Wahitimu wa Tanzania hamuajiriki

Wahitimu wa Tanzania hamuajiriki

Yaan hii thread inanikera kila niionapo,pumbaaav sana.
 
Nilikuwa kwenye ukurasa mmoja tunajadiliana hatua ya bunge la Tanzania kupitisha sera inayotia ugumu kwa waajiri kuajiri watu kutoka nje ya Tanzania. Katika majadiliano baadhi ya waajiri wakawa wanatoa misimamo yao, wengi walionesha kutokuwa na imani na wahitimu wa vyuo kutoka Tanzania. Hakika points wanazosimamia ni za ukweli, wahitimu wengi wanaakisi sura ya mazao duni vyuoni mwetu.
Kaka RENE JR,
Usiwe bias kiasi hicho,amini watanzania wana weza Bwana,ndio wapo wasiojiweza,kuwa na skills na wana apply,unataka kuniambia hakuna wenye good and skills zinazohitajika?mbona hawajawataja kuwa pia alipokea CV Za watu wazuri?
Huyu anashawishiwa na Wazungu kuwa Watanzania hawawezi...
Mwambie huyo HR Akitaka wafanyakazi wazuri Atangaze Dau zuri na Atangaze kwenye Magazeti ya Daily News,Guardian na Mitandao kama Kazi Bongo nk,Wazuri wapo,ni kiasi cha mtu anaacha kazi hapa anaenda huko kwake kama kuna maslahi mazuri..yeye anatangaza kazi yenyewe mshahara laki9 halafu anataka mtu mzuri sanaaaa,asubirie fresh from the school tuu,sisi wazoefu ili atupate aweke Dau Zuri...
Tena akome kutufanya wa TZ Hatuna kitu,yeye kkachagua cv Mbovu ndo anaweka hapa..ni kweli vijana wengi hawajui kuandika CV,BUT Sio wote..
 
Ujue wanafunzi wengi tunaxomea mitihani kwamba mitihani ije tufaulu lakini uhalisia wa kitu tunacho kisomea haupo ndomana ata waajiri wanataka mtu mwenye uzoefu wa miaka 7adi 10 na kwendelea ndo akukabidhi office...
 
Time Bandit;

Yan tume kwisha kabixa...inabidi sisi wanafunzi wenyew tujiongeze mda wa likizo ule kuomba temple za kujitolea ili kupata uzoefu wa kazi kutokana na taaluma tunayo isomea......
 
Last edited by a moderator:
FaizaFoxy;

Lol....kwa ao watu Jaman n halali mtu ulie na kucheka....at the same time
 
Last edited by a moderator:
hv huyu faizafix n raia wa wap..? kama n mtanzania huna haki ya kudharau elimu yetu kiasi hiki! kisa kujua kuandika aina ya vibarua.. wapo wanaojua zaid yako hawaongei.. mi natamani npate chance ya kuasses uwezo wako someday..

Nooo bro ujamuelewa faiza ni kwamba anatoa uzoefu wake aliokutana na watu uko ktk kuwa assess na ajadharau elimu ya mtu yeyote.....ucpanc bro
 
monaco;]

Ni WACHACHE SANA! Na kwa nini fresh from school ashindwe hata kujieleza tu, kitu rahisi...KUJIELEZA vyema, tena kwenye field yake aliyosomoea miaka mitatu chuoni! Barua ya maombi ya kazi ameandika graduate lakini haina tofauti na aliyoandika mtoto wa kidato cha nne! Hapo jamaa amesema wala hakuwa ametangaza nafasi yoyote ya kazi, waombaji tu walikuwa wakijaribu kumshawishi kuwa wanaweza kuifaa ofisi yake kwa namna moja au nyingine. Sikatai kwamba hata fresh from school wapo walio vyema, nachosema ni kwamba ni wachache sana. Vijana wanatanguliza maslahi mbele bila wao kuonesha "thamani yao", wewe umetoka chuoni mwaka huu unataka uanze na mshahara wa milioni mbili, haya nioneshe basi kwamba wewe una thamani hiyo, first impression inatakiwa iakisi thamani yako. Nadhani umeona mfano hai kutoka kwa faiza fox ,

INASIKITISHA!
 
Last edited by a moderator:
FAIZA FOXY...
Napenda pia jina lako,sana tuu dada yangu.

ok turejee kwenye mada;

Anyway labda hawa wa social sciences,but umesema kuandika barua na utaratibu umewapa ni kuweka katika kiingerreza tuu????,OK,NAKUJA KWAKO KWANINI Umpe mtu wa nje wakati kuna wanye uzoefu wazawa wa hiyo kazi?mimi nina Miaka 7 kazini lakini utafikiri nina Miaka 15 au 20.Mwanzo Mgumu..kuna on job training lazima mtoto anapoajiriwa kazini Akabidhiwe Mtu kwanza baada ya Mwezi 1 au2 anafanya mwenyewe.unakuta Boss kabisa ametoka chuo na Masters yake kaenda say ofisi Fulani anamkuta Technician ana miaka 17 kazini ndo alikuwa anakaimu nafasi ile,kwa hiyo ana kuwa nae say for 3 or 6 months baada ya hapo Mkuu anakabidhiwa ofisi,ipo sana tuu hiyo.

