iunajua ukiwa na macho ya makengeza ukiangalia unaona watu wawili lakini kumbe ni mtu mmoja, sasa huyu mwenye makengeza asipojitambua kuwa macho yake ndio yenye tatizo anaweza kumlaumu mtu mwingine kama alidhani pale kulistahili kuwepo mtu mmoja.
lipo tatizo la watu wasio na sifa za kuwa viongozi lakini ambao ujanja umewafanya kuwa viongozi kutokujua the right aproach ya kufanya "recruitment" alafu wanaposhindwa kupata wanachokitafuta wanalaumu wengine.
mwajiri yeyote anayeweza kutoa kauli hiyo kwa shughuli zinazofanyika hapa tanzania kwa sasa kimsingi yeye ndiye mwenye matatizo.
kiukweli ukitafuta wataalamu wa nyukilia, wana sayansi za kwenda mwezini au nje ya dunia hao kwa tanzania huwezi kuwapata na mwajiri mwenye akili hawezi kulalamika.
lakini lipo tatizo la wahuni ambao wamepiga porojo tu wakaonekana wanafaa kumbe wababaishaji watupu wanapopewa ofisi hawakosi visingizio.
akiona mrembo anamuahidi kazi na hapo atafanya awezavyo kutengeneza nafasi ya kazi ama kwa kuweka nafasi ambayo haipo au kumfukuza mtu.
mjinga ndiye anaweza kuwa na kazi akaita mtu mmoja amletee maombi ya kazi na kama huyo atakosea aanze kulalamika.
hivi nini maana ya interview? au usaili?
pale kazi inapotangazwa wanajitokeza waombaji wengi, wapo wenye sifa, wapo wahuni wanaofoji sifa, wapo wasio na sifa lakini wanajaribu bahati yao.
sasa ni wajibu wa mwajiri kuwachambua hawa kupata mwenye sifa.
sasa wewe unaenda unamchukua mtu anayejiuza anakudanganya amesoma chuo fulani na unaamua kumuajiri lakini yale uliyomtuma afanye anaposhindwa bado unamtetea yeye na kuona shule alikosoma ndiko tatizo???? huo ni ujinga!
yeyote anayetafuta wafanyakazi kwa kuangalia rushwa ama ya fedha au ya starehe, yeyote anatafuta wafanyakzi kwa kutaka kuajiri watu anaowajua au kuwasaidia ndugu zake atavuna matokeo ya mfumo mbovu anaoutumia katika kutafuta wafanyakazi na matokeo hayo atabeba dhamana yake yeye mwenye kuwa mpumbavu na sio kubebesha wengine lawama.
hakuna kampuni inayotengeneza faida kwa kuangalia makampuni makubwa iliyowahi kutoa malalmiko kama haya, sasa huyu ni nani? hawa wanaoajiriwa na wengine wamesomea wapi?
lipo tatizo la sometimes mtu anapopata nafasi yeye anadhani anajua kila kitu hivyo kama ni interview ataendesha yeye. na ujinga huu umewapotosha wengi kwa maana kila mtu anapekua vitabu na makablasha kutafuta swali na jibu.
elimu ya mtu inachangiwa na mambo mengi sana lakini kila mwajiri ajitambue yeye kwanza badala ya kukimbilia kubebesha wengine lawama.
Nilikuwa kwenye ukurasa mmoja tunajadiliana hatua ya bunge la Tanzania kupitisha sera inayotia ugumu kwa waajiri kuajiri watu kutoka nje ya Tanzania. Katika majadiliano baadhi ya waajiri wakawa wanatoa misimamo yao, wengi walionesha kutokuwa na imani na wahitimu wa vyuo kutoka Tanzania. Hakika points wanazosimamia ni za ukweli, wahitimu wengi wanaakisi sura ya mazao duni vyuoni mwetu.
======================
======================