Nilikuwa kwenye ukurasa mmoja tunajadiliana hatua ya bunge la Tanzania kupitisha sera inayotia ugumu kwa waajiri kuajiri watu kutoka nje ya Tanzania. Katika majadiliano baadhi ya waajiri wakawa wanatoa misimamo yao, wengi walionesha kutokuwa na imani na wahitimu wa vyuo kutoka Tanzania. Hakika points wanazosimamia ni za ukweli, wahitimu wengi wanaakisi sura ya mazao duni vyuoni mwetu.
Tuache kuwabeza wasomi wetu kwa kuangalia vitu visivyo na mashiko.
1. Wasomi wa Tanzania wapo vizuri sana katika taaluma zao, tatizo kubwa ni lugha ya malkia.
2. Makampuni mengi hapa TZ wapo watz kibao ambao ndiyo vinara wa operations kubwa katika makampuni hayo. Mfano kampuni za SIMU hapa TZ zinategemea vichwa vya ki Tanzania kuliko hao mnaowahusudu.
3. Sijawahi kusoma ndani ya nchi ya Tanzania, lakini elimu ya Tanzania bado ni nzuri kuliko hata za hao mnaowahusudu.
4. Nimesoma na watu wa mataifa kibao, wengi wao walikuwa watupu, wana copy hadi assignment kutoka kwetu vijana wa Ki Tanzania. Sasa sioni faida ya hicho kiingereza chao kama darasani wao ni majanga
5. Ajira nyingi hapa nchini mmewapa hao majirani zetu ama kwa ulimbukeni ama kutokujua athari za mnachokifanya. Hivi juzi tumeshuhudia car parking ya hapa Tanzania iko managed na wafanyakazi wakenya, then bado mnajiona mna akili timamu.
6. Ma HR kibao kwenye makampuni hapa TZ ni wakenya na waganda na wao wamekuwa wakiwahifadhi na kuwaficha wahamiaji haramu au wale wanaofanya kazi bila work permit, bado mnajiona mmefanya uchaguzi sahihi.
Tuna kila sababu za kuwapongeza wabunge walioibua hii ISSUE kwani imeharibu na itaharibu ma deal kibao yaliyokuwa yakichezwa na hawa washenzi wanaojiita wafanyakazi wenye sifa.
Mwisho ndugu zangu wa Tanzania, tusibweteke. Kama unaweza kujifunza Driving muda wa jioni basi weka na muda mwingine ukasome lugha ya malkia pale British Council au kwingineko. Kujifunza ni sehemu ya maisha yetu.
Msiogope kwa kutojua lugha hiyo vizuri, waoneni wachina majority hawajui hiyo lugha lakini wapo mbali kimaendeleo kwasababu wanajituma na wanajifunza sikuzote.
Umasikini wetu upo mfukoni, SIYO KICHWANI.