John porter
Member
- Jul 8, 2013
- 65
- 28
Ndugu Zyamwelele, mimi kwa kweli nimefurahia sana ulivyosema. Umeamua kuwa objective na hiyo pekee ndio itakayotuondoa hapa tulipo. Kwa ujumla nawashangaa hawa wanaosema tunasemwa vibaya. La hasha, hatujasemwa vibaya ila tumeambiwa ukweli. Tatizo ni kwamba ukweli waliosema ni madudu tunayoyafanya kwa kuwalinda viongozi waliojaa ubinafsi. Mimi nawashukuru hawa jamaa walioandika, angalau tumeoneshwa kwamba madudu yetu si siri tena. Sasa badala ya kulalamika, tuichukulie kama ni changamoto, tuanze kuwawajibisha viongozi wetu ili rasilimali za nchi ziwanufaishe wananchi kwa ujumla wao na si viongozi na familia zao pamoja na wawekezaji.
Utakuwa umetuelewa vibaya.. Si mfuatiliaji saana wa siasa ila siku za nyuma Raisi wetu aliitwa kama sikosei "mpuuzi" ikawa kelele ooh kakosewa heshima aombwe radhi na kadhalika
Lengo la kuweka hayo yasemwayo na wazungu juu yetu ni kuwafahamisha enyi watanzania wenzangu muone uongozi wetu ulivyo kuwa mbovu kiasi kwamba Raisi wetu ambaye ni muwakilishi wa taifa hili tajiri anasemwa kama mtu asiye na wadhifa wowote.. Kama ukirejea hizo kauli za huyo mwandishi amemuongelea kiongozi wetu kama ombaomba hana mbele wala nyuma
Swali ni nini tufanye watanzania kuiepuka hii hali?
Kabla ya kulalama kutwa kucha kuhusu kipi ambacho serikali haitufanyii basi nasi tujiulize kipi tumeifanyia nchi yetu?