tu!!!