Moja ya factor za Improve Productivity ni on job training,job rotation,training and development ili ku match Basic Principles za shule na kazi halisi.
wageni ni Mwiko kwangu kabisa wakati wazawa wapo,hata experienced wa hiyo kazi wapo,coz wapo watu wanataka kubadilisha kazi ,na SHERIA MPYA YA AJIRA ZA WAGENI INAANZA MWEZI JULY,2015,Hawaruhusiwi kufanya kazi kama kuna Mtanzania mwenye huo ujuzi halafu yeye aje afanye kazi hiyo.imepitishwa juzi bungeni kama SHERIA/MUSWADA WA DHARURA.Itakuwa chini ya wizara ya kazi ndo itatoa vibali vya kazi na ku asses vyeti vya hao experts.
 
Kwa elimu yetu hii ya kukariri maswali ili tuweze kujibu mitihani wakati maarifa kichwani yakiwa ni sifuri unadhani atataujiri nani...?? Unaweza ukawa unafanya mahojiano na mtu mwenye degree ukadhani unahojiana mtoto wa darasa la saba kwa jinsi wasivyojua kujieleza......wanachokijua huko vyuoni ni kugomea mikopo ili wapate hela ya kufanyia starehe.......wasomi wa TAIFA hili ni mizigo na hasara kwa serikali na taifa kwa ujumla........
 
monaco;

Duh, hiyo miaka yako saba kazini ina walakini. Samahani lakini.

Soma tena post ya Faiza Fox utaelewa ni kwa nini hao vijana walipewa kazi ya "kuandika barua", jaribio dogo tu la communication skills linamwacha hoi graduate!...kweli mkuu? Waliona tabu hata kuatempt, wakatafuta visingizio kama kawaida ya wabongo!! On-job training kwa vitu basics ni gharama zisizo za msingi kwa kampuni, vinginevyo wangekuwa wanazoa tu watu.."tutawafundisha".
 
Last edited by a moderator:
Duh, hiyo miaka yako saba kazini ina walakini. Samahani lakini.
Soma tena post ya Faiza Fox utaelewa ni kwa nini hao vijana walipewa kazi ya "kuandika barua", jaribio dogo tu la communication skills linamwacha hoi graduate!...kweli mkuu? Waliona tabu hata kuatempt, wakatafuta visingizio kama kawaida ya wabongo!! On-job training kwa vitu basics ni gharama zisizo za msingi kwa kampuni, vinginevyo wangekuwa wanazoa tu watu.."tutawafundisha".
NOT ACCEPTED,
Dont generalised but be specific to a group of people...The portion is agreed the remain NOT AGREED AT ALL..I REMAIN NEGATIVE..
 
Kama mtu ambaye yupo serious anatafuta ajira ni lazima ahakikishe anajiendeleza kuhakikisha kuwa barua yake inaleta impression nzuri. Mfano kuna mitandao kadhaa inatoa kozi fupi bure kuhusu uandishi wa barua za kikazi na Cv Mfano

PRDV102: Resume Writing | Saylor Academy

Katika dunia ya sasa hakuna mtu atakuhurumia kwamba kwa kuwa unatokea kijijini hakuna umeme wala kompyuta wakati wenye sifa wapo tele



Corse ya kuandika barua alimaarufu communication skills vyuo ving huwa inafundishwa semista moja tuu ya mwaka wa kwanza na mtu unakuta anamiaka mitatu au mnne ndo anamalza unadhani atakumbuka kweli kuandika cv au official letter? Sasa change inabidi ianzie vyuoni ikiwezekana ilo somo lisomwe semista zote mwanafunzi awapo chuoni
 
FaizaFoxy

Kitu kinachojitokeza hapo pia ni kukosa kujiamini pengine ndio tatizo kuu la vijana wasaka ajira. Mtu anaenda kwenye inerview akiwa tayari anaamini sifa stahili hanazo lkn anajaribu tu. Nataka kushare nanyi interviea tatu za kazi nilizohudhuria.

Ya kwanza ilikuwa kwenye shirika moja la kimataifa arusha. Kabla ya interview niliingia net na kureview vitu gani natakiwa nivijue kabla ya kwenda interview. Nikaandaa list na nikahakikisha nimevipitia vyote. Shirika lilikuwa linaongozwa na mghana mholanzi na mkenya. Kulikuwa na candidate kama kumi na nafasi ilikuwa moja. Basi tukaanza interview ya kuandika maswali manne kwa mtindo wa essay. Baada ya kupewa karatasi msimamizi akatoka nje.

Kama kawaida ''simbi'' zikaanza. swali la kwanza linauliza tuandike tunalifahmu vipi shirika pamoja na vission na mission yake. Kila mmoja anamuuliza mwenzake kama anajua. Mimi nlikuwa nimeshasoma kwenye mtandao na wakati tunasubiri kuanza interview nikawa naperuzi vipeperushi kadhaa vilivyokuwa mezani zaidi kuhusu hilo shirika.

Kuepuka usumbufu nikaanza kujibu maswali mengine. Hata hivyo kwenye oral nilishindwa kujibu swali moja na hivyo sikuipata ajira hii. Baada ya mwezi mmoja walinipigia wakaniambia nilikuwa second best hivyo wanataka waniajiri tena. Nikaenda tukazungumza tukakubaliana na nikapangiwa tarehe ya kusign mkataba na kuanza kazi. Lakini ksichoriziki hakiliki kwani kabla sijasaini mkataba shrika likasitisha kuajiri ghafla nadhani project ilisimamisha.

Ya pili ilikuwa iringa ambayo nilijiandaa vyema zaidi ya ya kwanza. Katika hii interview nilibabaika kujibu swali moja lililoulizwa na mkurugenzi mmoja mmarekani kwani lugha yake ilinipiga chenga lakini wengine ambao walikuwa ni wakenya wakarudia kuuliza nikaelewa nikajibu. Niliamini ntaipata hii kazi. Baada ya wiki mmoja mkurugenzi akanipigia simu kwa namba yake ya simu ya mkononi. Akaniuliza kama ni mimi nliyefanya interview nilipojibu akaniambia sawa ataanipigia baadaye kunifahamisha zaidi. Nikajua tayari.

Ajabu wiki ikapita. Nikaona bora nimpigie mimi akapokea na akaniambia nisubiri watanipigia baadaye nikajua nimeshachezewa faulu. Baadaye nilikuja kufahamu kuwa katika tuliofanya interview alikuwepo mtoto wa kurugenzi mstaafu wa hiyo kampuni ambaye alipewa hiyo kazi lkn kutokana na ulevi wa kupindukia mwaka mmoja baadaye kazi ile ikatangazwa. Classmate wangu aliyekuwa kwenye kampuni ile akaniambia mabosi walijuta baadaye kwa kutonipa ajira.

Ya tatu ilikuwa unilever. Hii ilikuwa ya siku mbili na ngumu. Waliomba zaidi ya watu 300 tkwa nafasi nne. Tukaitwa kwenye interview watu 30. siku ya kwanza tukatembezwa sehemu zote za kampuni mpaka jioni saa 11 tukapewa karatasi yenye maswali manne ya kiutendaji. Siku ya pili asubuhi tukaingizwa kwenye ukumbi tukapewa swali tufanye debate na tuje na ufumbuzi huku tumevaa lebo za majina yetu kila mchangiaji wananote jina. Baada ya hapo ikawa ni face to face. Watu wanne wanakuuliza mmoja baada ya mwingine unamjibu maswali yake. Na yalikuwa maswali ya kiujumla kutokana background ya mtu lakini magumu. Mfano namna ambavyo umewahi kusolve matatizo huko nyuma ya kikazi au kimasomo. Hata hivyo nilitishika na mazingira na nikaamua siwezifanya kazi hapo. Tuliambiwa mwaka ulopita wafanyakazi 11 walikufa kwa kupigwa na radi na mwaka huo tayari 8 walishafariki. kampuni ilifunga minara ya kutect radd ambapo dakika 15 kabla ya radd taarifa husambaza na watu hukimbilia ndani haraka. Wakati tunasubiri interview mara kweli watu wakaanza kukimbilia ndani tukaambiwa tusitoke mpaka radd ipige. Nikaona dah siyawezi maisha hayo nikaomba usafiri wa kunrirudisha mjini na jioni hiyohiyo nikaondoka iringa. Hata hivyo nilijifunza mengi na nikajua kwa mazingira kama hayo hakuna mbabaishaji anaweza kupata ajira na hata wakurugenzi wengi wa hapo walitoka kenya.

samahanini kwa gazeti
 
Last edited by a moderator:
Umesema sawa kwa kweli sisi tu wazuri sana kwenye kukariri maswali na majibu ya mtihani mtindo wa kinyambari nyangwine. Wakati mwingine sio makosa ya mwanafunzi tu bali ya mtaala pia ambao haumpi mwanafunzi muda wa kutosha wa kujisome hivyo anaishia kuzima moto tu.

Jambo kubwa ni badala ya kuwa kunfidence za kijinga tuukubali ukweli huu na mtafuta kazi kujitibu mwenyewe kwa kujiendeleza kusoma kwa kuelewa.

Kwa elimu yetu hii ya kukariri maswali ili tuweze kujibu mitihani wakati maarifa kichwani yakiwa ni sifuri unadhani atataujiri nani...?? Unaweza ukawa unafanya mahojiano na mtu mwenye degree ukadhani unahojiana mtoto wa darasa la saba kwa jinsi wasivyojua kujieleza......wanachokijua huko vyuoni ni kugomea mikopo ili wapate hela ya kufanyia starehe.......wasomi wa TAIFA hili ni mizigo na hasara kwa serikali na taifa kwa ujumla........
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom